Steve Nyerere Aomba Msamaha kwa Ommy Dimpoz

Msanii wa maigizo nchini Steve Nyerere , amefunguka na kuamua kufunguka kuhusu swala lililokuwa limezuka na kusambaa sana katika mitandao ya kijamii kuhusu ommy dimpoz.Steve Nyerere, amefunguka na kuomba msamaha kwa Ommy dimpoz hasa baada ya kauli yake aliyowahi kusema wakati msanii huyo akiwa hospitali akiwa anaumwa.

Steve alisikika akisema kuwa Ommy Dimpoz hawezi kuimba tena kutokana na malazi yanayomsumbua na kwamba hata kama aatapona lakini hawezi kurudi katika muziki kitu ambacho baada ya ommy kutoka aliweza kujibu maneno ya watu kama Steve kwa kutoa wimbo mpya .

download latest music    

Hata hivyo , Ommy alipoulizwa kuhusu kauli ya Steve hakuonekana kukwazika sana ingawa maneno katika mitandao ya kijamii yalizidi kufanya watu kuwa na tension kubwa sana.

hivyo Steve ameamua kuomba msamaha kwa msanii huyo kwa kisema kuwa wakati anasema hakukusuduai kile ambacho wengine wamekipokea zaidi ya kuwa mitandao wamekuwa wakizidisha chumvi.

Katika ukurasa wake wa instagram alielezea maengi kuhusu kauli hiyo lakini kitu cha mwisho kabisa alikubali kosa hilo na kukiri lakini pia aliomba msamaha kwa kusema

Nakiri kukosea kutokana na ile kauli yangu zidi ya Ommy Dimpoz.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.