“Sina Bifu na Ali Kiba Ila Kuna Watu Wanatia Chokochoko” – Diamond

Mwanamuziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz anayeendelea kufanya vizuri na albamu yake mpya ya ‘A boy From Tandale’ amefunguka na kusema hana tatizo na Ali Kiba ila kuna watu wanataka kuwagombanisha.

Diamond na msanii mwenzake wa Bongo fleva Ali Kiba wamesemekana kuwa na bifu kwa muda mrefu sana huku kila mmoja akikataa pembeni kuwa hana bifu na mwenzake lakini vijembe wanavyorushiana vinasema vingine.

download latest music    

Tetesi za wasanii hawa kuwa na bifu zilishika kasi baada ya Alikiba kutoa wimbo wake wa ‘Seduce me’ na Diamond kutoa Zilipendwa kisha kuanza kurushiana maneno Twitter jambo lililopelekea hadi kutukanana.

Lakini jana Kwenye Interview ambayo Diamond alifanya na LilOmmy Kwenye The Playlist alisisitiza kuwa hawana bifu ila kuna muda watu wanakuwa wnawachochea maneno maneno ili kutaka watengeneze bifu.

Unajua watu wanaweza wasiwe na matatizo ila sometimes watu wanakuwa wanatia chokochoko kati yenu na kama wanadamu zinakuja zinawa provoke na mnajikuta mnataka muingie kweli kwenye bifu, lakini baadae mkikaa mnajifikiria kuwa sisi ni watu wazima wenye akili mnajikuta mnagombana halafu wanakuja kufaidika watu wengine kwa sababu mimi kugombana na Ali hakuniongezei chochote kwenye maisha yangu”.

Diamond amesema hawezi kuwa na tatizo na Ali Kiba kwani kila mtu ana mashabiki zake hivyo hana haja ya kuwa na ugomvi naye.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.