Shilole Amponda Hamisa na Kumsifia Zari

Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole Kiuno amefungukia suala la Hamisa na Zari na kuweka neno lake. Kama ilivyokuwa kwa wasanii wengi wametoa maoni yao juu ya jambo hili Shilole pia amefunguka na kuonyesha wazi yupo upande wa Zari na kumponda Hamisa.

Kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram Shilole amefunguka kuwa kitendo alichofanya Hamisa kimewadhalilisha wanawake wote kwani  amemtumia mtoto wake kutafuta kiki.

download latest music    

Shilole amefunguka;

“Mwanamke asiyejielewa ndio hutumia mwili wake kujidhalilisha na kuwatumia watoto malaika wasi na kosa kutafuta kiki. Mwanaume akikupenda atakuweka ndani atakuthamini. Kinyume na hapo mtatumiana kwa maslahi yenu binafsi. Ukiwa mwizi unakuwa hata na heshima kwa mwenye mali yake ya nini mpaka udhalilishwe na mwanaume ijulikane hupendwi ila umetumiwa tu. Vinginevyo hata huduma unayopata kwa wiki utaisikia bombani. Kwani haiwezekani mwanamke kufight na kutulia na watoto wako mpaka utengeneze drama? Hebu tubadilikeni jamani huu ni u GOLD DIGGER unatudhalilisha tu. Aggh mi nakereka tu hebu niendelee na umama ntilie wangu au sijui na mimi nitafute wababa wa watoto wangu tuanza drama”.

Kwa upande mwingine Shilole amemposti Zari na kumuonyesha yuko upande wake na anamkubali yeye. Shilole kaweka picha ya zari na maandishi “Ijumaa Kareem! Mashallah umependeza wifi”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.