Shetta Ataja Sababu Ya Kutofautiana na Diamond

Staa wa muziki wa Bongo fleva Shetta amefunguka na kuweka wazi sababu hasa za yeye kutofautiana na msanii mwenzake Diamond Platnumz.

Shetta na Diamond mbali na kufanya kazi wote na kutengeneza hits mbali mbali Lakini pia walikuwa ni marafiki wa karibu lakini siku za hivi karibuni wamekuwa hawaonekani pamoja.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Shetta amefunguka na kusema hakuna bifu kati yake na Diamond kama watu wengi wanavyodhani bali wametangana kwa sababu za kibiashara:

Sidhani kama kuna bifu lakini mimi nafikiri biashara sababu mwanzo tulikuwa tunaishi kama washikaji lakini ikimbukwe sote ni wanamuziki ili kutafuta inabidi kila mtu apambane.

Siri ya biashara kila mmoja anataka kufanikiwa, kila mmoja anataka kuwa namba moja na kuna series za mafanikio. Automatic wewe kama mwanamuziki na sifaidiki na wewe kwa njia moja au nyingine, siwezi kukupa njia zangu na wewe huwezi kunipa njia zako lakini haiwezi kuwa kama tatizo”.

Wasanii hao wameshafanya ngoma kali kama vile Nifanganye na kerewa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.