Barakah The Prince Adai Bado Yuko Juu Kimuziki

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince ameibuka na kudai kuwa hajashuka kimuziki kama ambavyo imekuwa ikidaiwa kwenye Mitandao ya kijamii.

Barakah alikuwa amesiniwa chini ya staa wa Bongo fleva Ali Kiba Kupitia Label yake ya Rockstar 4000 lakini Barakah alijitoa kutokana na kutofautiana na uongozi Wake.

Baada ya kuachana na Label hiyo Barakah amekuwa hana hit song kama zamani na pia amedaiwa kuwa amefulia kimuziki pia kumaanisha hajapata wimbo uliosumbua redioni kwa miaka kadhaa sana.

Katika mahojiano aliyofanya na kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Barakah amekataa Tetesi Za yeye Kufulia na kusema kuwa hakufulia bali aliamua kupumzika na kuwapa nafasi wasanii wengine:

Mimi sijashuka kimuziki Lakini nilikaa pembeni ili kuwapisha wasanii wengine wachanga ili waweze kuonekana, na pia sitaki kukibaliana na usemi kuwa nimeshuka bali nimerudi rasmi na hata ukiangalia hapo nyuma ngoma nilizokuwa natoa nilikuwa siendi kwenye media nilikuwa natoa kwenye Mitandao ya kijamii”.

 

Baraka The Prince Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma Za Utapeli

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amedaiwa kuelekeza chini ya ulinzi siku ya Leo kwa kile kinachotajwa ni utapeli ambao Msanii ameufanya.

Siku ya jana kuna video ilisambaa kwenye Mitandao ya kijamii iliyomuonyesha Barakah akiwa anabishana na maaskari ambao walikuwa wanamkamata na mara moja ilisemekana aliwekwa chini ya ulinzi na kupelekwa kituoni.

Stori za chini ya kapeti zinadai kuwa Barakah aliokuwa polisi Baada ya kudaiwa kufanya utapeli ambapo inadaiwa alimtapeli mdada mmoja kiasi Chan shilingi milioni tano kwa ahadi ya kumpa Penzi Lakini Baraka aliishia kuchukua pesa hiyo na kununua gari.

Ulipofika muda wa kumpa Penzi mdada Yule ambaye alikuwa amemzimikia msanii huyo alimpa taarifa kuwa yeye hawezi kuwa naye kimapenzi kwa kuwa yupo na Mpenzi Wake Naj, taarifa hizo zilimvuruga mdada huyo ambaye alihisi ametapeliwa kwani aliishia kumuitia polisi ambao walimtia Ndani.

Hii n video ambayo inamuonyesha Baraka alipokuwa anatiwa mbaroni:

Barakah The Prince Afungukia Tetesi Za Kufilisika

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefunguka na kuongelea tetesi zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa amefilisika.

Tetesi hizo zimezidi kupamba Moto sasa hivi kwa sababu Barakah ameonekana kukonda kupita maelezo hali iliyopelekea wengi kufikiria huenda ni kwa sababu ya maisha magumu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha XXL ya Clouds Fm, Barakah amesema kuwa yeye hajawahi kuwa tajiri na hivyo kwasasa ndio ameanza kuitafuta hela yake kwa kuanza kufanya kazi zake mwenyewe huku akidai kuwa yeye sio msanii wa kuweka maisha yake hadharani.

Mimi ni mmoja ya wale artist sipendelei   sana kuweka hadharani hali  ya uchumi wangu au maisha yangu na ndio maana ni vigumu mtu kujua kama niko sawa Kiuchumi au nimeshuka Kiuchumi kwasababu nina Personal life so naamini pia pesa inatautwa nikiitafuta inakuja na inaweza yakatokea matatizo ikatumika labda vibaya”.

Na sio kama tatizo kubwa sana kwasababu hata makampuni makubwa huwa yanayumba, matajiri wapo wengi kuliko hata mimi na mimi sijawahi kuwa tajiri labda nimefilisiki sijawahi kuwa na hela mimi sasa hivi ndio nataka labda niitafute hela sasa now ndio naenda kuitengeneza hela yangu, kwanza niko nafanya kazi zangu mwenyewe kwasababu mi sio yule artisht wa kuonyesha maisha yangu”.

 

Barakah The Prince Afunguka Mazito Kuhusu Ruge

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefunguka mambo mazito sana kuhusu Mkurugenzi wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba Baada ya kuugua.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Barakah The Prince amefunguka mazito juu ya mchango wa Ruge kwake na katika muziki Wake na kumtakia kheri:

https://www.instagram.com/p/Bqow-5Nh8fC/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=11rvm40wvfi6z

“Naj Hakujua Kama Nabadilisha Dini”- Barakah The Prince

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince ameibuka na kudai Mpenzi wake Naj hakuwa na taarifa kuwa amebadilisha dini.

Barakah amefunguka hayo Baada ya tetesi kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Barakah amebadili dini kisa mpenzi wake Naj ambaye ni  Muislamu.

Katika mahojiano yake na mtandao wa Dizzim Online, Barakah ameweka wazi kuwa alipofikia uwamuzi wa kubadilisha dini hakumshirikisha mpenzi wake Naj mpaka zoezi lile lilipokamilika:

Ni kweli kabisa nimebadili dini kutoka ukristo na kuwa Muislamu na hivi sasa naitwa Abdulmalik na nilifanya kwa maamuzi yangu mwenyewe kwa sababu mimi sio wa kwanza, kuna ndugu zangu kibao kwenye familia yangu wamekwisha badilisha dini na Naj mwenyewe hakujua kama nimebadilisha dini mpaka alivyoona mtandaoni, nilimficha sikutaka ajue”.

Taarifa zilisambaa Kuwa huenda Barakah aliamua kubadilisha dini ili apate kufunga ndoa na mpenzi wake huyo ambaye anaishi majuu kwa sasa.

Barakah The Prince Adai Ali Kiba Anampotezea

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince ameibuka na kudai Msanii mwenzake Ali Kiba amekuwa akimpotezea na kukataa kujibu meseji zake anazomtumia.

Sakata kwa Ali Kiba na Barakah The Prince lilianza mara baada ya Barakah kuamua kujitoa katika label ya Ali Kiba Ya Rockstar 4000 kwa madai ya kutosimamiwa vyema na kazi zake kuthaminiwa.

Lakini baada ya kutoka kwenye Label hiyo Barakah aliitupia tuhuma nzito na pia kumtuhumu Ali Kiba kwa kufanya kila njia kumharibia muziki wake ikiwemo kumfutia Chanel yake ya Youtube na kufuta nyimba anazotoa ili asifike mbali.

Tuhuma hizo hazijawahi kujibiwa na Ali Kiba lakini Barakah baadae alienda kuomba radhi kwa maneno hayo, Lakini sasa Barakah ameibuka na kudai amekuwa akijaribu kumtafuta Ali Kiba lakini meseji zake hazijibiwi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo,Barakah amefunguka haya kuhusu jitihada zake za kutaka kumtafuta Ali Kiba.

Nilishawahi kumtext nikamwambia brother kuna hichi na hichi na haya ni maisha na haya mambo ambayo yanayoendelea tuachane nayo tudeal na maisha mengine, mimi bado ni kijana nahitaji muongozo wao ili nifanikiwe”.

Barakah amefunguka na kusema pamoja na kumtumia meseji Ali Kiba meseji na kutojibu Lakini pia alimtumia meseji ya msamaha Seven Mosha, Kidboy na Mgagulah ambao wote hawakujibu.

Barakah Adai Baada Ya Kusoma Biblia na Quran Ameamua Kuwa Muislam Ili Kuwa Karibu na Mungu

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefungukia uamuzi wake wa kubadilisha dini kutoka kuwa mkristo na sasa kuamua kuwa Muislamu.

Barakah amedai kuwa maamuzi hayo ya kubadilisha dini hawakuwa ya ghafla bali yalichukua  muda mrefu hadi kuyatekeleza.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, amesema kuwa amejitahidi kusoma Biblia na Quran na akaja kubaini kuwa Uislamu ndio dini yake pekee kwa sasa ambayo itamuweka karibu na Mungu.

Baada ya kusoma biblia sana na kusoma Quran sana kukawa kuna vitu nikawa nimeipenda dini ya kiislamu Lakini pia naamini Mungu ni mmoja na tunamuamini Mungu mmoja tofauti ni dini tu”.

Lakini pia Barakah ameweka wazi kuwa pamoja na kubadilisha dini na kuwa Muislamu na kuupenda zaidi Uislamu lakini bado anasoma biblia kwani anataka kumjua Mungu zaidi na kuwa karibu naye.

Siku za nyuma baada ya Barakah kubadilisha dini na kuwa muislamu kuna tetesi zilidai kuwa alibadili dini kwa ajili ya mpenzi wake Naj ambaye ni Muislam taarifa ambazo Barakah alizikataa.

Barakah The Prince Ajibu Tuhuma Za Kuwa na Kiburi

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefungukia tuhuma ambazo amekua akirushiw ili nyingi kuwa ana kiburi.

Mashabiki wengi wa muziki wa Bongo fleva wamekuwa wakimtuhumu Barakah The Prince kwa kudai kuwa ni mtu ambaye ana kiburi hasa kwa mashabiki wake.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Barakah amefunguka kuwa yeye sio mfuatiliaji mzuri wa comments za mashabiki wake kwenye mitandao ya kijamii na kuhusu madai ya kuwa ana kiburi ameeleza kuwa wanamkosea sana Mwenyezi Mungu kwani wanaamini vitu ambavyo hawaambiwa bila kuthibitisha.

Mimi sio msamaha sana wa comments za mashabiki maana naamini ukisikiliza maoni ya watu unaweza ukachanganyikiwa mwisho wa siku unatakiwa ufabye kitu ambacho unajua kitakuwa Kiba faida kwako kuliko kufuata matakwa ya watu.

Unajua watu wanaamini wanachokisikia kuna kundi Dogo la watu linalowaaminisha watu wengi kuwa mimi mjeuri jambo ambalo sio la kweli kwani mashabiki wangu wa kweli wanajua mimi siko hivyo kabisa”.

 

Diamond Ndio Msanii Mwenye Mafanikio Yanayoonekana- Baraka The Prince

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Sina’ Barakah The Prince amefunguka na kumtaja Diamod kama Msanii Mwenye mafanikio ambaye yanaonekana.

Barakah amemtaja Diamond baada ya kuulizwa kuhusu wasanii mwenye mafanikio ambapo amekiri kuwa wasanii kadhaa wenye mafanikio sana lakini Diamond ndiye anayeonekana kufanikiwa zaidi.

Kwenye mahojiano na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Barakah amesema wasanii wenye mafanikio wapo wengi lakini hajui mkwanja wao benki au hawajionyeshi sana lakini Diamond anaonekana wazi kabisa:

Wasanii wengi wana mafanikio wakina Ali Kiba, AY, Joti, Masanja, sitaki kujudge kama Diamond ndio Msanii wa kwanza kwa sababu sijui akaunti yake lakini kwa nje kila mtu anaweza kuwa na mtazamo huo kwa sababu anafanya vitu vinavyoonekana katika jamii”.

Barakah aliendelea kufunguka kuwa:

Lakini hatuwezi kusema nani namba moja kwa sababu hatujui akaunti ya Sugu ipoje? Ommy Dimpoz, Profesa Jay, Juma Nature na wasanii wengineo”.

Msanii Chemical amewahi kumtaja Diamond kama Msanii Mwenye mafanikio na pesa zaidi Kwenye muziki wa Bongo fleva.

Barakah The Prince Akiri Tetesi Za Kufulia

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefunguka na kuweka wazi kuwa tetesi zilizokuwa zinasambaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa alikuwa amefulia zilikuwa za kweli.

Baada ya kuondoka chini ya uongozi wa Rockstar 4000 Barakah aliamua kufanya kazi mwenyewe kwa kile alichodai kuwa chini ya uongozi ule alikuwa hapati mafanikio kwani alikuwa haruhusiwi kutoa nyimbo na hata kufanya shoo.

Barakah ameachia wimbo wake mpya unaoitwa ‘Sina’ ambao amekiri Kwenye wimbo huo kuwa kipindi hiko amekuwa hana pesa yaani amefulia vibaya mno na chanzo ameweka wazi kuwa ni kuwa chini ya uongozi uliomzuia kufanya shoo kwa mwaka mzima.

Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi kwamba Barakah ameishiwa kabisa hana kitu yaani kafulia na kwenye mahojiano yake na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Barakah amefunguka haya zaidi:

’ Sina’ ni wimbo wangu ambao naweza kusema nimeurekodi wakati nikiwa katika situation mbaya sana kimaisha yaani kuna siku naamka naangalia king’amuzi kimeisha, Tv haiwaki naangalia ndani sina chochote na gari haina mafuta nikasema haya maisha gani haya.

Kama mtakumbuka mwaka jana sikufanya shoo kabisa kutokana na situation iliyotokea kwaiyo nilikuwa siruhusiwi kufanya shoo yoyote kwaiyo nilikuwepo tu kwaiyo huu wimbo ‘Sina’ nimeuvaa uhusika kwa sababu nilikuwepo katika hiyo situation”.

 

Barakah The Prince Hana Mpango Wa Kuwa Chini Ya Label Yoyote Tanzania

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Baraka The Prince amefunguka na kuweka wazi kuwa kwa hivi sasa hataki kuwa chini ya Label yoyote nchini Tanzania.

Barakah anaweza akawa mmoja kati ya wasanii ambao wameshama hama Label kadhaa hapa nchini kwani ameshafukuzwa na kuacha mara kadhaa na mwishowe ameamua kufungua label yake mwenyewe.

Moja kati ya Label maarufu ambayo Barakah aliwahi kuwepo ni 4000 Rockstar iliyo chini ya staa wa Bongo fleva Ali Kiba lakini alihama mwaka jana na kudai hakupata maslahi.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari  Barakah anaweka wazi kuwa hana mpango wowote wa kusainiwa katika label yoyote hapa nchini Tanzania:

Kwa Tanzania hakuna mtu yoyote anayeweza kunisainisha mkataba nikawa chini yake, sijafikiria hilo na wala halitokuja kutokea na hakuna mkakati wa mimi kusainiwa na mtu yoyote”.

Barakah The Prince ameanzisha Label yake mpya akishirikiana na mpenzi wake Naj inayoitwa ‘BaNa Recording Label’ ambayo pia inasimamia kazi za  wasanii kadhaa.

 

Baraka The Prince Ahofia Kuachia Ngoma Mpya Kisa Kombe La Dunia

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefunguka na kuweka wazi kuwa hawezi kuachia ngoma mpya kwa sasa pamoja na kuwa mashabiki zake wanamtaka afanye hivyo.

Baraka The Prince amefunguka na kudai kwa sasa kuna matukio mengi ambayo yamekuwa yakiendelea kwa mfano jambo kubwa kwa sasa ni Kombe la dunia.

Barakah amekaa kimya kwa muda mrefu bila ya kuachia ngoma yoyote ile kwa kipindi sasa kiasi cha mdahabiki zake kumfuata Kwenye mitandao ya kijamii na kumuulizia ngoma mpya.

Ambapo amekiri kuwepo kwa matukio mbali mbali kama misiba na na bifu ya wasanii wengine mbali mbali au hata wasanii wengi kuachia ngoma kwa wakati mmoja husababisha ngoma kufeli sokoni.

Lakini Baraka amedokeza ujio wa ngoma yake mpya itakayoitwa ‘Sina’ ingawa hajaweka wazi kuwa ngoma hiyo itatoka lini lakini itakuwa mara baada ya Kombe la dunia kuishia.

Baada Ya Tetesi Za Kusainiwa WCB, Barakah The Prince Azungumza

Mwanamuziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefungukia tetesi ambazo zimekuwa zikisambaa kwa muda mrefu sasa kuwa amejiunga na label ya WCB.

Tetesi za Barakah kusainiwa WCB zilianza kushika kazi siku za hivi karibuni baada ya kuonekana ana ukaribu na wasanii wa label hiyo na hata wadau wa WCB.

Lakini tetesi hizi ziishika hatamu zaidi pale Barakah alipodaiwa kutengeneza kiki ya uongo ya Rommy kumtongoza mpenzi wake Naj ilimradi watangaze ngoma yao mpya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Rick media, Barakah The Prince amekana tetesi za yeye kujiunga WCB na kudai ni marafiki tu wa karibu:

Hapana, WCB ni kama familia yangu, mara nyingi hata mameneja wa WCB ndio wanakuwa wananiongoza na kunielekeza nifanye nini.

“Kwa hiyo tumeamua kuwa kama familia na kuna wasanii wengi wanafanya vizuri, lakini sio kwamba nipo chini ya WCB, no siyo kweli“.

Hapo nyuma Barakah hakuwa na ukaribu na WCB mpaka pale alipojitoa Kwenye label ya Rockstar 4000 ya Ali Kiba.

“Barakah The Prince Alikuwa Anatembea na Marafiki Zangu Wakati Tupo Kwenye Mahusiano”- Nisha

Muigizaji wa Bongo movie aliyegeukia fani ya muziki na kutoa wimbo wake wa ‘Bachela’ Nisha amefunguka na kuongelea uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Barakah The Prince aliodai ulimuumiza sana maisha mwake.

Nisha amedai kuwa imepita miezi 24 tangu yeye na Barakah waachane lakini amekiri hivi karibuni maumivu aliosababishiwa kwenye penzi hilo ndio yameisha na hivyo amepata ujasiri wa kuliongela penzi hilo.

Kwenye mahojiano na Enews ya EATV, Nisha amefunguka na kusema ameumizwa sana na Barakah mtu aliyekuwa anakataa wapo Kwenye Mahusiano mbele za watu lakini nyuma ya pazia yeye ndio alikuwa anamuhudumia:

Barakah alikuwa ananifanyia vituko vingi sana ikiwemo kutembea na marafiki zangu mtu anafanya vitu vya ajabu ajabu kwa sababu anajua fulani ananipenda ila ndio hivyo kwa muda mrefu Nilikuwa siwezi kuzungumza haya mambo kwa sababu aliniumiza sana mpaka hivi sasa maumivu yameisha”.

Kumekuwa na tetesi kuwa mtu aliyemtuliza moyo Nisha ni Brown ambaye ni Ex boyfriend wa Wolper ingawa wote wamekataa kuwa hawana mahusiano ni kazi tu lakini bado inasemekana kuwa wapenzi.

Maumivu ya Penzi la Barakah The Prince Yameisha- Nisha

Muigizaji wa Bongo movie ambaye hivi sasa amegeukia muziki wa Bongo fleva Nisha Jabu amefunguka na kusema maumivu aliyoyapata kutoka na penzi la staa wa Bongo fleva Barakah The Prince yameisha.

Nisha na Barakah The prince walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi miaka miwili iliyopita lakini penzi hilo liliingia shubiri baada ya Barakah kumtosa Nisha na kuanza Mahusiano na msanii mwenzake mwanadada Naj.

Nisha ambaye ametawala vichwa vya habari hivi karibuni baada ya tetesi kuanza kusambaa kuwa ana Mahusiano ya kimapenzi na Ex boyfriend wa Wolper Brown ambaye ameonekana kwenye video ya wimbo wake wa Bachela.

Ndani ya wimbo huo Nisha amemchana sana Barakah kwa kudai alimfanyia vimbwanga vingi tu enzi za Mahusiano yao ikiwemo alikuwa ana kama kwenye media mbali mbali na kusema hawana mahusiano.

Kwenye Interview aliyofanya na Enews ya EATV Nisha amefunguka mengi juu ya maumivu aliyopata kutoka kwa Barakah na kusisitiza maumivu hayo yameshaisha kwa sasa:

Kuna vitu vingi tu vilivyokuwa vinajiyokeza moja wapo ni kuweza kukanwa kwenye media kuwa hatoki na mimi wakati tunaishi nyumba moja wakati mimi ndio namsapoti na kusapoti kazi yake inafika pale alipo mpaka anajulikana”.

 

Barakah The Prince Adai Kuchoshwa na Hujuma

Mwanamuziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amerudi tena kwenye headlines za mitandao ya kijamii baada ya kudai kuwa amechoshwa na mtu anayemfanyia hujuma.

Mwezi uliopita Barakah alitengeneza headlines na kuzua balaa baada ya kuenda  kwenye vituo vya habari na kudai kuwa uongozi wake wa zamani ukiongozwa na Ali Kiba na meneja wake anauejulikana kama Seven wanamfanyia hujuma ili nyimbo yake mpya isifanye vizuri.

Barakah alijitoa chini ya uongozi wa Rockstar 4000 kwa kile alichodai kuwa walimchelewesha kutoa kazi zake katika wakati husika. Lakini  baada ya kuondoka huko alianza kuwatuhumu Alikiba na Seven kwa kumuhujumu na kudai wanatumia njia mbali mbali ili kizui nyimbo yake ya ‘sometimes’ isichezwe ikiwemo kiharibu utaratibu mzima wa akaunti yake ya Youtube ili asipate mashabiki wa kuangalia nyimbo yake.

Kutokana na hayo Barakah amefunguka na kudai kuwa amechoshwa na hujuma hiyo anayofanyiwa kwenye mtandao wa youtube na kuamua kutangaza dau la milioni tano kwa yeyote atakayeweza kumgundua mtu atakayeweza kumtambua mtu anayepunguza watazamaji wake kwenye mtandao wa Youtube.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio Barakah alizidi kufunguka yafuatayo:

Kwanza nishukuru mashabiki zangu mnaozidi kunipigania na kupoteza muda wenu kwa ajili ya kazi zangu lakini kuna mtu mmoja ambaye aliumbwa kwa ajili ya kurudisha nyuma hatua za watu kila siku views zinazidi kupungua sasa basi matangaza kumpa mtu dau la milioni 3 kwa yeyote atakayethibitisha na kutuletea huyo mtu”.