T.I.D Awaachie Hayo Mambo Gigy Money Na Amber Lulu -Dudubaya

Wiki iliyopita kuna picha zilikuwa zimetanda sana katika mtandao wa kijamii wa instagram ukimuonyesha msanii T,I,D akiwa kitandani na mwanamke huko wakionekana kuwa faragha, mashabiki wake walikuwa wakiiuliza kuhusu picha hizo zimetokea wapi, je kuna video mpya inakuja au vipi.

Msanii mkongwe wa bongo fleva Dudubaya ameamua kuongelea swala hilo akiwa kama mtu wa karibu wa T.I.D lakin pia kama msanii mwenzie mkongwe walioanza muziki kipindi cha nyuma kidogo,akiongelea picha hizo Dudubaya anasema kuwa kwa umri na heshima aliyonayo T.I.D  hakupaswa kufanya mambo kama hayo kwa sababu kwanza anae mtoto mkubwa  ambae endapo atakuwa ameona picha hizo itakuwa imeleta pichambaya , lakini pia akiwa kama msanii mkongwe mambo ya kutafuta kiki kwa kupiga picha za hivyo anapaswa kuwaachia kina Gigy Money na Amber Lulu, hayo mambo yeye hayamfai tena.

download latest music    

“Picha ya T.I.D  nimeiona  kimaadili sio picha nzuri kwa age yake yeye maana tayari anamtoto, Tid juniour, mimi ninamjua ni mkubwa na anajitambua kabisa, lakini pia sisi ni kizazi cha analogi, na sasa hivi ni kizazi cha digitali na kizazi cha digitali kikikuteka basi usiwe kama Amber Lulu au Gigy Money, ambao ni kizazi cha digitali, waachwe wafanye mambo yao ya kidigitali,” aliongea dudubaya

Dudubabya anaongeza na kusema kuwa ingawa kwa sasa ni lazima ufanye kitu kikupe kiki lakini hayo hayafai kwa T.ID”wasanii wengi underground wanakwambia ili uweze kujulikana lazima ufanye kitu upate kiki,..lakini unapotengeneza kiki ni lazima uiangalie je iyo kiki unayoitengeneza yupo nani nyuma yako, mama yako, babako , kuna watoto wako.’  aliongeza Dudubaya.

Inawezekana ndivyo wasanii wengi wanavyoamini kuwa katika kufanya muziki ili watu wakujue na upate jina basi ni lazima ufanye jambo la aibu ili uweze ku-trend katika mitandao, lakini kumbe sio kwa sababu unapaswa kwanza kuangalia heshima yako lakini pia kile unachokifanya kina athari gani kubwa zaidi ya kile unachokitafuta kwa muda huo.Wasanii wanapaswa kujifunza kitu kutokana na hilo.

 

Picha ya T.I.D iliyosambaa kwa kasi katika mtandao hasa wa instagram.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.