Quick Rocka Afungukia Mahusiano na Kim Nana

Msanii wa muziki wa Bongo fleva  nchini Aboot Rocka maarufu kama Quick Rocka amefunguka kuhusu  mahusiano na mrembo ambaye ni video queen Lilian Kessy maarufu kama Kim Nana.

Kim Nana alijizolea umaarufu miezi michache iliyopita Baada ya kusemekana kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na staa wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz.

download latest music    

Quick Rocka ameibuka na kukana kuwa kwenye mahusiano na mrembo huyo na kusisitiza kuwa mahusiano pekee aliyokuwa naye ni urafiki wa kawaida sana.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Quick Rocka amefunguka haya:

Ni kweli namfahamu Kim Nana kama mtu niliyekuwa nafanya naye kazi tu lakini hakuna mambo ya mapenzi kabisa.”

Tetesi za Kim Nana kutoka na Quick Rocka zilianza baada ya msanii huyo kuonekana anamposti mrembo huyo mara kwa Mara kupitia ukurasa wake wa Instagram.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.