Rayvanny Agoma Kufuta Wimbo wa Mwanza Kwenye Mitandao
Licha ya kwamba msanii Rayvanny alitakiwa kuufuta wimbo wake wa mwanza ambao umetangazwa na BASATA kuwa hauna maadili yoyote katika jamii na kuamuliwa kufutwa katika mitandao ya kijamii lakini bado msanii huyo mpaka muda huo wa saa moja hakuwa amefuta wimbo ho zaidi ya kutoa shukrani kwa mashabiki wake kuufanya wimbo huo kuwa namba moja katika trending ya mtandao wa you tube.
Rayvanny na Diamond walitakiwa kuufuta wimbo huo uliotoka siku chache baada ya Basata kuhakikisha kuwa wimbo huo haupaswi kusikiliza katika eneo lolote kwa sababu una hamasisha maswala ya kingono ambayo ni kinyume na maadili ya kitanzania.
Wimbo wa Mwanza mpaka sasa umeingia katika trending na kuwa -viewed na watu zaidi ya milioni 1 ndani ya siku mbili.