Zari na Hamisa Wazidi Kuvurugana Kisa Diamond

Baada ya kumalizika kwa utata wa muda mrefu baada Diamond kukiri kuwa ni baba  wa mtoto wa Hamisa, mashabiki walidhani sakata hilo limeisha na halitasikika tena lakini imekuwa tofauti na matarajio ya wengi kwani picha ndo kwanza kama linaanza kwani sakata hilo limechukua sura mpya.

Zari na Hamisa ambao kwa sasa wote ni mama watoto wa Diamond wameonyeshana chuki kwa kupitia mtandao wa kijamii Snapchat,huku wakiweka wazi  kuwa tusitegemee kuwaona wakiwa marafiki mda wowote kuanzia sasa. Hamisa kwa kudhani kuwa mtoto wake Dylan ameshakuwa na undugu na watoto wa Zari na Diamond Nillan na Tiffah akaamua kuwafata (follow) kwenye instagram kwakutumia ukurasa wa Dyla lakini Zari hakufuraishwa hivo kwa kupitia Snapchat akamwambia Hamisa amuachie watoto wake na wazimu wake unahitaji kupelekwa hodi ya machizi

Kupitia Snapchat Zari aliandika;

“Laki 2 stop following my kids lol, Your obsession needs a mental institution. Like hell?”.

Baada ya kuona hivyo Hamisa ilibidi awa-unfollow watoto wa Zari na kuandika haya kwenye Snapchat;

“Na kama kuna mwanamke mwingine unampenda zaidi yangu…….Bai mwambie mzaa chema shkamoo”.

“Waambie waliopanga mwenye nyumba kaja ndani……Ana meremeta”.

Ingawa watu wengi wangependa kuwaona wanawake hawa wanapatana kwa sababu tu ya watoto wao kwani wote baba yao ni mmoja hivyo wakiwa na maelewano angalau watoto watakua wakijuana kama ni ndugu.

Zari Ajibu Mapigo Baada ya Sakata la Jana

Baada ya Msanii wa kizazi kipya Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ kukiri kuzaa mtoto na mwanamitindo Hamisa Mobetto, hatimaye mama watoto wake Zarinah Hassan azidi kumuweka njia panda juu ya uhusiano wao.

Mwanamama huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, ameeleza kupokea ushauri uliotolewa na baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii. “Watu wakiamua kuchepuka au kudanganya ni sawa na kujipotezea muda, ingawa wanahisi wanakuchezea wewe, hivyo usikate tamaa na kujilaumu wewe kwa ajili ya makosa ya watu wengine, maisha lazima yaendelee.

“Mambo yaliyotokea hayawezi kunipungizia hadhi yangu, usijilaumu kwa mambo yaliyotokea, zingatia malengo yako na kufanya maisha yako yaendelee”.am edema Zari.

Amesema kuwa yale yote yaliyosemwa katika sakata hili yanabaki yalivyo na muda huu anaamua kuyaweka kando na kuelekeza nguvu zake katika kusheherekea siku yake ya kuzaliwa.

Sakata hili limeibuka siku moja baada ya ya Zari kujibu mapigo katika mtandao wa Snapchat akionya asihusishwe na kitendo alichokifanya Diamond, cha kuzaa na Hamisa Mobetto.

Awali Katika maelezo yake mwanamuziki Diamond alisema kuwa ameshazungumza na mpenzi wake huyo kuhusiana na  mtoto aliyezaa na Hamisa na kwamba ameelewa na  hakuna tatizo tena.

Diamond Amtambulisha Mtoto wake Aliyezaa na Hamisa

Mwanamuziki Diamond Platnumz kwa mara ya kwanza amemkubali mtoto wake aliyezaa na Hamisa Mobetto na kumuweka wazi ili watu wote wamuone.

Katika mahojiano aliyoyafanya leo Diamond alikiri kuwa mtoto yule no wake na jina lake ni Dylan. Alipoulizwa na waandishi Kama Ana uhakika yule ni mtoto wake na kama amefanana naye Diamond alijibu kuwa ataposti picha baadae ili watu wamuone na waamue wenyewe Kama amefanana naye au la. Japo kuwa mama wa mtoto, Hamisa hakuweka picha ya mtoto huyo Familia ya Diamond ndio ilikuwa ya kwanza kutuma picha hiyo mitandaoni.

Baada ya kumaliza mahojiano hayo, Diamond kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alituma picha ya mtoto wake huyo na kusindikiza kwa maneno yaliyosema “Young Lion”.

Bob Junior- Acheni Kuingilia Kati Bifu Langu na Diamond

Aliyekuwa Producer wa Diamond Platnumz ambaye pia ni mwanamuziki wa Bongo Fleva Bob Junior, Amewataka mashabiki kuliacha kama lilivyo swala lake yeye name Diamond kwani hakuna anayejua mwanzo wa kazi zao.

Msanii huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ya mpya ya ‘Give me’ ameiambia Bongo dot home ya Times FM kuwa mashabiki wanaingilia Kati kitu wasichokijua kiundani kitu ambacho sio sawa.

Katika mahojiano aliyofanya Bob Junior alisema;

“Ukweli ni kwamba hawapaswi kunizungumzia na yeye kwasababu kipindi tulikuwa tunatengenezana tulikuwa wawili, kwa hiyo huwezi kuingilia wewe kama shabiki maandazi kea kuingilia vitu ambavyo huvijui. Mimi na yeye  tulikuwa tunafahamiana wakati tupo chumbani, wakati chumba ni studio lakini baada ya hapo tukawa wakubwa, sasa wewe shabiki ambaye unazungumza unamjua yeye? Au unanijua Mimi? Au Mimi na  yeye ndo tunajuana vizuri name zaidi”.

Pia ameongeza Kuwa;

“Kwa iyo wewe unaingia Kati baada ya kumfahamu Bob Junior na huyo muhusika (Diamond), unanza kumtetea yeye au kunitukana mimi wakati sisi hutuwafahamu?”.

Bob Junior amekuwa akimshutumu Diamond kwa kutangaza Kuwa kuna kolabo ambayo wangefanya pamoja lakini hakuna utekelezaji wowote na amekuwa akimtafuta ili kuzungumza hilo lakini Diamond amekuwa akimpuuza.

 

Faiza Ampongeza Diamond Kwa Kumkubali Mtoto Wa Hamisa

Mwanamitindo Faiza Ally amefunguka na kumpongeza Diamond kwa hatua aliyochukua ya kwenda kwenye vyombo vya habari na  kuweka wazi kuwa yeye ndiye baba wa mtoto wa Hamisa. Kwa muda mrefu katika mazingira mbalimbali Diamond alikanusha kuwa name uhusiano na Hamisa name pia kuzaa naye. Leo kwa kupitia kipindi cha Leo Tena Diamond amekubali kuwa shetani alimpitia na amewahi kuwa name mahusiano ya kimapenzi na Hamisa.

Baada ya mahojiano hayo kuruka hewani mwanadada Faiza kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alifunguka new kuandika yafuatayo:

“Nasikiliza Clouds FM Naseeb nakupenda wewe ni mwanaume ea maana  saana sema wanawake wa Uswahilini ni kama ile methali ya Hamisi, yaani unaweza ukamtoa Hamisi shamba lakini usilitoe shamba kichwani kwa Hamisi #hope hutarudia Tena ujinga wako”.

Inasemekana Kuwait suala la Diamond kumkubali mtoto huyo na kumuhusumia limemgusa sana Faiza kwa sababu halo aliyonayo saivi ni Kuwa baba wa mtoto wake hamuhudumii mtoto wake ipasavyo ndio maana ameona kitendo alichofanya Diamond ni  cha kishujaa.

Diamond na Dillish Mathews katika skendo nzito

Mwanamuziki Diamond Platnumz amejikuta katika skendo nyingine ya kimapenzi safari hii akiwa na mwanadada mrembo kutoka Namibia Dilish Mathews ambaye ni mshindi wa Big brother Africa mwaka 2013. Inasemekana kuwa Diamond na Dillish wameonekana kwenye visiwa vya Zanzibar wakila bata kwa pamoja katika hoteli ya kifahari ya La Gemma.

Dilish ambaye aliposti kwenye kurasa yake Instagram Siku tatu zilizopita baada ya kufika kwa mara ya kwanza kwenye visiwa hivyo ambapo aliandika:

“First time in East Africa…I am so in love with Zanzibar #Journey of a humble dreamer #Princess #Africa”.

Baada ya muda Dillish alionekana akiposti video na picha kwenye mitandao yake ya kijamii huku akisindikiza na nyimbo za Diamond, katika video alizotuma alionekana akimuita mtu huyo aliyekuwa nae “Bae” ambapo inasemekana mtu huyo ni Diamond baada ya wote wawili kuposti picha wakiwa sehemu moja.

Baada ya habari hizi kuenea mtandaoni imekuwa skendo kwa Diamond ambaye tayari ana mpenzi wake Zari ambaye pia ni mama wa watoto wake wawili na anasemekana kuwa atakuwa baba wa mtoto wa Hamisa Mobetto ingawa ameendelea kukataa kuwa yeye sio baba.

 

Zari: Majizzo ni baba wa mtoto wa Hamisa sio Diamond

Kumekuwa na tetesi kwenye mitandao ya kijamii na mashabiki  wanajiuIiza  maswali je Diamond ni  baba halisi wa mtoto wa Hamisa?Ingawa Diamond amekataa tangu mwanzoni kuwa mtoto yule sio wa kwake licha ya Hamisa kumpa mtoto jina la baba ake na  Diamond “Abdul Naseeb”.

Katika mahojiano aliyofanya Zari  nchini Uganda amedai kuwa Diamond sio baba wa mtoto wa Hamisa na amekataa mara nyingi bali baba wa mtoto ni Majizzo,  ambaye tayari ni baba wa mtoto wa hamisa, amedai kuwa sababu pekee inayomfanya majizzo  akatae mtoto ni kwasababu  anamuogopa Lulu Michael ambaye ni mpenzi wake, na pia amedai kuwa Majizzo ndiye anayemlipia  kodi ya nyumba na kumuhudumia kila kitu. Lakini  Zari amefunguka kuwa amekwisha mwambia Diamond kama mtoto atatokea akawa  wake {za diamond} basi itabidi amuhudumie na amkubali ingawa hawezi kumlazimisha kama akikataa mwenyewe.

Diamond amekuwa akihusishwa kimapenzi na Hamisa kwa muda mrefu licha ya yeye kuendelea kukataa. Hamisa  hajamuweka wazi mpaka sasa baba wa mtoto wake, licha ya kuwa kutangaza arobaini ya mtoto itakayofanyika hivi karibu ambapo bila shaka baba wa mtoto atajulikana.

 

Diamond Platnumz asaini dili nono

Msanii machachari wa Bongo fleva Diamond Platnumz amelamba shavu nono la kuingia mkataba wa kibiashara na kampuni ya vinywaji vikali ya Luc Belaire ya nchini Ufaransa, ambapo Diamond amekuwa mmoja kati ya mabalozi wa kinywaji hiko.

Kupotia ukurasa wa instagram wa kampuni ya kinywaji hicho wamethibitisha kuwa Diamond atakuwa mwanafamilia mpya kwenye kuitangaza bidhaa hiyo, pia kupitia ukurasa wake wa instagram Diamond mwenyewe amethibitisha hayo.Pia ataungana na mastaa kibao duniani ambao pia ni mabalozi wa bidhaa hiyo akiwemo rapa maarufu kutoka Marekani Rick Ross ambaye pia kupitia ukurasa wake wa instagram alimkaribisha Diamond kwa kuandika “Self Made Tastes Better” caption iliyoambatana na picha ya Diamond Platnumz.

Dili hilo ambalo halijawekwa wazi ni kiasi gani Diamond ataingiza baada ya kusaini na kampuni hiyo, lakini huenda ikawa ni dili la mamilioni ya fedha kwani Rick Ross ambaye ni Balozi wa Belaire anakadiriwa kulipwa kiasi cha Dola za kimarekani milioni 4.1 ambayo ni zaidi ya bilioni 8 za kitanzania.

Diamond ataungana na wasanii maarufu ambao nao ni mabalozi kama Dj Khaled, Rick Ross pia mlimbwende kutoka Kenya Huddah Monroe pia ni moja ya wanafamilia wa Belaire.

Aslay aeleza kwanini hawezi kubali kusainiwa Wasafi

Dogo Aslay ambaye yuko katika lebo ya Mkubwa na Wanawe amefunguka na kusema kuwa hawezi kubali kujiunga na lebo ya Diamond Platnumz – Wasafi.

Staa huyo wa Yamoto Band ambaye ameanza kutoa nyimbo zake binafsi amesema kuwa malengo yake yamezidi kuwa msanii wa Wasafi ya Diamond.

Aslay

Aslay alieleza kuwa mipango yake ni kufikia kiwango cha Diamond na Ali Kiba kwa hivyo hawezi kusainiwa na Wasafi kama anataka kufikia malengo yake.

“Kusainiwa WCB hapana, kwa sababu mimi nina ndoto za kuwa zaidi ya WCB au kuwa zaidi ya kitu kingine chochote, naamini nitakaza nitafika hizo sehemu, naweza kusema nina ndoto za kufika kama alipofika Chibu, nina ndoto za kufika kama alipofika Ali Kiba. Inabidi nikaze niwe mimi kama mimi nitafute njia ya kutoboa nifike level hiyo, yaani sio yeye pekee yake mtu yeyote, wakisema wanisaini siwezi kukubali sasa hivi”  Aslay alisema katika kipindi cha XXL ya Clouds FM.

 

“Mimi sihitaji sifa za kijinga” Hamisa Mobeto aweka wazi ishu ya kupachikwa mimba na Diamond

Hamisa Mobeto amefunguka kuhusu madai kuwa msanii Diamond Platnumz ndo baba wa  mtoto anayembeba tumboni mwake.

Mrembo huyo aliweka wazi kuwa Diamond hakumpachika mimba, alisema hawezi tambua hadharani nani ndo baba wa mtoto wake mtarajiwa kwasababu hayo ni mambo yake ya kibinafsi.

“Huu uvumi unataka niweke wazi maisha yangu. Hilo halitajitokeza kwangu kwani mtu akishaumwa na nyoka akimuona mjusi anamuogopa. Baba wa mtoto wangu mtarajiwa namjua mimi na familia yangu. Nadhani inatosha.

“Sidhani kama ni lazima nimtaje kwenye media (vyombo vya habari) lakini wale wanaosema ni Diamond tafadhali sana, siye. Baba wa mtoto wangu yupo na sio matangazo ya biashara kila mtu majue mpenzi wangu.

“Hao wanaotutukana mbona maisha yao wameyaweka siri, au mimi tu ndiyo nijianike? Siwezi kufanya hivyo, najua nachokonolewa ili niseme lakini sitasema,” amesema Hamisa.

Hamisa pia alikana madai kuwa anatafuta kiki kwa kutumia jina la Diamond, alisema yeye haitaji sifa za kijinga.

“Maisha yangu binafsi yatabaki kuwa yangu mimi mwenyewe ila ya kibiashara yatajulikana na kila mtu. Mimi kwa sasa sihitaji sifa za kijinga, nahitaji mashabiki zangu wafahamu nafanya nini katika jamii na wanishabikie hivyo, sio kwa maisha yangu binafsi.

“Kuruhusu ushabiki katika maisha yako binafsi hasa ya mapenzi ni kujijengea uadui na marafiki wa uongo ambao wengi wao wanakuja kinafiki na kujifanya wanakufahamu kiundani au mpenzi wako kumbe ni waongo. Wanataka kuwavuruga na wakifanikiwa hutawaona,”alisema Hamisa.

 

Hamisa Mobetto aandika ujumbe ambao umewaacha wengi wakijiuliza Kama mtoto anayemtarajia ni wa Diamond Platnumz

Hamisa Mobetto ameonyesha kuwa yeye hamuogopi mtoto yeyote ata Zari Hassan ambaye ni ‘mke’ wa Diamond Platnumz na mama ya watoto wake wawili.

Hii ni baada ya mrembo huyu kuandika ujumbe ambao umewaacha wengi wakijiuliza ikiwa mtoto anaye mtarajia ni wa Diamond Platnumz. Mrembo huyu aliandika kusema,

Mama Daa…? Mama dee…? Mama dii..? Mama doo..? Mama duh..?

Kulingana na mashabiki wa mrembo huyu, kuna unawezo kuwa Hamisa Mobetto alikasirishwa na video ambazo Zari aliwachia Jana kwenye Instagram yake – huku akionekana akitabasamu Diamond akimchezea gitaa wakiwa wawili huko Afrika Mashariki.

Hata hivyo hii sio mara ya kwanza ya Mobetto kufanya jambo kama hili kwenye mitandao yake ya Instagram. Ingawa hapo awali Diamond Platnumz alikuwa ameilana mimba hiyo….kwa hivi sasa hakuna uhakika nani anasema ukweli.

Tazama post hiyo hapa;

Hii ndiyo sababu ya Diamond kukosa kuhudhuria matanga ya Ivan licha ya kudhibitisha awali kuwa angehudhuria

Akiongea kwenye kipindi ya The Trend ya NTV Kenya Ijumaa iliyopita, Diamond Platnumz alisema kuwa atasafiri kuenda Uganda kuhudhuria matanga ya Ivan Ssemwanga baada ya kumaliza show yake Nairobi.

“Well kwa ukweli ulikua ni wakati mgumu na mbaka saa hivi ni wakati mgumu kwasababu nlikua nko booked muda kidogo kuhusiana na Korogo festival, na msiba umetokea sasa kucancel tu ghafla show ya watu unajua inawezekana ukapata taswira tofauti, wengine wakachukua tofauti. Sikua na jinsi. So, lakini nliongea na mzazi mwenzangu (Zari) akanielewa, lakini nikimaliza hapa show tu na ntaenda Uganda kwasababu ya mazishi, kuzika. Baada ya hapo ndo ntarudi nyumbani,” Diamond alisema.

Lakini hata hivyo jana Simba hakuonekana kwa matanga ya Ivan, kwasababu gani? Meneja wa Diamond Sallam Sharaff alisema kuwa msanii huyo hangeweza kusafiri kwenda kumzika Ivan kutokana na ratiba kuingiliana.

“Kwenye mazishi hatujahudhuria, ilikuwa twende leo alfajiri lakini sasa kumbe wao wametoka usiku kwenda kijijini. Kwa hiyo nadhani ratiba yetu imeingiliana maana na sisi tulitoka Nairobi jana jioni.” Sallam alikiambia kipindi cha U-heard cha Clouds FM.

Skiza Sallam akielezea kwanini Diamond hakuweza kusafiri kuenda kumzika Ivan hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=elxy8DgyaFo

Diamond aeleza kwanini hajawai achia collabo na Zari

Je, unajua kuwa Zari Hassan alikua mwimbaji kabla ya kukutana na Diamond? Mashabiki wa Zari walitaka kujua kwanini Diamond hajamsaidia Zari kufanikiwa kimuziki kama anavyowasaidia wasanii wengine.

Akihojiwa katika kipindi cha the Trend ya NTV ya Kenya, Diamond alieleza kwanini hajampiga jeki mkewe kimuziki; swali hizo liliulizwa na mwanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi.

Simba alisema kuwa Zari alikuwa ashawacha kuimba walipokutana, alieleza kuwa kama Zari bado angekua mwimbaji labda hawagekuwa pamoja kwasababu ya songombingo ya muziki.

Tazama video hapo chini uone mahojiano yote:

Picha 10 za Dogo Janja ambazo ni dhibitisho kuwa anang’ara kimavazi kushinda Diamond Platnumz

Muonekana wa Dogo Janja dhibitisho kuwa mwanamuziki huyo amewekeza pesa na muda katika mavazi. Dogo Janja sasa anashindana na Diamond kung’ara.

Msanii Madee alisema kuwa Dogo Janja amefanikiwa katika uvaaji kwa asilimia 92, alifunguka na kusema kuwa alikaa na Dogo chini na kumshauri

“Hicho ndio kitu tulijaribu kumshauri Janja na tukakaa naye vizuri na kumueleza na ndio kitu amefanya na amefanikiwa kwa asimilimia 92 na baada ya siku kadhaa naamini tutafika kule ambapo tunataka Janja awe na ule muuonekano,” Madee aliambia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio.

Picha hizo hapo chini ni dhibitisho kuwa anang’ara kimavazi kushinda Diamond Platnumz:

Ujumbe Ne-Yo alitoa baada ya Diamond Kuzindua Chibu Perfume

Wiki iliyopita Diamond alizindua manukato yake ya Chibu perfume katika sherehe moja pale GSM ambayo ilihudhuriwa na washika ndau wengi pale Tanzania.

Watanzania wengi na watu wengio humo nje walimpigia kifua kwa kujikakamua na kumtia motisha aendelee hivo hivo.

Mmoja wao alikuwa msanii wa Marekani ambaye alimpigia debe aendelee na kazi mzuri aliyoianza.

Mtazame Diamond akielezea hilo kwenye interview na Millard Ayo: