“Sipendi Ujinga Nikiwa na Mwanaume”-Tunda

Video vixen maarufu Bongo Anastasia Sebastian maarufu kama Tunda amefunguka na Kusema tofauti na watu wengi wanavyomfikiria yeye anaweza sana kudumu na mwanaume Kwenye Mahusiano.

Tunda amewajia juu na kuwashangaa watu wanaomuona yeye  hawezi kudumu na mwanaume mmoja, lakini ni kwa sababu hapendi kufanyiwa ujinga kisha kunyamaza kama walivyo wanawake wengine.

download latest music    

Katika mahojiano yake na gazeti la Ijumaa Wikienda, Tunda alisema sasa hivi wanaume wengi wanapenda kuwachezea wanawake kwa sababu wanawajua ni dhaifu, lakini wangejitambua thamani yao wala wasingekubali kupelekeshwa na wanaume.

Sijui kabisa kitu kubembeleza mwanaume ni kitu ambacho sijajaliwa kabisa. Mimi najua kupenda kama mwanaume atakavyonipenda, lakini mambo mengine hapana, vitu vingine anatakiwa anifanyie mimi kama mwanamke wake”.

Siku za hivi karibuni Tunda alidaiwa kumwaga mpenzi wake wa Miezi kadhaa Casto Dickson na kuanzisha Mahusiano na Jamaa mwingine lakini juzi Tena ameonekana na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.