Rammy Awajibu Wanaomwambia Anaringa
Msanii wa bongo movie Rammy Galis amefunguka baada ya kuulizwa kuhusu baadhi ya wasanii wenzake na mshabiki wake pia kumwambia kuwa ana ringa sana na pia amekuwa ni moja kati ya wasanii wenye dharau sana kwa watu.
Rammy Galis anajitetea na kusema kuwa hakuna kitu kamma hicho ingawa hata yeye alishawahi kusikia watu wakimuongelea hivyo lakini ukweli ni kwamba labda kutokana na muonekano wake na pia kutokana na tabia yake ya kukaa kimya sana ndio maana watu wanakuwa wanampa hizo tuhuma.
mara nyingi sana nimekuwa nikisikai watu wakisema kuwa eti mimi nalinga au nina dharau sana kitendo ambacho kina nikera sana , kwa sababu mimi sipo hivyo labda ukimya wangu sijui lakini siko hivyo wanaona nina kaa kimya ndivyo nilivyo.-Alisema rammy aliokuwa akiongea na GPL