Sina Mpango Wa Kuoa- Dully Sykes

Msanii mkongwe wa Bongo fleva Dully Sykes amefunguka na kuacha watu vinywa wazi baada ya kuweka wazi kuwa hana mpango wa kufunga ndoa pamoja na kuwa na watoto kadhaa.

Kauli hiyo iliyotolewa na Dully iliwashangaza mashabiki zake kwani ilitolewa mbele ya kadamnasi ya mashabiki.

download latest music    

Dully alifunguka suala hilo wakati akiwa jukwaani akikamua kwenye Tamasha la Komaa, lililofanyika kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, ambapo akiwa katikati ya shoo alisema kwa nguvu.

Dar es Salaam…hatupoi… hatuboi na wala hatuoiii…”.

Baada ya kauli hiyo swangwe ziliibuka kila kona na baadhi ya mashabiki walianza kuzungumza chini kwa chini juu ya kauli hiyo kwamba huenda Dully hana mpango wa kuoa kweli ndiyo maana kasema juu ya kauli hiyo.

Dully amekuwa akiulizwa kuhusu kufunga ndoa kwa miaka mingi sasa ambapo amekuwa akidai muda ukifika ataoa lakini mpaka leo bado hajaoa licha ya kuwa na watoto kadhaa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.