Sugu Aapa kuiburuza BASATA Mahakamani, Asema Wasimfananishe na Roma
Baada ya kupokea barua kutoka BASATA msanii wa hip-hop wa muda mrefu Sugu amefunguka na kuongea akiwa bungeni Dodoma anasema kuwa anaona kama BASATA wanafanya uonevu kwa sababu hata sasa wimbo huo uliofungiwa bado alikuwa anautoa rasmi bali ulikuwa umevuja lakini kitu cha ajabu ulishafunguiwa kabla haujatoka.
Lakini pia sugu amewaomba BASATA wasimfananishe na Roma ambae waliweza kumfungia na baadae kusema wamemsamehe kwa sababu waliweza kumuonea huyo.
Wimbo umevuja wao wanatoa statement ya kufungiwa,hawajawahi hata kuingia studio , hawajui hata gharama za wimbo na kutengeneza hayo,wanataka tuimbe nyimbo za matusi..mimi sio kama Roma ,,ninaiburuza mahakamani BASATA , mimi wimbo sijatoa bado ila umevuja tu , nina mawakili sita na nitawaburuza mahakamani ndio watakoma.