Simjui Brown, Ila Wolper Akinitaka Namkubali -Msami Baby

Mwanamuziki na dancer Msami baby kutoka nyumba ya vipaji THT amefunguka na kudai kuwa Jacqueline Wolper ni msichana mzuri hivyo akimtaka hawezi kukataa.

Msami ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji wa bongo movie Irene Uwoya baada ya tetesi kuenea kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Wolper.

download latest music    

Katika mahojiano aliyoyafanya na Bongo 5, Msami amedai kuwa hamfahamu mpenzi mpya wa wolper anayejulikana kwa jina la Brown hivo ikitokea Wolpee akamtongoza basi hatasita kuwa naye.

“Mi namjua Wolper simfahamu huyo Brown, mpenzi wa mwisho wa Wolper ninayemfahamu ni Harmonize kwaiyo Wolper ni msichana mzuri akiniambia ananipenda why not bwana?  Alafu sina haja ya kumtumia DM yaani mi namfuata moja kwa moja si ninajua kama anapatikana na yeye kama ananipenda ataniambia basi tutakua pamoja”.

Katika upande mwingine Msami aliweka wazi uhusiano wake na mwanamuziki Nandy;

“Sina uhusiano wa kimapenzi na Nandy, yule ni kama dada yangu au mdogo wangu inawezekana siku moja tukaqa zaidi lakini kwa sasa ni marafiki yaani kwa maana wote tumetokea kwenye familia ya THT kwa hiyo ni kama familia yangu”.

Msami amewahi kukiri kuwa anavutiwa na wanawake wakubwa kiumri kuliko yeye na moja ya mpenzi wake aliyemzidi umri ni mwana dada Irene Uwoya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.