Ray C Amuonya Nandy Kutumia Nyimbo Zake Kwenye Show

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva ambae kwa muda takribani miaka minne alikuwa kimya kutokana na athari alizozipata kwa matumizi ya madawa ya kulevya Rehema Charamila maarufu kama Ray C ameibuka na kuwalalamikia wasanii ambao wamekuwa wakitumia nyimbo zake katika show bila kumshirikisha  au kumnifaisha na chochote kutoka katika nyimbo hizo,

Msanii huyo aliandika maneneo hayo katika ukurasa wake wa instagram akimlenga zaidi msanii wa kike ambae pia kwa sasa anafanya vizuri katika tasnia ya muziki , Nandy ambae amekuwa akiimba nyimbo za Ray C katika matamasha ya Fiesta ambayo yanaendlea kwa sasa yakizunguka nchi nzima, Nandy amejuwa ni moja wa wasanii amabo huimba nyimbo za wasanii wengine majukwaaani huku wakibadilisha kidogo muonekao (melody)wa nyimbo hiyo.kumbe swala hilo limemkwaza msanii menye nyimbo hizo.

download latest music    

Ray C aliandika”jamani hii tabia sio nzuri kabisaa!! sijafa bado, kama mnaona umuhimu wa  sauti yangu kwenye shoo zenu muwe mnaniitaga basi,sina cancer ya koo kushindw kuziimba  hizo nyimbo!! nandy hii ni mara ya mwisho ukipanda fanya kazi zako.hii ni mara ya pili ujue, mashabiki zangu hamuwatendei haki, idont like it! sipendi maana hata tukigongana  muda mwingine hata salamu hamnipi , staki maozea ‘niliimba tusitafutiane pisha sio presha tena’#sipendiunafki #nawewetena #mnaninilakini #kilamtuapaterizikiyakeyajasholake” aliandika Ray C

Ray c ambae analalamika na kuona kuwa wasanii wenzie wanakuwa kama wanafaidika na nyimbo zake wakati yeye mwenyewe yupo na anauwezo wa kuimba nyimbo zake, ivyo waache kuimba kama wanataka shoo za nyimbo izo basi waangaike kumtafuta na kumualika katika shoo ilia akutane na mashabik wake mwenyewe.Kitu kingine kinachomkwaza Ray C ni jinsi ambavyo baadhi ya wasanii wanapokuta mitaani huwa wanashindwa hat kusalimiana.

Rehema Chalamila ni mmoja wa wanadada wa zamani waliokuwa wakitumia sauti na kiuno chake vizuri katika muziki na alikuwa akiitwa’ kiuno bila mfupa’  baadhi ya nyimbo zake ni  Uko wapi,Sogea sogea, Wanifuata nini na hivi karibuni alitoa wimbo unaojulikana kama Unanimaliza ikiwa ni wimbo wake wa kwanza tangu arudi katika game la muziki baaada ya kukaa kwa muda mrefu.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.