“Sijazaa na Diamond Pamoja Majizzo Kwa Ajili Ya Pesa”-Hamisa

Mwanamitindo na Msanii wa Bongo fleva Hamisa Mobetto amefunguka na kuweka wazi kuwa hajazaa na Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz na CEO wa EFM kisa pesa kwani ana pesa zake binafsi.

Hamisa amesema watu wengi wakisikia amezaa na wanaume wenye uwezo kama hao basi moja kwa moja wanafikiri kuwa amefuata pesa Lakini hawajui kuwa pesa zake anatafuta mwenyewe kwa jasho lake.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari, Hamisa amekana stori za kuwa amegeuza watoto wake mtaji kwa kuishi kutegemea matunzo atakayopewa kwa ajili ya Watoto Wake na Diamond pamoja na Majizzo.

Mimi ni mtu ambaye nilikuwa najiweza vizuri tu kabla ya kuzaa na ninataka wasichana wadogo wanaoniangalia wajue kuwa kuzaa ndio kutoka kimaisha hapana sio hivyo, Nataka watu wajue kuwa sio kwamba kwa sababu nimezaa na wanaume wenye pesa basi ndio nimejirahisishia maisha hapana kila kitu nilichokuwa nacho ni jasho langu mwenyewe na nguvu zangu nimetumia kuvipata”.

Siku za nyuma Hamisa ameshawahi kusemekana kupangishiwa jumba la kifahari na baba wa Mtoto Wake Diamond Platnumz na kabla ya kuhamia hapo anadaiwa kuwa alipangishiwa nyumba na Majizzo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.