“Ruby Inabidi Ujifunze Kula na Kipofu”-Vanessa Mdee

Msabii wa muziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee maarufu Kama Vee Money ameibuka na kumtaka Msanii mwenzake Ruby kujishusha kwa watu na kupunguza kiburi.

Kwa muda mrefu kumekuwa na tuhuma dhidi ya Ruby kuwa ni mgumu kufanya naye kazi kwani Ana kiburi kupitiliza kwaiyo inakuwa ngumu kwa wasanii wenzake na wadau kufanya naye kazi.

download latest music    

Siku ya jana Mange Kimambi alimchana Ruby kuhusu taarifa za kuwa mjeuri na kiburi mbele ya watu wanaomsaidia na kudai Ana kipaji sana lakini hafanikiwi kwa sababu watu wengi hawataki kufanya naye kazi kwa ajili ya kiburi chake.

Vanessa Mdee naye ameibuka na kumpa ushauri Ruby na kumtaka ajishushe anapokuwa na watu ili azidi kufanikiwa zaidi.

Kupitia Instagram, Vanessa Mdee amemuandikia maneno haya Ruby:

Leo nimekutana na Ruby na tumeongea sana kuhusu hii ishu yake, Nakupenda sana Ruby tupige kazi mama kula na kipofu, kuna muda mwingine jifunze kukaa kimya halafu acha muziki wako uongee zaidi fanya kwa manufaa yako na Mtoto wako”.

Ruby anatarajia kujifungua Mtoto Wake wa kwanza muda  wowote kuanzia sasa kwani hapo alipo ana  ujauzito wa miezi kadhaa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.