Brown Aongelea Mahusiano Yake Na Wolper

Kulitokea tetesi nyingi hivi karibuni kuhusu mahusiano ya msanii wa bongo movies Jackline Wolper na mpenzi wake Brown ambae alifuta picha za Jacky zote baada ya kusemekana kuwa alichukizwa na kitendo cha Jacky kwenda katika birthday party ya Diamond Platinumz na kukutana na mpenz wake wa zamani Harmonize.

Akiongea na Friday Nite Live ya EATV, Brown ambae ni video model  anafunguka na kuongelea mahusiano yake na msanii huyo wa kike wa bongo movies na kusema kuwa Jacky ni mwanamke pekee ambae alishawahi kumpenda na bado ataendelea kumpenda daima na wala hana mpango wa kumuacha.Brown akisema kuwa Jacky ni mwanamke ambae amepitia mambo mengi tangu ameingia katika sanaa na tangu ameanza kuwa maarufu hivyo, maswala madogo madogo ambayo mpaka sasa yanaendelea katika mitandao na maneno anayozushiwa ni ya kawaida kwa sababu alishawahi kukutana na makubwa zaidi ya hayo.

Hata hivyo Brown alisema kuwa meseji zilizovuja hivi karibuni zikimuonyesha Jacky anachat na mpenzi mpya wa Harmonize sio za ukweli hata kidogo kwasababu hata yeye alipoangalia meseji zile alijua kuwa ile haikuwa charting ya mpenzi wake. ‘Zile meseji si zake, sio Jacky kabisa mimi najua mwandiko wa mwanamke wangu,yaani hata kama mtu akichukua simu ya Jacky akachart na mimi ninakuwa najua kabisa huyu sio Jacky’

Brown alifunguka na kusema kuwa kati ya wanawake kumi alikuwa nao tangu aanze mahusiano ,Jacky bado anampa namba moja na kutaja baadhi ya mambo ambayo yanamfanya amuweke Jacky katika nafasi iyo aliyataja pia kuwa ni “Nampenda sana Jacky nae ananipenda sana, kwanza ana heshima ni tofauti  na wanawake wengine ukimwambia kitu atakujibu weweeeee..,pili Jacky ni mcha mungu sana , familia yake ni ya dini na familia yangu ni ya dini pia.

Akiendelea kuongea, Brown alikana tetesi za watu kusema kuwa pamoja na kuwa Jacky yupo na yeye lakini yupo mwanaume mwingine mwenye fedha anaemuhudumia Jacky kifedha na kusema kuwa wao wamependana hivyo wanachojari ni mapenzi na wala sio kingine”kama alikuwa anafanya hivyo ni  kwa wanaume waliopita lakini sio kwangu maana ye mwenyewe anajua nini ninampa

Wolper: Sina wivu na Harmonize

Jacqueline Wolper hana machungu yoyote na mpenzi wake wa zamani – Harmonize. Mwigizaji huyo wa filamu za Bongo alisema kuwa aliachana na Harmonize miezi sita iliyopita. Alieza pia vitu vinavyo mvutia kwa mpenzi wake mpya – Brown.

“Tumeachana kama miezi sita hivi tulikuwa hatuelewani. Huyu BFF yaani Best Friend Forever tuna kama wiki hivi. Tulikutana vizuri tu alianza kuniona kama miaka minne hivi before. Kinachonivutia kwake ni mpole na mkweli, kwa hiyo ni rafiki yangu mzuri sana,” Wolper alisema kupitia kipindi cha The Weekend Chart Show ya Clouds TV.

Jacqueline Wolper na Brown

Wolper hata hivyo alisisitiza kuwa yeye na Brown ni marafiki tu wala sio wapenzi;

“Mimi siwezi kuingia kwenye vita na siwezi kuwa na uchungu japo stress hazifichiki na furaha haifichiki. Kwa hiyo nyie mnaweza mkajadili. Vitu vya instagram siyo vya kweli vyote japo wanakuwa na vitu vyao vina ukweli kidogo. Huyu kaachana na mtu wake miezi miwili halafu mwezi wa tatu tukakutana. Kwa hiyo, hizo ni story tu wote tumekutana single ila tofautisha wale ni wapenzi na sisi ni BFF na tupo serious. Ni marafiki wa kweli. Mimi siyo mtu wa TV naye siyo mtu wa TV.”

 

Jacqueline Wolper ajibu wanaosema amenyakua mume wa mtu

Inasemekana kuwa mpenzi mpya wa Wolper anayejulikana kama Brown ni mume wa mtu. Wolper amekemewa kwa tendo lake la kupora mume wa mtu.

Hata hivyo muigizaji huyo wa filamu ya Bongo amewajibu wanaomsuta kwa kusema kuwa mtu yeyote anayedai kuwa Brown ni mume wa mtu ajitokeze hadharani kuliko kusema mitandaoni.

Soma pia: Picha 10 za mpenzi mpya wa Jacqueline Wolper

Akiongea na Amani, Wolper alisema madai mitandaoni ni ya upuzi kwani hakuna mtu aliyeibuka na kusema Brown ni mumewe kabla ya yeye kuanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Brown.

Jacqueline Wolper na Brown

“Kinachonishangaza ni kitendo cha mimi kuwa naye tu ndiyo watu wanaanza kuibuka na kusema eti ana mke, duh! Mbona kipindi siko naye, hakuna mwanamke ambaye alikuwa anasema ni mumewe. Sasa basi kama kuna mwanamke ambaye anadai ni mumewe ajitokeza hadharani. Nilichogundua baadhi ya wanaoibuka ni wale ambao waliwahi kuwa naye kitambo, sasa nasema hivi, huyo anayesema ni mume wake basi ajitokeze,” alisema Wolper.