Snura Afunguka Kupewa Mimba na Kibenten

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Snura Mushi maarufu kama Snu Sexy amefunguka na kuongelea Mahusiano Yake na mpenzi wake ambaye pia ni msanii mwenzake maarufu kama Minu Calypto.

Kwa Miezi kadhaa sasa kumekuwa na taarifa kwamba Snura ni mjamzito na Baba wa mtoto huyo sio mwingine bali ni kibenten cha Snura.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers Snura amefungukia Mahusiano Yake na kijana huyo na kuweka wazi kuwa wana mahusiano na kuhusu ujauzito amewataka watu wasubiri wajionee:

Tusubiri tu muda utafika tutaiona kama kweli ipo au haipo, maana mimba huwa hazijifichi itajulikana tu.

Mimi mwenyewe huwa nashangaaga watu wanadai eti natoka na kibenten, kwa sababu mimi sio mtu wa kwanza kufanya hivyo hata mtume wangu Mohammed (SW) alizidiwa umri na mkewe. Alimzidi karibia miaka 15 kwa hiyo hilo suala sio mimi wa kwanza kulianzisha sisi wenyewe tumelikuta kwa hiyo sio kitu cha ajabu.

Snura ambaye tayari ni mama wa watoto wawili alitengeneza sana headlines baada ya kujulikana kuwa ana uhusiano na Minu ambaye ni kijana mwenye umri mdogo sana kwake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.