Shilole Amjibu Ebitoke na Kudai Sio Hadhi Yake

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amemjia juu msanii wa vichekesho kutoka Timamu Tv, Ebitoke na kusema sio mtu wa hadhi yake.

Siku ya jana Ebitoke alimuongelea Shilole Kwenye Interview yake na kudai hajui nyumimbo hata moja ya Shilole kwa sababu hajui kama ni msanii au ni mama ntiliye.

download latest music    

Kwenye mahojiano na EATV, Shilole amesema hawezi kubishana na mtu kama Ebitoke kwa kuwa hana pesa na pia sio level zake na pia kama anatafuta kiki basi yeye hatoi kiki sahivi:

Nyumbani kwake ananitazama kila siku, wengine wanapenda wanisikie nikiongea, mimi siwezi kuongea na mtu ambaye hana hela, lakini wakati huo ananijua na ananiangalia kwenye tv sebuleni kwake, mimi sitoi kiki sasa hivi“.

Mbali na kuwa msanii Lakini pia Shilole ni mjasiriamali ambapo anamiliki mgahawa wake unaoitwa Shishi Food.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.