Ruby- Sihitaji Makalio Makubwa Ili Kuvutia Wanaume

Mwanamuziki wa Bongo fleva Ruby anayetamba na kibao chake cha ‘Nayule’ amerudi tena katika vichwa vya habari kuhusu makalio makubwa huku safari hii akidai kutu hatoweza kutumia madawa ya kichina kuongeza makalio ili tu avutie wanaume.

Wiki iliyopita Ruby aliwashangaza watu wengi pale alipotupia picha Instagram akiwa amefungasha bonge la wowowo hali iliozua utata kutokana na kuwa ukweli unaojulikana ni kuwa Ruby ni msichana mwenye umbo dogo kwaiyo hata makalio yake huwa ni madogo kwaiyo kitendo cha kuposti picha ambayo ghafla ilimuonyesha na msambwanda mkubwa ulishtua wengi.

download latest music    

Baada ya picha hizo kusambaa na kupata attention kubwa ya wanaume huku wengi wakimsifia  akiwa na wowowo kubwa Ruby amedai kuwa hatojiaribu kwa kufanya vitu vya ajabu ili kupata makalio makubwa ili tu apendwe na wanaume.

Kwenye interview aliyofanya na Enews ya East Africa Tv, Ruby ameongea haya kuhusiana na ishu hii;

Kwa kweli watu wengi walionesha muitikio mkubwa sana baada ya zile picha kutoka inaelekea wengi sana walivutiwa lakini kitu ambacho nimejifunza kwa mashabiki zangu ni kujikubali yaani siwezi kujibadilisha ili nikubalike na watu huyu mnaeniona ndio mimi siwezi kubadilika hasa eti tu ili nipendwe na mwananume hapana huyo sio mimi”.

Ruby ambaye ametoa nyimbo yake mpya baada ya kukaa kimya kwa muda karibia mwaka mzima ameoekana kupokelewa vizuri na watu kuikubali kazi yake mpya aliyoitoa baada ya hii kiki ya makalio.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.