Rommy Jones Adai Mwanamke Pekee Anayemfaa Diamond ni Zari

Kaka wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Rommy Jones ameibuka na kudai mwanamke pekee  anayemfaa mdogo wake ni Mpenzi wake wa zamani na mzazi mwenzake Zarinah Hassan ‘Zari’.

Mahusiano ya Diamond yameendelea kutengeneza headlines Kwenye mitandao ya kijamii hasa sasa kutokana na warembo wawili ambao ni Kim Nana na Lynn kuonekana kugombani Penzi la staa huyo.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Rommy Jones, amefunguka kuwa mke pekee ambaye anamfaa mdogo wake huyo ni mzazi mwenziye Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’.

Nasema ukweli ndani ya moyo wangu, Zari ni mwanamke ambaye anafaa kuwa mke na kuwekwa ndani kwa sababu anajielewa na anasimama kama mama kuanzia kwenye ulezi wa watoto wake na kila kitu ndani ya nyumba”.

Rommy amesema anatamani Zari awe shemeji yake wa maisha na ikiwezekana wafunge ndoa kwani ana kila sifa ya kuwa mke na ndiye mwanamke pekee anayeweza kumuweka sawa mdogo wake na akaenda kwenye njia sahihi.

Unajua kila familia ingependa sana kuona mtoto wao anapata kitu kilicho bora, yaani mke ambaye anaweza kusimama vyema kama mama hivyo mimi leo nikiamka Diamond aniambie anamuoa Zari, nitafurahi sana kwa sababu najua atakuwa amepata kilicho bora kabisa”.

Lakini pia Rommy hakusita kuwaongelea Lynn na Kimnana ambapo amesema;

Unajua Diamond kwa hao (Lynn na Kim Nana) ni kama tu zile za mwanaume kutenda kosa na kuchepuka nje, lakini akawa na msimamo na mwanamke wake, kwa hiyo kwa hao siwezi kumuongelea sana kwa sababu pia sisi hata siku moja hatukai na kujadiliana naye mambo yake ya kimapenzi, ila ukizungumzia mke, basi nitakuambia ni Zari tu”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.