Mtoto Wangu wa Tatu Nitazaa na Mwanaume Atakayenioa-Hamisa Mobetto

Muigizaji wa Bongo movie Hamisa Mobetto ameweka wazi kuwa endapo atazaa mtoto mwingine basi atazaa na mwanaume atakuwa amemuoa.

Hamisa ambaye tayari ana watoto wawili ambao kila mmoja ana Baba yake ambaye mmoja amezaa Mkurugenzi wa EFM Majizzo na mtoto mwingine amezaa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi nyingi za Diamond kufunga ndoa ambapo mwanzoni mwa mwaka huu alisema lazima ataoa lakini kwa sasa inasemekana kuwa atamuoa mpenzi wake Hamisa.

Kwenye mahojiano aliyofanya hivi karibuni Hamisa ameweka wazi kuwa tetesi zinazoendelea kuenea kuwa yeye anaolewa na Diamond sio kweli lakini anachojua ni kwamba hana mpango wa kuzaa mtoto mwingine mpaka aolewe.

Kusema ukweli sijui kitu chochote kuhusu harusi lakini ninachojua nitazaa mtoto wangu wa tatu na mume wangu wa ndoa ambaye mpaka sasa sijui atakuwa nani”.

 

Tunda Amtupia Dongo Zito Hamisa Baada Ya Kumuona na Diamond

Video vixen maarufu Tunda Sebastian amerudi tena Kwenye headlines baada ya kumtupia Dongo Zito hasimu wake namba moja Hamisa Mobetto baada ya video zake za chumbani na Diamond kuvuja mtandaoni.

Usiku wa jana Diamond na Hamisa walizua gumzo baada ya kuonekana pamoja chumbani wakiwa wanakumbatiana kwenye mahaba mazito jambo lililozua gumzo kuwa wamerudiana.

Lakini muda mfupi baada ya Hamisa kuonekana na Diamond video zilizomuonyesha Diamond na demu wa kizungu wakila Madenda nazo zilivuja mtandaoni jambo lililowachanganya watu wengi kuona Diamond na wanawake wawili tofauti katika usiku mmoja.

Kama utakumbuka Tunda na Hamisa wameshawahi kuwa na bifu siku za nyuma huku ikiaminika kuwa walikuwa wanamgombania Diamond kwani wote wawili wameshahusishwa kuwa na Mahusiano na Diamond.

Tunda ameibuka na kumpa Dongo Zito Hamisa baada ya video zake na Diamond kusambaa mtandaoni ambapo amedai kuwa anamuonea huruma Hamisa maana amedhalilishwa na mwanaume ambaye ni wazi kabisa kuwa hamtaki.

Kupitia ukurasa wake wa Snapchat, Tunda kaandika maneno haya:

 

Hatma Ya Kesi Ya Hamisa dhidi Ya Diamond Kujulikana Leo

Miezi miwili iliyopita mwanamuziki Diamond Platnumz alikiri kuzaa na mwanamitindo Hamisa Mobetto, lakini baada ya wiki kadhaa Hamisa aliibuka na kudai kuwa Diamond amekataa kumuhudumia mtoto wao na kuwa alikuwa hatoi pes yoyote ya matunzo hali iliyopelekea kumfungulia kesi ya madai katika mahakama ya Kisutu’

Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu siku ya leo Novemba 10, 2017 inatarajia kutoa uamuzi dhidi ya kesi ya matunzo ya mtoto, uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu mkazi Devota Kisoka upande wa watoto.

Hatua hiyo imekuja baada ya mahakama kusikiliza hoja za pande zote husika kutokana namsaini Diamond kuwasilisha pingamizi kupinga kesi hiyo kwa madai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi.

Katika kesi hiyo Hamisa alifungua kupitia kwa mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Goodluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys ambapo anaiomba mahakama imuamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi kupitia hati hiyo ya madai, mwanamitindo huyo anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoshtua familia yake.

Hata hivyo Diamond aliwasilisha hati ya majibu ya kinzani akipinga maombi hayo akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi ni sh. milioni tano kwa ajili matunzo ya mtoto ni kubwa sana na hawezi kuzimudu.

Mange Ampa Mbinu Hizi Hamisa Ili Azikombe Pesa za Diamond

Mwanasiasa maarufu mtandaoni Mange Kimambi, ameibuka tena na jipya huku safari hii amempa mbinu mpya Hamisa atakazotumia ili aweze kupata pesa ya kulea mtoto wake kutoka kwa Diamond.

Tangu Diamond na Hamisa waweke wazi kuwa wamezaa mtoto kumekuwa na visa baada ya visa hasa baada ya Hamisa kudai kuwa Diamond amegoma kutoa pesa ya matumizi kwaajili ya malezi ya mtoto, kitu kilichopelekea Hamisa kumpeleka Diamond mbele ya sheria.

Baada ya habari kutapakaa kuwa familia ya Diamond inamkataa mtoto wa Hamisa na Diamond hataki kutoa pesa ya malezi, Mange ameibuka tena na safari hii kadai kuwa zari, Diamond na familia yao wanataka kumchosha Hamisa ili akate tamaa na kuifuta kesi yake mahakamani dhidi ya Diamond.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange alimpa mbinu hizi Hamisa ili aweze kupata pesa kwaajili ya malezi ya mwanawe.

Nimepitia kidogo sheria ya matunzo ya mtoto wa Tanzania inafanana na ya marekani, wanaangalia kipato cha wazazi na matunzo yanatolewa kutokana na kipato cha mzazi, ila tatizo wanawake Tanzania wanashindwa kuthibitisha kipato cha mwanaume mahakamani, Hamisa kama uyashindwa kupeleka ushahidi wa kipato cha Diamond utaishia kupewa laki mbili kwa mwezi. Kwanza ujue Diamond hawezi kutaja kipato chake cha kweli mahakamani inabidi umlazimishe”.

Pia Mange aliendelea kufunguka mbinu ambazo Hamisa atatumia kupata kipato halisi cha Diamond:

Ushahidi wa Kwanza ni uombe mahakama ikupe order ya bank account zote anazoweka pesa Diamond kuanzia mwezi wa 1 mwaka 2015, kampuni zote zilizoratibu show zake zote wapeleke order ya mahakamani wapeleke contract, kampuni zote zilizompa matangazo kama Danube na Vodacom na Diamond Karanga wote wachape barua za mahakama wapeleke mikataba.

Then peleka order ya mahakama kwa kampuni ya WCB na ile website yao wanayotunia kuuza nyimbo za wanamuziki na pia ichape barua ile Chibu perfume anayo share na Kusaga wote wachape barua waonyeshe mikataba yao na Diamond anaingiza shilingi ngapi. Ukitoka hapo wachape barua TRA kutoa rekodi ya malipo yake ya TRA”.

Mange alimalizia kwa kumshauri Hamisa asikate tamaa kumlea mtoto wake kwani kama alimpigania mpaka Diamond akamkubali mtoto wake hadharani basi aendelee kumpigania mpaka pale atakapokubali kumlea mtoto wake.