Snura Afungukia Bifu lake na Shilole

Mwanamuziki wa Bongo fleva Snura Mushi Majanga amefunguka kuhusu uwezo wa bifu lake na msanii mwenzake wa Bongo fleva Shilole.

Kwa muda mrefu kumekuwa na habari za kuwepo kwa bifu kati ya Shilole na Snura huku siku za nyuma wasanii hao walionekana wakibishana na hata kurushiana maneno.

download latest music    

Lakini Snura amedai hivi sasa hakuna bifu kati yake na Shilole kwani mambo yaliyotokea siku za nyuma yameachwa huko na hivi sasa wameendeleea mbele

Snura alifunguka hayo Kwenye mahojiano na Bongo 5, ambapo amedai hata tuzo yake aliyopewa na Aunty Ezekiel yeye ndio alimpokelea na akampelekea.

Sina beef hadi juzi kwa Aunt mimi sindonimempokelea zawadi, yeah, hatuna bifu na nimempelekea”.

Snura kwa sasa anatamba na ngoma ‘Vumbi la Mguu’ baada ya kufunika na Zungusha ambayo alimshirikisha Christian Bella.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.