Ruby Azunguzmia Swala la Kuwa Mjamzito
Mwabadada Rubby ameamua kumuweka wazi mpezi wake anaesme akuwa amekuwa nae katika mahusiano kwa muda wa zaidi ya mwaka sasa na haoni hasara kumuanika na watu wamuone.
Akiongea katika FNL na Sam misago,Rubby anasema kuwa watu wamekuwa wakimuuliza sana kuhusu muonekano wake wa sasa na kwamba anaonekana kama ni mjamzito ,akijibu swala hilo Rubby anasema kuwa kwa kawaida mimba haiwezi kujificha hivyo kama kweli ni mjamzito lazima muda ukifika mimba itaonekana tu.
Mwanaume huyo aliemtambulisha Ruby anajulikana kwa jina la kusa ambae pia ni mwambishi wa nyimbo za wasanii mbalimbali anasema kuwa yeye haoni shida kuweka mapenzi yao hadharani kwa sababu wamekuwa katika mahusinao ya muda mrefu.
Rubby ambae hivi karibuni alitajwa na uongzo wake kuwa wameshindwa kuelewana na kufanya kazi kwa pamoja, ni moja ya wanamuziki wazuri lakini amekuwa akishindwa kufanya kazi na menejimenti mbalimbali kwa sababu ya utovu wa nidhamu.