RC Makonda Aagiza Harmonize Akamatwe Kama Anavuta Bangi

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda ameagiza Msanii wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Harmonize Akamatwe kama atakutwa na hatia ya kuvuta bangi.

Makonda ameyasema hayo siku ya jana katika mkutano Wake aliyofanya na wasanii mbali mbali wa Bongo fleva na Bongo Movie ambapo amekemea matumizi ya madawa ya kulevya.

download latest music    

Makonda ameweka wazi kuwa serikali inafanya kazi kubwa ya kupambana na matumizi ya madawa ya kulevya na hivyo haitawavumilia watu ambao watasika kujiingiza huko.

Makonda ameweka wazi anataka Harmonize achunguzwe kama anatumia bhangi kama anavyoonekana kwenye pich zake kwenye Mitandao ya kijamii na kama kweli basi Akamatwe awekwe Ndani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.