Rayvanny Awashangaa Wanaomtuhumu Kujichubua

Msani Ray Vanny amekanusha taarifa za mitandao na kurasa za udaku kuwa kwa sasa ameanza kujichubua.

Akiongea na waandishi wa habari wa  Ijumaa Wikienda, Rayvanny alisema kuwa anashangaa maneno hayo yanatoka wapi kwani katika maisha yake haja­wahi kuwaza kufanya hivyo na anachoamini yeye watu watakuwa wanaongea kwa sababu ya muonekano wake kwenye picha.

download latest music    

“Jamani mimi hizo tabia nimezianza lini tena? Yaani walimwengu hawakosagi cha kusema, unajua kuna picha ambazo zikitupiwa mtandao­ni naonekana mweupe sana na nyingine zinakuwa zime­toka vibaya, hapo watu ndiyo huanza kusema nimejichibua, kitu ambacho siyo kweli,” alisema Rayvanny.

Hivi karibuni msanii huyo aliposti picha kwenye akaunti yake ya Instagram akiwa ana­toka kwenye mahojiano na moja ya vyombo vya habari hapa nchini, ambapo picha hiyo ilionesha magoti yake ni meusi tofauti na sehemu nyingine za mwili wake hivyo kuwafanya wadau kudhani amejichubua.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.