“Situmii Mwili Wangu Kama Kitega Uchumi”- Poshy Queen

Mrembo anayekimbiza kwenye Mitandao ya kijamii kwa umbo lake matata Jackline Obeid maarufu kama Poshy Queen amefunguka na kusema kamwe hawezi kutumia mwili Wake kama kitega uchumi.

Poshy Queen amesema hawezi kufuata mkumbo wa warembo wengi hapa mjini ambao wamekuwa na tabia ya kujiuza ili wapate kipato kwani hata Mingu hapendezwi na tabia hizo.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la  Ijumaa, Posh Queen alisema mwili na umbo zuri amepewa kama zawadi kutoka kwa Mungu hivyo hawezi kuutumia vibaya kwani atakuwa anamkosea aliyempa.

Kuna watu wengi wananisumbua sana wakijua mimi ni kama wale, hapana, kiukweli ninajiheshimu na watu wanaonifikiria kuwa najiuza hivyo nawaambia kuwa hapa siyo mahali pake kabisa, nimeitafuta elimu ili niweze kupata kazi ya kujikimu maisha yangu mwenyewe“.

Lakini pia Poshy ameweka wazi kuwa ana Mpenzi Wake tayari ambaye amekiri anapata wivu sana kutokana na usumbufu anaopata kwa wanaume wengine.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.