Daxo Chali Yuko Tayari Kufanya Kazi na Nini, ni Baada ya Kuachana na Nay

Mtayarshaji maarufu wa muziki nchini Daxo Chali amefunguka na kusema kuwa yeye hana kinyongo na kufanya kazi na mwanadada nini ambae hapo awali alikuwa akifanya nae kazi lakini alihama kwake na kwenda kufanya kazi na nay wa mitego.

Daxo Chali ambae ndie aliona vipaji vya Nini na Hytham mara ya kwanza na kuanza kufanya nao kazi lakini baadae walikuja kukorofishana sana baada ya Nini kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi na Nay wa mitego hivyo kutokuwa na nidhamu na kuwa akifanya yale anayojisikia hivyo kushindwana katika swala la kufanya kazi pamoja.

ata hivyo, baada ya muda Nini na Ney hivi karibuni walijitangaza kuwa wameacana huku sababu kubwa nini akisema kuwa wanawake wengi alionao nay wamemfanya aachane na Nay, Daxo Chali alipoulizwa kuhusu mahusinao hayo alijibu kuwa hajui swala la kuachana kwao kama ni kweli au kiki kwa sababu hata kipindi wapo katika mahusiano walikuwa wakikataa sana.

Daxo Chali aliulizwa kama angeweza kumpokea Nini tena kama atarudi kwake na yeye hakusita kusema kuwa kama nini atakuja kufanya kazi kwake atamokea kama wasanii wengine wanavyokuja na kulipa kiwango kinachotakiwa basi hana kinyongo cha kufanya nao kazi.

Daxo Chali anasema kuwa anafurahi kuwasaidia wasanii na kufikia muda wa kujitambua na kuamua kufanya kazi kama wao hivyo kwa Nini hakuwa na shida nae hata kidogo na ndio maana alimuacha aende.

“Daxo Chali Alikuwa Aliniimbisha Muziki Siujui”- Nini

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake ya Kolo, Mwanadada Nini ameibuka na kudai Daxo Chali alikuwa hajamjulia mziki wake wa kufanya kwani alikuwa anaimba nyimbo za ajabu.

Kama utakumbuka Nini alikuwa yupo chini ya label ya MJ Records chini ya Producer Daxo Chali lakini aliishia kutimuliwa baada ya kudaiwa kuwa na utovu wa nidhamu.

Baada ya kuondoka Kwa MJ Records, hivi sasa Nini yupo chini ya uongozi wa Nay wa Mitego ambapo amedai ndipo alipopatia umaarufu zaidi na muziki wake kujulikana zaidi kwani anafanya muziki mzuri.

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Nini amedai kuwa mziki aliokuwa anaimba chini ya uangalizi wa Daxo CHali haukuwa muziki sahihi kwake na wala alikuwa haujui wala haupendi.

Mashabiki zangu wameongezeka kwa sababu mziki ninaoinba sasa ni tofauti na niliokuwa naomba kwa Daxo Chali kwa sababu mziki ninaoinba sahivi ni ule mziki ambao Watanzania wameshazoea kuusikia na kuupenda na  mimi nafurahia zaidi kuimba stabilizer hii ya hivi sasa”.

Kumekuwa na tetesi kuwa Nini anatoka kimapenzi na Nay wa Mitego, taarifa ambazo mwenyewe amezikataa kabisa.