Snura Mushi aeleza chanzo cha ajali mbaya aliyonusurika

Snura Mushi amekana habari zilizoenea kuhusu chanzo cha ajali mbaya aliyonusurika. Awali iliripotiwa kuwa mrembo huyo alipata ajali kwasababu alikua akiendesha gari lake kwa kasi.

Chanzo kilichokuwa eneo la tukio kilisema kuwa Snura alikuwa kwenye mwendo wa kasi na kushindwa kukata kona iliyopo maeneo ya Cocacola Mikocheni.

download latest music    

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Snura alipinga kuwa ajali aliyopata ilisababishwa na yeye kuendesha gari lake kwa kasi.

Snura alieleza kuwa alipoteza mwelekeo kwani hakua anajua hio barabara vizuri, alisema ajali hio ilitokea kwasababu hakujua kuna kona kali mbele.

“Unajua ajali ilikuwa mbaya sana, nashukuru waliotuokoa, chanzo cha ajali ni kwamba ile barabara siijui vizuri kwa hiyo sikujua pale kama kuna kona kali ndiyo maana nikapoteza mwelekeo. Kupona au kutoka hivi salama kwenye ile ajali ni Mungu tu, maana gari liliacha njia na kupinduka, lakini mimi na mdogo wangu tulipata michubuko midogo tu mwilini na sasa hivi tunaendelea vizuri tu,” alisema Snura.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere