Casto Dickson- Natamani Sana Kufunga Ndoa

Mtangazaji wa Clouds Tv Casto Dickson ameibuka na kuweka wazi kuwa hakuna kitu anatamani Hivi sasa kama vile kufunga ndoa.

Casto amesema ingawa anatamani kuoa lakini Mpaka sasa hajui ni mwanamke gani atakayemuoa kwa sababu kila mwanamke anayekutana naye ana sifa ambazo hazipendi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Mchanganyiko, Casto amesema ana hamu ya kuoa, lakini tatizo linakuja kwa wanawake anaotaka kuingia nao kwenye ndoa kwani wengi wao hawako tayari na wengine kuna vitu wanavitaka hivyo mwisho wa siku inashindikana.

Unajua mimi siyo mhuni kama ambavyo watu wananifikiria, mimi ni mwanaume ninayejielewa na najua nini nafanya. Ndiyo maana huwa siruhusu hata siku moja kuyumbishwa na maneno ya mtu, kiukweli natamani sana kuoa tena ikiwezekana hata kesho ila tatizo ni kwamba bado sijapata mwanamke sahihi, wengi wao wanapenda starehe tu na siyo vitu vingine vya maana”.

Casto alikuwa kwenye mahusiano na video vixen maarufu kama Tunda Lakini aliishia kumwagwa na kuachwa na tattoo yake mkononi ambayo anayo Mpaka leo.

Casto Kufuta Tatoo ya Tunda

Mtangazaji wa kipindi pendwa  kutoka Clouds Media Casto Dickson  amefunguka na kusemakuwa hata baada ya kuachwa na mpenzi wake Tunda haoni haja tena ya yeye kuendelea kuwa na tatoo ya mwanadada huyo kwa sababu tayari hawana mahusiano.

Ikumbukwe kuwa Casto na Tunda waliwahi kuwa katika mahaba mazito  na hata mtangazaji huyo kusema kuwa hataki kujali wala kusikiliza maneno ya wat wanayosema kuhusu mwanadada huyo,

Casto alifikia hatau ya kutangaza ndoa kwa mwanadada huyo na ksuema kuwa alikuwa mbioni kumpeleka kwa wazazi wake ili akajitambulishe huko.

Sasa basi hata  baada ya kuachana ,Casto anasema kuwa haoni haja ya kundelea kuwa na tatoo hiyo hivyo ataifuta muda wowote.

 

 

 

Casto Dickson Amkumbuka Mtoto Wake.

Mtangazaji wa clouds media Casto Dickson ameonyesha kumkumbuka aliyedaiwa kuwa ni mtoto wake ambae alizaa na msanii muna love kipindi wakiwa wapenzi .

Mtoto huyo aliyewahi kujizolea umaarufu wake akiwa bado mdogo kutokana na maajabu makubwa aliyokuwa akiyafanya baada ya kuokoka alifariki Dunia mapema mwaka huu na kuacha mashabiki wake na wa mama yake katika masikitiko makubwa lakini kubwa zaidi ni ile pande mbili kugombania maiti hiyo.

Hata hivyo cCasto aliandika katika ukurasa wake kuwa amekuwa akimmisi mtoto wake huyo ambapo kipindi cha msba alijitokeza baba mwingine na kudai kuwa mtoto huyo alikuwa wake.

Casto Athibitisha Ndoa Hivi karibuni.

Mtangazaji kutoka clouds media Casto Dickson ambae alivuma sana baada ya kuingia katika mapenzi na mwanadada Tunda video vixen lakin baadae kuonekana kulega lega kwa penzi hilo hata kusemekana kuwa waili hao kwa sasa wameachana amefunguka na kusema kuwa anakaribia kufunga ndoa.

Maneno hayo yanaleta mshangao mkubwa kwa sababu kila shabiki yake anataka kujua kuwa mwanamke anaefunga nae ndoa atakuwa ni nani  kwa sababu wengi wanajua kuwa ameachana na Tunda.

Hata hivyo alipokuwa akiongea na Millard Ayao , Casto hakutaka kusema ni mwanamke gani anafunga aneo ndoa zaidi ya kusema kuwa anakaribia kufunga ndoa hivi karibuni.

Hata hivyo wawli hao wanaonekana bado kuwa pamoja hasa katika kipindi hiki ch karibuni baada ya Casto kuweka picha katika mtandao huku akimsifia mpiga picha kuwa ni Tunda.

Casto aliwahi kutangaza kuwa anatarajia kufunga ndoa na mwanadada huyo hapo siku za nyuma.

Tunda Abambwa na Diamond Baada Ya Kumwaga Casto (+video)

Socialite na video queen maarufu Bongo Tunda Sebastian amerudi Kwenye headlines baada ya kuonekana na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Tunda ameshawahi kusemekana kuwa Kwenye Mahusiano na Diamond lakini baadae alianzisha Mahusiano na Mtangazaji wa clouds Tv Casto Dickson.

Pamoja na kwamba Casto alichora bonge la Tattoo ya Jina la Tunda Kwenye Mkono wake lakini aliishia  wiki chache zilizopita na siku ya jana ameonekana Kwenye Birthday party Diamond.

Diamond alionekana akicheza na Tunda kwa ukaribu sana kiasi ya kupelekea kuzua tetesi za kuwa Tunda kamtosa Casto na Kurudisha majeshi yake kwa Diamond.

https://www.instagram.com/p/BodZvdkn_6e/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1mcmagtlbnvu

Siku ya jana ilikuwa ni Birthday party ya Diamond na housewarming party ya nyumba yake mpya ambapo alifanya Private party na kualika Mastaa kibao ikiwemo timu nzima ya WCB , Navy Kenzo, Dully Sykes, Billnas, Tunda na wengineo.

Uimara Wangu Unatokana na Mwanamke Niliyenae ;-Casto Dickson

Mtangazaji kutoka Clouds Media anasema kuwa wa sasa hana anachojali pale anapokuwa anaongelewa kwa sababu ya kuwa imara kutokana na mtu aliyenae katika mahusiano ambae ni Tunda.

Mimi binafsi mitandao haijafanikiwa kuniumiza kabisa katika kipindi hiki uwezi amini , tangu nimeingia katika mhusiano na Tunda  na matatizo ya misiba yaliyotokea, ninaamini kuwa uimara wangu umejengwa na mwanamke ambae kwa sasa niko nae katika mahusiano.

Casto anasema kuwa sababu kubwa anayoamini kuwa Tunda ndio uimara wake kwa sababu Tunda amekuwa akitukanwa sana katika mitandao ya kijamii  kwa muda mrefu hivyo amekuwa akipata ujasiri kutoka kwake kwasababu yeye alishayapitia hayo.

Hii inatokana na mishale mingi ambayo yeye amekutana nae katika mitandao ya kijamii,kwaio kwa uimara wangu naona kabisa kuwa sihitaji kuliongelea hilo kwa sababu ninapaswa kulitumia   kama mwanaume.

Casto anasema kuwa amekuwa akisemwa atangu hata mtoto bado hajafariki hivyo kwake ni kitu cha kawaida ukizingatia kuwa wameshasema sana na itafika sehemu watanyamaza tu.

Kama niliweza kupambana na mishale ya kuwa sikuwa nampost mtoto wangu kipindi anaumwa nitanshindwa kupambana na hiyo ya kipindi anafariki?

Casto Aomba Maamuzi yake Yaheshimiwe kwa Tunda.

Mtangazaji wa clouds media , Casto Dickson Amfunguka na kuwaomba watu wanaomsema na kumshangaa kwanini ana mpenda sana tunda wamuache na kuheshimu sana maamub=zi yake kwa sababu hapo ndipo alipofikia na ana mapenzi ya dhati na mwanadada tunda.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram, casto anasema kuwa tunda ndie mwanamke anampa ratiba zake za kila siku katika kazi zake katika maish yao.

respect my choice, she is the one who tells me casto its time to job,casto una ahadi ya kikao sehemu,unatakiwa kwenda kwenye hiki na hiki ila nyie majiran hamjui,yaacheni ya moyoni yabaki ya moyoni, nawaheshimu na nina wapenda sana, i love you mmachame wangu,

Tangu mahusiano ya catso na tunda yameanza kwa zaidi ya miezi sita sasa, mashabiki wamekuwa wakimsema sanacasto hasa kutokana na yale aliyowahi kuyafanya nyuma tunda, hata hivyo anachoamini casto kwa mwanamke wake ni kwamba hayuko kama zamani .

Ujio Mpya wa Casto Baada ya Kupotea Mtandaoni Baada ya Msiba.

Ni kama wiki sasa inakatika tangu kutokee kwa msiba wa mtoto wa msanii Muna love, msiba ambao ilizua tafrani baada ya maiti kugombaniwa na baba na mama baada ya mama kutamkia kuwa baba wa mtoto wa marehemu ni Casto na sio Peter,

Hata hivyo kipindi hicho chote casto hakutaka kuongea chochote kuhusu swala hilowala kutaka kuzaungumzia kitu chochcote kuhusus swala hilo, hata hivyo mashabiki wake walikuwa wakimpa msukumo sana kuongea chchote kuhusu swala hilo lakini hakutaka kujibu chochote.

Baada ya ukimya huo wa muda mrefu, kwa mara ya kwanza Casto ameweka picha katika ukurasa wake wa instgram akiwa ameinamisha kichwa chini  huku akiwa hajaandika chochote kuhusu picha hiyo wala hakutaka kujibu maoni yoyote katika ukurasa wake.

Baadhi ya mshabiki zake wamemtaka kuongea kitu chochote kuhusu swala hilo ili kuwaweka wazi nini hisia zake kuhusu hilo lakini Casto haonekanai kujali hisia hizo kwa sababu hata za kwake pia hakutaka kushare na mashabiki.

Aliyezaa na Casto Afunguka , Asema Casto ni Mchafu.

Huku akiwa bado ndo kwanza kidonda kibichi cha kufikwa na msiba wa mtoto wake  lakini kumekuwa na maneno mengi yamekuwa yakimuandama mtangazaji wa kipind cha siz kitaa kinachorishwa na Clouds tv  kutokana na mambo mengi anayoyafanya katika mitandao ya kijamii.

Moja ya wanawake aliwahi kuwa nao katika mahusiano na kubahatika kupata naeo mtoto Don Posh amefunguka na kusema kuwa casto hawezi kuwa na mahusiano na tunda bali wanakuwa  pamoja kwa ajili ya kutafuta kiki tu na wala sio vinginevyo.

Mwanadada huyo akiwa anaongea na waandishi wa habari anasema kuwa casto hawezi kupata mwanamke atakae mpenda kama alivyowahi kumpenda yeye na kwa sasa anahangaika tu wala hakuna cha maana anachopata katika mapenzi, na kusema kuwa yeye bado anampenda sana casto.

Hata hivyo Don Posh anasema pamoja na kwamba anampenda sna casto lakini hawezi kutembea nae tena kwa sababu casto amekuwa mchafu kutokana na picha na video zake vchafu anazoweka katika mitandao ya kijamii akiwa na huyo Tunda.

Siwezi Kupata Taarifa za Mtoto Wangu Kupitia Instagram:-Casto

Baada ya kutukanwa na kutupiwa maneno mengi katika mitandao kuhusu kutokuwa akijali kuhusu hali ya mtoto wake ambae yuko hospitali kwa sasa na kwamba hali yake imekuwa mbaya na yeye yuko busy na mahaba mapya na mpezni wak tunda, Casto Dickson amefunguka na kuongea mazito.

Akiongea na moja ya waandishi wa habari wa Clouds Tv, Casto anasema kuwa  kumekuwa na maneno tofauti tofauti kuhusu hali ya mtoto wake huku kukiwa hakuna mtu yoyote wa karibu na mtoto anaetaka kumwambia taarifa za kueleweka kuhusu mtoto huyo.

kwanza kabisa ilizuka kuwa mtoto kafa lakini nikawapigia simu hadi kwa bibi yake nikawaambia kuwa niambie ukweli kuhus hali ya mtoto wake, sio kwamba napenda  i dont know ingawa najua kabisa mtoto wangu anaumwa.mi siweizi kupata taarifa za mtoto wangu kupitia instagram.Ninamuombea sana mtoto wangu Mungu ampe nafasi ya  pekee maana najua umri wake mdogo sana miaka saba  lakini anapitia situations nyingi sana,

Mamia Wamtolea Maneno Casto Kuhusu Kutokujali Hali ya Mtoto Wake na kumjali mwanamke.

Ikiwa mtoto aliyezaa na mzazi mwenzie Muna akiwa hoi kitandani anaumwa watu wamekuwa wakijudge mtangazaji Casto amekuwa akijisikiaje na drama za mapenzi yake na Tunda zinazoendelea ktika mitandao ya kijamii huku mtoto huyo akiwa hospitali.

Katika kusambaa kwa picha zikimuonyesha mtoto huyo yuko hospitali wakati huku mahojiano mengi ya Casto yakiwa yanahusu kuwa katika mahusiano na tunda na kuchora kwake tatoo, watu wamejikuta wakimtolea povu kwa madai ya kuwa na uchungu na kile anachofanya Casto kuwa sio kizuri kwa sababu aliyepo hospitali ni mtoto wake pia.

pamoja na kwamba wasanii wengi wameonekana kuguswa na maumivu  ya Muna na familia yake lakini Casto inasemekana kutoonesha chochcote kuhusu swala la kuumia wala kuumwa kwa mtoto wake huyo.