Pesa Inaleta Dharau Bongo Movies-Cloud

Msanii mkongwe wa bongo movies nchini Cloud, amefunguka na kuongelea sababu ya kuwa na mikwaruzano mingi  ndani ya bongo movies.Kwa kipindi kirefu baadhi ya wasanii wa bongo movies wamekuwa wakirushiana maneno  binafsi ambayo kwa namna moja au nyingie hayajengi kabisa tasnia hiyo, moja ya wasanii hao ni Duma pamoja na Gabo ambao wamekuwa  wakipeana maneno ya kashfa kuhusu maisha binafsi,

Akiongea na eNews ya EATV, Cloud amefunguka na kuweka bayana baadhi ya mambo yanayovuruga bongo movie, ambapo anasema kuwa zamani kulikuwa na upendo na umoja kwa sababu watu walikuwa wanafanya maigizo bila kulipwa lakini baada ya kuanza kuigiza filamu watu wanajipatia vipato wanaanza kuonana mmoja ni mkubwa kuliko mwingine.”zamani wakati watu wanaigiza alafu hawalipwi pesa pale umoja ulikuwa unapatikana, watu walikuwa wanalipiana hadi nauli  ya daladala,lakini baada ya kuanza kufanya filamu watu wameanza kupata hivi visenti watu vimeanza kuwatia dharau, lakini baada pesa zikaanza kuwatoka kwaiyo mtu akawa akipata deal hataki kumshirikisha mwenzie kwa sababu ya wivu”

download latest music    

Clouds anafunguka na kudai kuwa bongo movie watu wengi sana ni maadui na hawapatani kabisa , kumekuwa na uadui mkubwa na anakiri hata yeye wapo watu wanaomchukia sana anawajua lakini anawaombea kheri tu,”kuna vitu vingi vipo ndani ya pazia kuhusu bongo movies,ni vigumu kuelezea kwanini watu hawapatini, na ni kweli watu hawapatani , hata mimi nina maadui wengi katika bongo movies” aliongezea Cloud

hata hivyo katika kumalizia kwake, clouds alitoa ushauri kuwa inabidi watuwaanze kujielewa na kujikubali ilikutatua matatizo yaliyopo katika bongo movies,”tatizo kubwa mbali ya yote niliyoyaongea ni kwamba tunakosa elimu ya kazi tunayoifanya, na tunakosa uelewa wa position tulizonazo, lakini kama tutapata elimu ya kazi na position tulizonazo nina imani izi figisu figisu zinazokuwepo hazitakuwepo tena” aliongea Cloud

hata hivyo Cloud anasema kuwa umaski wa wasanii wengi ndio unaofanya bongo movies kuvurugika, na umasikini ndio unaofanya watu kuoneana wivu na kuchukiana katika tasnia.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.