AY amwomba mpenzi wake Remy afunge naye ndoa

Ambwene Allen Yessayah maarufu kama AY sasa huyo tayari kuingia kwa ndoa. Rapa huyo amepropose kwa penzi wake Remy.

AY alijulisha watu nia yake ya kufunga ndoa na Remy wakati alihudhuria harusi ya Professor Jay. Nduguwe Jay alisema kuwa AY alimwambia anataka kumoa Remy.

Remy na AY wakiwa kwa harusi ya Professor Jay

“Muda uliopita nilikuwa naongea na AY hapa akawa ananiambia na yeye soon anafunga ndoa na mpenzi wake. Kwa hiyo mimi naweza kusema kila kitu kinakuja kwa wakati,” Black Rhyno aliambia Bongo5.

AY alimwomba Remy afunge naye ndoa siku chache baada ya harusi ya Professor Jay. Tazama video hapo chini: