Ruby afunguka kwa nini alimtema Soudy Brown wa Cloud FM

Ruby alikua mpenzi wa Soudy Brown (mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu cha Clouds FM) kwa muda wa miaka mbili. Mrembo huyo amefunguka kuhusu mahusiano yake na mtangazaji huyo.

Ruby alisema kuwa Soudy Brown ndiye mwanaume pekee kutoka kwenye industry ya muziki ambaye yeye amewai kuingia kimapenzi naye.

download latest music    
Ruby

Mrembo huyo alifunguka na kusema kuwa aliamua kumwacha Soudy Brown kwa sababu aliona mtangazaji huyo hakuwa na msimamo.

“Nikisema nitoke na mastaa wenzangu sio kwamba hawanisumbui wananisumbua sana lakini nawajua tayari the way walivyo. Lakini vitu vingi ambavyo naona wanafanyiwa wasanii wenzangu na mimi kweli nikawe na msanii? Hapana siwasemi kwa sifa mbaya wasanii lakini mimi siwezi kuisha nao kutokana na tabia zao kwa sababu mimi ni mwepesi sana kuumia. Mimi mwanaume ambaye nimetoka naye kwenye mapenzi na yupo kwenye industry yetu only ni Soudy Brown, na nimeishi naye kwa mwaka mmoja na miezi sita,” Ruby aliuambia mtandao wa Spin Tanzania.

 

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere