Shilole- Mama Yangu Alinifunza Kujitoa Kwenye Matatizo Ya Wengine

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kusema Mama yake alimfunza kujitoa Kwenye matatizo ya binadamu wengine.

Shilole ambaye alijizolea sifa kubwa Kwenye msiba wa msanii wa Bongo movie Agnes Masogange ambapo alionekana akishughulika kupika chakula na wanawake wengine Kwenye msiba.

download latest music    

Shilole baadae aliweka wazi kuwa alipofika tu msibani hapo badala ya kwenda kukaa pembeni na wasanii wenzake alienda jikoni kujiunga na wanawake wengine na kuanza kupika chakula.

Shilole ameweka wazi Kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa hivyo ndivyo alivyo siku zote kwani mama yake alimfunza kujitoa kwa ajili ya matatizo ya watu wengine:

Kabla mama yangu hajafariki aliniambia sifa ya binaadamuu! Kujitoa kwa wenzio hasa Kwenye matatizo kwani raha zipo tu. Pumzika kwa amani mama yangu japo uliniacha nikiwa na miaka saba hekima zako bado nazifata”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.