Sister P Kurudi Tena Kwenye Bongo Fleva

Msanio mkongwe wa muziki wa Bongo fleva aliyewahi kusambaa Kama mmoja wa Wasafi wanaochana miaka ya hiyo Happy Pela ‘Sister P’ ametangaza kurudi tena kwenye gemu.

Sister P ametangaza Kurudishwa kwenye gemu na mwanadada Matata ambaye ameamua kumsimamia ili aonyesha kipaji chake cha kuchana alichokuwa nacho tangu zamani.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Sister P anayetamba na Ngoma ya Tingisha alisema kuwa, kipaji anacho sana ila alikuwa hana mtu wa kumuinua na kumsimamisha hivyo anamshukuru sana Matata kwa kumfikisha alipo.

Yaani naamini hata upoteeje Mungu anaweza kukuibua kivingine kabisa kama alivyomleta Matata, yaani hapa nilipo niko vizuri kabisa na hata kama nilipotea kwa kukosa muongozo sahihi huyu dada ameniinua vilivyo kabisa“.

Miaka ya nyuma Sister P aliwahi kutamba na ngoma yake inayoitwa ‘Anakuja’ lakini alijizolea umaarufu zaidi Baada ya kuwa na Bifu na msanii mwenzake anayeitwa Zay B.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.