Hii ndio sababu halisi iliyomtoa Almasi Mzambele WCB

Meneja Biashara wa Baraka the Prince na Bana Music Records, Almasi Mzambele leo alizungumzia sababu halisi ya kutoka WCB.

Akizungumza kwenye show ya  Adam Mchonvu leo 20th April 2017, alieleza kwamba mambo matatu yalifanya atoke WCB;  ubinafsi, wivu na utengano.

”Any way, sikufukuzwa nimetoka, ila kuna mengi japo sijapenda tuzungumzie huko sana. Hapo kwenye ubinafsi ndio point yenyewe, ila tukaushe kwenye hilo.” – Almasi Mzambele.