Amber Lulu Akiri Kubadilishwa na Penzi La Prezzo

Video queen na Msanii wa Bongo fleva Lulu Eugene maarufukwa jina la usanii Kama Amber Lulu ameibuka na kudai Mpenzi Wake Msanii kutoka Kenya Prezzo amembadilisha tabia yake.

Amber Lulu alianza mahusiano ya kimapenzi na Jackson Makini ‘Prezzo’ mapema mwaka jana Baada ya kuachana na Mpenzi Wake wa siku nyingi Young Dee lakini wawili hao waliachana kwa miezi michache lakini sasa wapo pamoja tena.

Katika mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda,Amber Lulu alidai kuwa Prezzo alishindwa  tabia zake akaamua kukaa pembeni lakini kwa sasa amebadilika sana ndiyo maana wameweza kuwa pamoja tena.

Baada ya kubaini ugomvi wetu chanzo kikubwa kilikuwa ni tabia yangu niliamua kubadilika, nikaacha yale ambayo mwenzangu alikuwa hayapendi ndiyo maana hata kwenye mtandao wa Instagram nimebadili hata vitu ninavyotupia tofauti na zamani nilikuwa natupia picha za aibu”.

 

 

Amber Lulu Arudisha Penzi Kwa Prezzo

Video vixen na Msanii wa muziki wa Bongo fleva Lulu Eugen maarufu kama Amber Lulu Amerudisha Penzi lake na msanii kutoka Kenya Prezzo Baada ya kuchana kwa miezi kadhaa.

Tetesi za wawili hao kurudiana zilishika kasi  katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita Baada ya Amber Lulu kuposti picha ya Prezzo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

 

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Amber Lulu aliweka wazi kuwa, huko nyuma aliteswa, kuumizwa na mara nyingine kuchezea vitasa kutokana na mapenzi, lakini alipoingia kwa Prezzo alijiona yuko peponi hivyo walipoachana, aliona kuna sababu ya kurudisha mapenzi kwake.

Nilipata maumivu sana kwenye mapenzi, nilidhalilishwa na kuumizwa. Kuna wakati nilipigwa sana, yaani nilikuwa kama teja, lakini siyo wa kuvuta unga, bali ni wa mapenzi, lakini kwa Prezzo nilikuta tofauti. Nimeona nirudishe penzi kwa nguvu zote”.

Prezzo alimwaga Amber Lulu miezi michache iliyopita Baada ya picha kusambaa kwenye mitandao ya kijamii akiwa anafanya kitendo kichafu na msanii mwenzake Nuh Mziwanda.

“Prezzo Anampenda Amber Lakini Tatizo Hajatulia”- Gigy Money

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money amefungukia penzi la shoga yake Amber Lulu na mpenzi wake Prezzo.

Siku za hali karibuni kumetokea sintofahamu Kwenye penzi la Msanii Amber Lulu na mpenzi wake Msanii kutoka Kenya Prezzo ambapo imesemekana wawili hao wameachana.

Lakini utata zaidi ulitokea siku mbili hizi baada ya picha kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii iliyomuonyesha Prezzo akiwa na mwanamke mwingine wakiwa kitandani.

Baada ya skendo hiyo Amber alitumia mitandao ya kijamii kutangaza kuwa amelitua Penzi lake na Prezzo na kuweka wazi kuwa kwa hivi sasa yupo single.

Kwenye mahojiano na XXL ya Clouds Fm, Rafiki wa karibu wa Amber, Gigy Money amefunguka na kudai Prezzo anampenda Amber Lulu Lakini tatizo lake hawezi kuacha michepuko:

Yaani mshakji (Prezzo) anampenda Amber Lakini ndio hivyo ana mambo mengi yaani amefanya vitu vya ajabu sana rafiki yangu kwa rafiki yangu yaani ana mademu kibao na hivi wapo mbali basi ndio vituko kibao”.

 

Prezzo: Bado Nampenda Amber Lulu

Mwanamuziki kutoka 254 Kenya, Prezzo amezidi Kupitia penzi lake kwa aliyekuwa mpenzi wake msanii wa Bongo fleva na video vixen Amber Lulu na kudai kuwa bado anampenda.

Wiki chache zilizopita kwenye birthday party ya Amber Lulu aliweka wazi kuwa ameachana na aliyekuwa mpenzi wake Prezzo na kumtambulisha rasmi mpenzi wake mpya anayeitwa Sam.

Habari za wawili hao kuachana zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii hasa baada ya kuacha kupostiana Kwenye mtandao wa Instagram kama ilivyokuwa kawaida yao.

Prezzo alifanya Interview na FNL ya EATV ambapo yupo nchini Tanzania kwa ajili ya kutangaza rasmi nyimbo yake mpya aliyofanya na Dogo Janja inayoitwa ‘Hamsamia’.

Kwenye mahojiano hayo Prezo alikataa kukubali kama kweli wameachana bali alisisitiza kuwa bado anampenda Amber Lulu na alipoulizwa kwa nini hakumposti Kwenye birthday yake alifunguka:

Kwani unajua birthday ngapi mama yangu hajaniposti Kwenye Instagram na sio kama hanipendi ananipenda ila ndio hivyo sio lazima kumposti ndo watu wajue kama unampenda kwaiyo mimi sikumposti Amber Lulu lakini Bado Nampenda”.

Prezzo alipotakiwa kuongelea kuhusiana na Amber Lulu kumtambulisha mpenzi mpya na kusema ameachana naye alikataa kata kata na kukimbilia kubadilisha mada.

Amber Lulu Amuanika Mpenzi Wake Mpya Baada ya Kumwagana na Prezzo

Video vixen na msanii wa Bongo fleva, Lulu Eugene maarufu kama Amber Lulu amemuanika live mpenzi wake mpya baada ya kumwagana na staa wa muziki kutoka Kenya, Prezzo.

Prezzo na Amber Lulu walikuwa kwenye mahusiano  kwa miezi kadhaa ambapo mara kwa mara pamoja na penzi lao kupondwa na watu kadhaa ikiwemo kama msanii TID, lakini walisisitiza penzi lao ni la kweli na litadumu.

Lakini baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu bila kupostiana Kwenye mitandao ya kijamii tetesi zilianza kusambaa kuwa wawili hao wameachana ingawa hakuna aliyethibitisha hilo mpaka wikiendi iliyopita kwenye birthday party ya Amber Lulu.

Global Publishers wanaripoti kuwa siku ya Jumamosi Amber Lulu alifanya party ya birthday ambapo alialika watu kadhaa na moja kati ya wageni alimtambulisha mwanaume mmmoja kama Sam ambaye aliweka wazi kuwa ni mpenzi wake.

Amber Lulu na Mpenzi Wake Sam

Amber Lulu alimtambulisha mpenzi wake Sam kwa wageni waliohudhuria sherehe hiyo na kusema:

Jamani huyu ndio naniliuu wangu yeye ni mkurugenzi hapa mjini lakini sitaki kumpamba sana kwenye pati yangu hii nisije nikaibiwa buree na vidaka tonge vya mjini, naomba kwa leo mjue hivyo tu”.

“Nimechoka Kusikia Kuhusu Prezzo” – Amber Lulu

Video queen maarufu aliyegeukia fani ya muziki wa Bongo fleva, Amber Lulu amefunguka na kudai amechoka kuulizwa maswali kuhusu mpenzi wake ambaye ni raia wa Kenya supastaa anayejulikana kama Prezzo.

Amber Lulu na Prezzo walianika wazi kabisa mahusiano yao mwaka jana baada ya kukataa mara kadhaa kuwa hawana uhusiano hata mara baada ya kubambwa wakiwa wote hotelini.

Tangu hapo wamekuwa wana uhusiano ingawa Amber Lulu anaishi Tanzania na Prezzo ni mkazi wa Kenya walidai wana uwezo wa kuwa na mahusiano mazuri tu bila wasiwasi wa kitu chochote.

Lakini mahusiano yao hayakuwa ya kimya kimya kwani mara kwa mara wameharibu hali ya hewa kwenye mitandao ya kijamii kwa kuweka picha ambazo mtu mwingine anaweza kukwambia hazina maadili kwani kuna siku walirusha picha ambazo ziliwaonyesha wakiwa watupu kabisa bafuni.

Pamoja na hayo yote kila mmoja amekuwa akisisitiza kuwa wanapendana na wana mapenzi ya kweli ambapo Prezzo ameshakiri kuwa wako ‘serious’ kiasi ya kwamba ameshaenda kumtambulisha Amber Lulu kwa mama yake mzazi na kusema mama yake amempenda kiasi ya kwamba wamekuwa marafiki.

Lakini jana wengi walishangazwa pale ambapo Amber Lulu aliwatolewa povu mashabiki zake kwenye mtandao wa Instagram baada ya kumuuliza kuhusu uhusiano wake na Prezzo kwa hivi sasa ambapo Amber Lulu aliandika:

Kila saa comments zenu mnamuongelea Prezzo tu nimechoka sitaki kusikia kuhusu mtu yoyote yule kila mtu ana maisha yake na pia kila kitu kinaenda kwa muda tu hebu tutafute hela sio kila saa kuongelea mb** tu # fu**”.

Baada ya povu hilo tetesi zilienea kuwa Amber Lulu na Prezzo wameachana ingawa hakuna kati yao aliyethibitisha hilo ila sababu iliyopelekea mpaka mashabiki kumuuliza sana Prezzo ni kwa sababu ameachana kabisa kumposti Prezzo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Amber Lulu Alilia Penzi la Prezzo, Haamini Kama Amemwagwa.

Msanii wa muziki anafanya vizuri katika muziki Amber Lulu ameonyeshwa kusikitishwa na habari zinazoendelea kutambaa kuwa mpenzi wake wasasa  ambae ni msanii mkubwa kutoka Kenya amemmwaga na kutafuta mwanamke mwingine na ameshaanza kumtambulisha kwa mashabiki katika mitandao ya kijamii.

Amber Lulu anasema kuwa kama ni kweli kuhusu tetesi hizo basi Prezzo atakuwa amemkosea heshima sana kwa sababu alikuwa ameshamueka moyoni na tayari alikuwa ameshaanza kumtambulishwa kwa baadhi ya ndugu zake.

Akikiri kuwa ameshasikia taarifa za kutambulishwa kwa mwanamke mwingine Amber Lulu akiongea na moja ya gazeti pendwa kutoka GPL, anasema kuwa  kitendo hicho  kama ni kweli basi mwanaume huyo amemdhalilisha sana.

hilo la kutambulisha mwanamke mwingine nimelisikia sana,lakini kama ni kweli amemtambulisha mwanamke mwingine basi  atakuwa amenikosea sana kwa sababu  yeye alikubali nimtambulishe mpaka kwa ndugu zangu na nikafanya hivyo na nilishamweka rohoni.

Amber Lulu na Prezzo walianza kuonekana pamoja mwaka jana(2018) na baadae waliamua kuweka wazi swala laola mahusiano kwa mashabiki wao na kusema kuwa wanategemea kufunga ndoa na wala hawataachana lakini mambo yamekwenda ndivyo sivyo na sanii huyo kutoka kenya ameonekana kuwa na mwanamke mwingine katika viwanja tofauti huko kwao.

Amber Lulu Adai Kuwa Akimwagwa na Prezzo Atarudi Kwa Young Dee

Muuza nyago kwenye video au video queen maarufu aliyegeukia Bongo fleva, Amber Lulu amefunguka na kudai kuwa endapo Prezzo atamwaga basi hataona hiyana kurudi kwa Young Dee.

Amber Lulu amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Prezzo msanii maarufu kutoka Kenya kwa miezi kadhaa sasa lakini imekuwa ikionekana kuwa mpenzi wake wa zamani rapa Young Dee anahusishwa sana au anatajwa sana kwenye mahusiano hayo.

Amber Lulu na Young Dee walikuwa wapenzi kwa kipindi kirefu ambapo kutoka katika vyanzo mbali mbali vilidai kuwa Amber alimpenda sana Young Dee ingawa alikuwa anamfanyia ndivyo sivyo, kuna siku hadi rafiki wa karibu wa Amber Lulu, Gigy Money alisikiaka akisema “Amber Lulu anampenda sana Young Dee sema tu Young D mwenyewe hataki kitulia”.

Hata hivyo hapa kati Young D na Amber Lulu waliingia katika majibizano ya kwenye mitandao ya kijamii baada ya kurushiana maneno mazito ambapo kisa kilianza baada ya  Amber Lulu kumtolea povu mtu alipomlinganisha Prezzo na Young Dee na kudai asimlinganishe mpenzi wake Prezzo na vitu vya ajabu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Amber Lulu alimtolea povu shabiki wake ambaye alimhoji endapo kuwa tetesi zinazoenea mtandaoni kuwa ameachana na mpenzi wake Prezzo zina ukweli wowote, badala ya Amber luli kumjibu shabiki huyo kama jibu ni ndiyo au hapana badala yake alimtolea povu zito na kuandika “Ndiyo siku nikiachana na Prezzo lazima nitarudiana na Young Dee”.

 

Penzi La Amber Lulu Na Prezzo Sasa Ni Mubashara.

Mwanadada Amber Lulu ambae mara ya kwanza alikanusha kabisa kuwepo kwa mahusiano katika yake na msanii kutoka Kenya Prezzo  baada ya kusamba kwa baadhi ya picha zilizokuwa zikiwaonyesha wako pamoja huku ikisema kuwa Prezzo alitoka Kenya kuja mpaka Tanzania kwa ajili ya kulifata penzi la mwanadada huyo. Wawili hao hivi sasa wameshindwa kuendelea kuficha tena  mahusiano yao kutokana na picha nyingi zinazoendelea kusambaa katika mitandao wakiwa pamoja sehemu mbalimbali huku msanii Prezzo akiwa ametoa wimbo ulikuwa na maneno ya kumsifia mwanadada huyo.

Hata hivyo mwanadada huo mbae amekuwa akimwagiwa sifa kemkem kutoka kwa mwanaume huyo ameonekana kufurahi na kulewa sifa hizo katika mitandao ya kijamii.Akielezea jinsi anavyojisikia kutokana na sifa anazomwagiwa tena hasa katika wimbo  mpya ambao Prezzo ameuachia huku akisema kuwa anampenda sana amber lulu,ni mzuri na ana roho nzuri na ameshamtambulisha kwa mama yake Amber Lulu anasema kuwa kwake ni furaha kuimbwa na msanii huyo na anajiona kuwa ni msichana mzuri kukubalika na watu wa nje.

Najisikia vizuri sana kusifiwa na prezzo,  maana mtu ukikubalika mbele ya mtu fulani  lazima ufurahi kwa kweli , ni mtu wangu wa karibu na tuna mpango wa kufanya kazi pamoja.Na kuhusu uchumba na kutambulishana  kwa mama yake ilo ni swala la siri kidogo kwa sasa kati yangu na yeye ,ikifika muda muafaka basi tutawaambia-amesema amber Lulu

Amber Lulu ambae alianza kupata umaarufu wake kupitia kuonekana katika video za wasanii mbalimbali nchini  alijitahidi na kufanya jitahada zake na kuanza kufanya vizuri na kuingia katika kuimba ambako pia alikuwa na anaendelea kufanya vizuri pia.

Ingawa amepitia mahusiano mengi nyuma na watu maarufu tofauti tofautri,mwanadada huyo ambae sasa hivi ameona bora kujiweka kwa msanii kutoka kenya anaonekana kufurahishwa na penzi ilo.Amber Lulu pia ni rafiki wa karibu wa msanii wa bongo fleva Gigy Money ambae walianza kustrugle na maisha wakiwa wote na mpaka sasa hivi wako wote kama marafiki.

Amber Lulu: Hakuna Kilichotokea Kati yangu na Prezzo

Video vixen maarufu mtandaoni Amber Lulu amefungukia ishu yake na Mwanamuziki wa Kenya Prezzo na kudai kuwa hakuna chochote kilichotokea baina yao.

Amber Lulu aliongea hayo baada ya tetesi kusambaa wiki chache zilizopita baada picha za wawili hao kusambaa mtandaoni huku zikiwaonyesha wakiwa katika mikao ya kimahaba na kuleta gumzo na hata kuonekana hotelini pamoja.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na East Africa tv katika kipindi cha Friday night live Amber Lulu alifunguka kuwa hakuna kitu chochote kilichotokea baina yao hasa upande wa uhusiano wa kimapenzi.

“Watu wengine washamba lakini ni vitu fulani vya kinyamwezi tu ambapo unaweza kukaa chumba kimoja lakini msifanye kitu chochote, unajua ndege wawili wanaofanana huwa wanaruka kwa pamoja kwaiyo Prezzo ni Kama rafiki kwangu hivyo hakuna tatizo la sisi kuwa hivi tulivyo”.

Pia Amber Lulu alimalizia kwa kudai kuwa watu walizusha kuwa yeye na Prezzo walionekana hotelini pamoja kitu ambacho sio cha kweli kwani walikaa kwenye nyumba ambayo ni apartment ambapo kila mmoja alikuwa na chumba chake.