Povu la Shilole Kwa Media Zinazompa Kiki Lynn

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole ametoa Povu zito kwa media ambazo amedai zimekuwa zikitoa Kiki za bure kwa watu ambao hawana vipaji na sio wasanii.

download latest music    

Watu wengi wamekuwa wakihoji kuhusiana na mafanikio ya ghafla na umaarufu wa video vixen Irene Hillary maarufu kama Lynn huku wengi wakitaka kujua ni kazi gani hasa anazifanya na kumpatia pesa alizonazo pamoja na mali.

Shilole ameamua kufunguka kuhusiana na media zinazompa air time officiallynn na kuuliza wadau ni kitu gani hasa amekifanya kwenye jamii mpaka kinawafanya wampe nafasi sana.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shilole alimwaga Povu hilo na kuandika:

Tuseme ukweli huyu dada anafanya kitu gani mpaka mwandishi aseme anatreand je anafanya movie ni mwanamuzik na amefanya nini ktk jamii ? Jamani waandishi wa habari kuweni makini ndio maana mnatuletea mambo ya akina Amber Rutty”.

Watakuja kuchafua sanaa yetu tuonekane wote wapumbavu kwa ajili ya mtu mmoja anapewa promo ya kijinga ili wapate habari Alafu wanaweka YouTube bila kujali mnazalilisha tasnia yetu wandishi wengine shame on you”.

Lynn alijizolea umaarufu Baada ya mahusiano na Diamond Platnumz ambapo miezi michache iliyopita Msanii huyo alimnunulia mrembo huyo gari kwenye birthday yake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.