Mzazi Mwenza Wa Chege Amwaga Povu Kwa Wanaomtaka Mpenzi Wake

Mzazi mwenzake na msanii mkongwe wa Bongo fleva Chege Chigunda anayejulikana kama Zahra ameshindwa kujizua na kumwaga povu zito kwa mwanamke ambaye amekuwa akimmendea Baba watoto wake.

Zahra alimwaga povu hilo baada ya kuwa na tetesi kuwa kuna mwanamke amekuwa akimtumia meseji za kumtaka kimapenzi Chege.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Zahra alimwaga povu hili:

Ifike steji wanawake tubadilike, hivi kwa nini wanawake hatupendani? Kipindi Chege yupo bachela hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kwenda Kwenye social media na kumzungumzia vibaya leo hii amekuwa staa kiasi gani hadi mtake kumuharibia CV yake Jamani? Kipindi hakai na mwanamke mlikuwa mnamuona muhuni sio handsome na maneno kibao ya kashfa kwa kaka wa watu hakuna hata aliokubali kuacha mambo yake nakuamua kumzalia kila mtu alikuwa anamdharau kwa staili yake leo mimi nimeamua kumzalia na kuishi naye mnaanza vitu vya ajabu! Ili baadae muanze kusema wasanii sio ya wanaume mbona kamuacha mzazi mwenzake. Nipumzisheni na DM zenu hakuna aliokamilika hapa duniani unamsema sijui ana wanawake wengi je wewe kwa mtu wako uko peke yako? Ndio kwanza mtoto ana Miezi mitatu mmeanza haya nikizaa wapili simtanirushia mabomu?”.

Chege na Zahra walianika mapenzi yao hadharani Miezi michache iliyopita baada ya kufanikiwa kuzaa mtoto wao wa kike anayeitwa Judah.

Chegge- Nimeumizwa na Kifo Cha Agnes Masogange

Mwanamuziki wa Bongo fleva Said Juma ‘Chege Chigunda’ ameongelea kifo cha msanii wa filamu na video queen Agnes Gerald ‘Masogange’ na kusema hatokaa amsahau mrembo huyo.

Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita katika kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngoma kilichopo Mwenge jijini Dar ambapo jana aliagwa katika Viwanja vya Leaders na kusafirishwa kwenda kwao Mbeya ambako alizikwa jana Aprili 24, 2018 kijijini kwao Utengule, Mbalizi.

Chege aliyasema hayo juzi Jumapili alipokuwa Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar katika kuuaga mwili wa Masogange aliyefariki ghafla baada ya kupungukiwa damu.

Kiukweli msiba umeniumiza kama msanii kwani sisi ni miongoni mwa wasanii wa Bongo Fleva wa mwanzomwanzo kumtoa Masogange kimuziki, kifupi sitamsahau na nawapa pole ndugu na wanafamilia”.

 

Chege na Mpenzi Wake Wamkaribisha Mtoto Wao

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Said Juma maarufu kwa jina la usanii kama Chege chigunda ametangaza rasmi ujio wa mtoto wake siku ya Jumapili tarehe 11 ambaye amempa jina la Jada.

Chege na mpenzi wake wa siku nyingi Zahra wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza wa kike. Chege alitoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo aliandika:

Ni kweli siku ya jana majira ya saa kumi jioni mtoto wangu alizaliwa namshukuru sana Mungu kwa sababu mtoto ni Baraka mimi na mama yake tuna furaha sana”.

Mkali huyo anayetamba na ngoma yake ya Kaitaba aliyomshirikisha Saida karoli aliweka wazi mwishoni mwa mwezi uliopita kuwa ana mpenzi wanaishi wote lakini kuhusu kufunga ndoa amekiri yeye atakuwa mtu wa mwisho kuoa.

Juma Nature afunguka kuhusu swala la kuchukiana na Chege Chigunda kwasababu ya mwanamke

Juma Nature ameongelea swala lililowafanya wengi kuamini kuwa hali sahani moja na Chege Chigunda. Msanii huyo mkongwe amekana kuwa mwanamke ndiye chanzo cha beef yake na Chege.

Cha kushangaza ni eti Nature hana beef yoyote na Chege; akizungumza katika kipindi cha eNewz ya EATV, rapper huyo alifunguka na kusema hajawahi kugombana na Chege.

Chege Chigunda

Jibu lake Juma Nature ni bainisho baada ya kuenea tetesi za kipindi kirefu zilikuwa zinawaaminisha watu kuwa mke aliyemuoa msanii huyo ndiye alikuwa mpenzi wa Chege hapo awali mpaka kupelekea kuimba wimbo wenye maudhui ya kumuaga mpenzi huyo uliyopewa jina la ‘Good bye’.

“Mimi sijawahi kugombana na mwanangu, sasa mimi nigombane na damu itawezekana kweli ?, hatuwezi kugombana, tutagombana stejini tu kwa sababu ya usanii lakini hatugombani kama hivyo unavyochukulia wewe”. Alisema Juma Nature.

Juma Nature