Rayvanny Awasihi Wasanii Wenzake Kusaidi Wagonjwa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB, Rayvanny ameibuka na kuwapa wasanii wenzake ambapo amewataka kuwa na moyo wa kusaidia wagonjwa ambao wapo mahospitalini.

Rayvanny amefunguka na kutoa ujumbe wa kuhamasisha watu wasanii na Watanzania wengine waweze kujitoa japo kidogo ili kuwasaidia wagonjwa wanaosumbuliwa na maradhi mbalimbali Hospitalini.

download latest music    

Rayvanny amefunguka hayo baada ya kutembelea katika Hospitali ya Muhimbili kumjulia hali mama  aliyekuwa anasumbuliwa na jicho kutoka Mbeya, ambaye wiki iliyopita video zake zilisambaa mtandaoni zikimuonesha akiomba msaada wa matibabu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rayvanny ameandika;

Nashukuru Mungu Leo Nimepata Nafasi Kutembelea Hospitali Ya Muhimbili, Kumuangalia Yule Mama mwenye tatizo la jicho. Kwangu Leo imekua kama darasa na Sehemu Ya kujifunza, kutokana na Hali Ya ndugu zetu pale Hospitali.Nilienda Kwa Ajili Ya Yule Mama lakini nikajikuta naenda Kwa Wodi Nzima…. KIDOGO NILICHOKUA NACHO NIKASAIDIA WODI NZIMA…. Maana Ya Mimi kupost Sio kujikweza Ila nikukumbushana Kwa Kidogo Tunachokua nacho Tusiache kusaidia ndugu zetu wenye Magonjwa,Matatizo mbalimbali na Wasiojiweza…. MUNGU AWABARIKI”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.