Sam Misago Amefunguka Baada ya Afande Sele Kudai Alimkatisha Tamaa ya Kuendelea na Mziki

Mtangazaji wa East Africa Tv na redio Sam Misago amejikuta kikaangoni baada ya Mkongwe wa mziki wa Bongo fleva Afande Sele kudai aliacha kufanya mziki kwa sababu alikatishwa tamaa na Sam Misago.

Afande Sele ni moja Kati ya wasanii wa kitambo sana ambaye hajaingia studio siku nyingi sana na alitaja moja ya sababu ya yeye kutoingia studio na kutoa nyimbo mpya ni kukatishwa tamaa na wadau mbali mbali wa muziki na mmoja kati ya wait hao ni Sam Misago.

download latest music    

Afande Sele amedai kuwa mara ya mwisho kutoa nyimbo yake ya ‘Amani na Upendo’ alishauriwa na Sam kuwa nyimbo aina ile hazina soko tena badala yake watu wanapenda nyimbo zenye swagga Kama anazoimba Diamond na wasanii wngine kitendo alichodai kilimkatisha tamaa kwani yeye anapenda kuimba nyimbo za kuelimisha watu.

Baada ya tuhuma hizo Sam Misago amefunguka kwenye interview aliyofanya na Planet Bongo ya East Africa Africa radio:

Naweza nikasema kilichotokea ni kwamba Afande Sele alinielewa tofauti alidhani niliongelea ujumbe wa nyimbo yake sikuongelea ujumbe ulikokuwa kwenye nyimbo ujumbe ulikuwa mzuri tu  ila niliongelea uwasilishwaji wa ule ujumbe wake ila ninamwambia Afande Sele akaze asikate tamaa maana gemu limebadilika tangu alipoliacha na asikatishwe tamaa kabisa na kauli yangu”.

Afande Sele aliweka wazi kuwa anarudi kwenye gemu lakini kamwe hawezi kuimba nyimbo ambazo hazina ujumbe kwa jamii hasa hawezi kuimba nyimbo zinazoongelea mapenzi, kulewa na anasa nyingine.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.