Rosa Ree Atoboa Siri Ya Kuzidi Kufanikiwa

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa kwa staili yake ya kuchana mwanadada Rosary Robert ‘Rosa Ree’ ametaja siri ya mafanikio yake.

Rosa Ree ni moja ya msanii ambaye amepata umaarufu kutokana na staili yake ya kipekee kabisa ya kuchana inayomtofautisha na wasanii wote wa Bongo fleva.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake na gazeti la Risasi Vibes, Rosa Ree alisema kuwa, siri hiyo ni namna ya uimbaji wake kwani haujakaa Kibongo sana na anajiweka ‘kimtoni’ zaidi ndiyo maana anafanikiwa.

Ukiwasikiliza wanamuziki wa kike wa Bongo, wengi wanavyorap ni ‘local’ ndiyo maana hata hawatusui kama mimi, kikubwa aina yangu ya uimbaji inanifanya kupata mashabiki wengi zaidi nje ya Bango”.

Rosa Ree anayeendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Way up’ amezidi kupata mafanikio zaidi kwani wiki chache zilizopita alitangaza kupata uongozi mpya kutoka South Africa ambao umemzawadia mijengo miwili huku mmoja wa Bongo ukiwa na thamani ya milioni 400.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.