Shilole Kamtosa Uchebe Karudiana na Nuhu Mziwanda

Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole amedaiwa kumtosa mpenzi wake Uchebe na kuamua kurudiana na mpenzi wake wa zamani mwanamuziki mwenzake Nuhu Mziwanda.

Uhusiano wa Shilole na Nuhu Mziwanda ulipata umaarufu kutokana na tofauti kubwa ya umri kati yao. Lakini baada ya kuwa pamoja kwa kipindi kirefu waliachana na kugeuka kuwa maadui wakubwa. Baada ya kuachana walitungiana nyimbo mbali mbali huku Nuhu Mziwanda kwenye nyimbo aliomtungia Shilole iliyoitwa jike shupa alidai kuwa alipokuwa kwenye uhusiano na Shilole  alikuwa anampiga sana tuhuma ambazo Shilole alithibitisha na wala hakukataa.

download latest music    

Miezi michache iliyopita Shilole alianza uhusiano wa kimapenzi na kijana anayeitwa Uchebe ambaye hakuwa na umaarufu wowote nikimaanisha kuwa hakuwa msanii bali ni fundi gereji lakini Shilole alisisitiza kuwa anampenda sana hadi kufikia hatua ya kutangaza kuwa wanategemea kuoana hivi karibuni na hata kusema watafunga ndoa Ulaya. Siku mbili zilizopita Shilole alienda kupiga shoo Tabora, Igunga ambako pia ni Nyumbani kwa wazazi wake na baadae aliweka picha kwenye ukurasa wake wa Instagram zikimuonyesha akiwa na Uchebe na Mama yake na kuweka wazi kuwa ameenda kumtambulisha kwa wazazi wake.

Baada ya hayo yote kutokea siku ya Jana picha zilisambaa zikimuonyesha Shilole akiwa amelala kitandani kimahaba kabisa na Nuhu Mziwanda jambo liliozua tetesi kuwa Shilole karudiana na Nuhu na kamtosa mpenzi wake Uchebe.

Hizi ni baadhi ya picha zilizosamvaa mtandaoni zikimuonyesha Shilole na Nuhu kitandani:

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.