Zamaradi Mketema Akana Kabisa Kuajiriwa Wasafi Tv

Mtangazaji na Mdau mkubwa wa tasnia ya Bongo movie Zamaradi Mketema ameibuka na kukataa kata kata kuwa amewahi kuajiriwa na kituo cha televisheni cha Wasafi Tv.

Miezi michache iliyopita Baada ya Zamaradi kuachana rasmi na Clouds Media alikokuwa anafanya kazi kwa muda mrefu alianza kuonekana na Mkurugenzi wa Wasafi Tv Diamond Platnumz na kuaminika kuwa ataanza kufanya kazi katika kituo hiko.

Lakini sasa Zamaradi anakataa na kusema kuwa tofauti na watu wengi wanavyoamini yeye hajawahi kuajiriwa na Wasafi bali aliingia nao mkataba wa kufanya nao kazi kama mtu anayejitegemea.

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa Dizzim Online, Zamaradi alifunguka hay kuhusu ishu yake ya kufanya kazi na Wasafi:

Kwani ni lini nilisema nipo Wasafi au sio huko Wasafi Tv ni partners tu na sijawahi kuajiriwa kokote na hii nilishawahi kuongea zaidi ya mara mia”.

Zamaradi alikana pia tetesi za kuwa amegombana na Diamond ndio maana mkataba Wake na Wasafi umevunjwa:

Sio kwamba tumeachana kuna project zipo zitakapokuwa tayari tutaendelea kufanya kazi kama kawaida kwahiyo siyo kwamba niliajiriwa  nikavunja mkataba au walikuwa wameniajiri wakanivunjia mkataba siajwahi kusaini mkataba na mtu yoyote wa ajira”.

 

Diamond Platnumz na Rayvanny Wafungiwa Kufanya Show Ndani na Nje Ya Nchi

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Rayvanny kutokea katika Label ya WCB wamefungiwa rasmi kutofanya show ndani na nje ya nchi kwa muda usiojulikana.

Baraza la  Sanaa Tanzania (BASATA) limetangaza kuwafungia Diamond na Rayvanny Baada wawili hao kukiuka masharti waliyopewa.

Taarifa  iliyotolewa leo Desemba 18, 2018 na BASATA,  imesema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya wasanii hao kuonyesha dharau kwa mamlaka zinazosimamia shughuli za sanaa nchini, kwa kufanya vitendo vinavyokiuka maadili.

Kwa upande mwingine, BASATA  wamefuta kibali cha Tamasha la Wasafi Festival linalotarajiwa kufanyika nje ya nchi baada ya kuzunguuka kwenye baadhi ya mikoa hapa Tanzania.

Imeelezwa kuwa wimbo wa Mwanza ndio uliowaingiza matatani, baada ya wasanii hao wikiendi iliyopita kuonekana jukwaani katika Tamasha la Wasafi Festival jijini Mwanza wakitumbuiza wimbo huo.

BASATA Kuwashughulikia Diamond na Rayvanny Baada Ya Kupiga ‘Mwanza’

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) linefungukia kitendo cha Wasanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Rayvanny kuperfom wimbo wao wa Mwanza ambao umefungiwa.

Mwezi uliopita Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) walitangaza kuufungia rasmi wimbo wa ‘Mwanza’ kwa madai kuwa wasanii hao wamekiuka maadili ya Kitanzania kwa maudhui ya wimbo huo.

Diamond aliimba wimbo huo alioshirikishwa na Rayvanny jana Desemba 15, 2018 katika tamasha la Wasafi lililofanyika jijini Mwanza jana, huku maelfu ya mashabiki wakimshangilia na kumfuatisha alivyokuwa akiimba. Mkali huyo wa Bongo Fleva aliimba wimbo huo  akiwa pamoja na Rayvanny.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Katibu mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza alifungukia ishu hiyo na kusema:

Nimepigiwa simu kuhusu hii kitu. Niko Arusha kikazi nimeshawasiliana na mwenyekiti wa bodi (ya Basata).

Basata itakuja na majibu muafaka kwani hapa (Diamond) kaonyesha kiwango cha juu cha dharau kwa baraza, bodi, wizara (Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo) na Serikali kwa ujumla”.

 

 

Baba Diamond Atoa Neno Kuhusu Ndoa Ya Diamond na Tanasha

Baba mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma maarufu kama Baba Diamond amefungukia Ndoa Ijayo kati ya Mwanaye Diamond na Mpenzi Wake Tanasha Donna.

Wiki chache zilizopita Diamond alitangaza rasmi kwenye mitandao ya kijamii dhamira yake ya kumuoa mrembo kutoka nchini Kenya, Tanasha Donna ‘Zahara Zaire’ ifikapo Februari mwakani na kufanya watu wengi kuwa na hamu ya kushuhudia harusi hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi, Baba Diamond amesema ingawa Mpaka sasa hajapewa taarifa kuhusu Ndoa ya mwanaye lakini anatamani siku ya Ndoa wamualike.

Sijaambiwa habari za ndoa ila nasikia tu watu mitaani wanazungumzia suala hilo, kikubwa naomba iwe ya heri Mungu afanikishe nitafurahi sana mwanangu akioa lakini namuomba sana asiache kunialika, asiponialika nitaona amenidharau sana, nitajisikia vibaya”.

 

Natafuta Mwanaume Ambaye Atakuwa Baba Kwa Watoto Wangu-Zari

Mfanyabiashara maarufu Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’ na mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amefunguka na kuweka wazi tangu ameachana na Diamond amekuwa akitafuta mwanaume ambaye atakuwa kama baba kwa Watoto Wake.

Baada ya mahusiano ya takribani miaka minne Zari alimtosa Baba Watoto Wake Diamond mapema mwaka huu katika siku ya wapendanao tena kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Sasa Zari ameweka wazi kuwa tangu aachane na Diamond  ameshakuwa na mahusiano na wanaume kadhaa lakini hivi sasa anataka mwanaume ambaye atakuwa mfano bora wa baba kwa  watoto wake wa kiume na mwanaume ambaye binti yake wa kipekee atatamani kuwa mfano wa mwanaume wa kuolewa naye.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari ameandika maneno haya:

BASATA Waibuka na Kumpongeza Diamond Platnumz

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) wamempongeza Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz Baada ya msaada aliotoa mkoani Sumbawanga alipokuwa kwenye shoo.

Sio Siri kuwa uhusiano wa Diamond na BASATA umekuwa wenye misukosuko kwani Wiki chache tu zilizopita msanii huyo alionekana akiwasihi Baraza hilo lisifungie nyimbo yake mpya ‘Mwanza’.

Baraza hilo limeamua kumpongeza Diamond Baada ya Shughuli za kijamii alizofanya mkoani Sumbawanga ikiwemo kuhaidi kutoa zaidi ya Milioni 68 kwa ajili ya kujenga shule ya msingi.

Kipitia ukurasa wao wa Instagram, Baraza hilo limeandika ujumbe huu:

Diamond, Rayvanny na Mbosso Wapata Ajali Stejini Sumbawanga (+Video)

Msanii wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Diamond Platnumz na wasanii wenzake Rayvanny na Harmonize walipata ajali katika Steji ya Wasafi Festival iliyokuwa inafanyika mkoani Sumbawanga.

Shoo hiyo ilifanyika siku ya jana 9 Desemba katika uwanja wa Nelson Mandela ambapo wasanii hao walikuwa wanaperfom wimbo wao pendwa kabisa wa ‘Zilipendwa’ lakini ndipo balaa lilipotokea Baada ya wasanii hao kula mieleka.

Lakini baada ya kudondoka kwa Diamond akifuatiwa na Mbosso wasanii hao waliinuka na kuendelea na shoo na iliripotiwa kuwa hakuna Msanii aliyepata majeraha makubwa zaidi ya michubuko ya hapa na pale.

Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale alitoa taarifa kuwa wasanii hao wanaendelea vizuri na hakuna aliyeumia.

Baada ya sakata hilo Kupitia ukurasa Wake wa Instagram, Diamond Platnumz aliposti video hiyo na kuandika:

https://www.instagram.com/p/BrK67ZVlDFX/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=d9geezbdwlgj

“Nampenda Sana Wifi Yangu Tanasha”-Esma Platnumz

Dada wa staa wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz, Esma Platnumz ameibuka na kusema hana neno na wifi yake mpya Tanasha Donna Oketh.

Wiki iliyopita Diamond alimtambulisha Mpenzi Wake Mpya na mara moja kutangaza kuwa ana mpango wa Kumuoa itakapofika mwakani tarehe 14 February.

Kwenye mahojiano na Gazeti la Risasi, Esma ambaye alikuwa beneti na Tanasha alifunguka kuwa kwa upande wake alimpokea wifi yake mpya kwa mikono miwili.Esma ambaye amepachikwa jina la Yuda mitandaoni kutokana na kuwageuka warembo ambao huwa wanakuwa na Diamond kisha kupigwa kibuti alisema:

Wala sina shida, nimemkubali wifi yangu na kwa sababu Nasibu (Diamond) mwenyewe ndiye amesema anamuoa na ameridhiana naye, mimi ni nani nikatae?

Kikubwa ninawaombea heri tu asiwe kama wengine ili na mimi nipate wifi wa halali, niache uyuda”.

Mashabiki wameituhumu familia ya Diamond kwa unafiki kwani Wiki mbili tu zilizopita walionekana na Kim Nana na hata Mama Diamond alisema mume Wake anamfundisha dini ili aweze kubadilisha dini na kuolewa na Diamond.

Ujumbe Wa Diamond Kwa Nillan Siku Ya Birthday Yake

Msanii wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz ameandika ujumbe mzito kwa Mtoto Wake aliyezaa na Zari The Bosslady Prince Nillan ikiwa ni siku yake ya kusheherekea birthday yake.

Siku ya Leo Nillan anafikisha umri wa miaka mieili pamoja na kuwepo maneno Mengi kwenye mitandao ya kijamii tangu anazaliwa kuwa sio Mtoto wa Diamond lakini Diamond amesema siku zote ni Mtoto Wake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond amemuandikia ujumbe mzito mtoto wake huyo na kusema:

Miaka miwili iliyopita Mungu alinibariki na Mtoto wangu wa kwanza wa kiume naye nilimuita jina la Nillan linalomaanisha Mwezi/ Asili/ Umaarufu/ Handsome na ni handsome kweli anayeng’aa zaidi ya nyota Happy Birthday Nillan Baba anakupenda”.

https://www.instagram.com/p/BrBZIwGl_mW/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=3ugwerk3u8km

“Bora Kufanya Kazi na Diamond Kuliko Alikiba”-Gigy Money

Video vixen maarufu na Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gift Stanford kwa jina la usanii Gigy Money amefunguka na kuweka wazi kuwa ni bora kufanya kazi na Diamond kuliko Ali Kiba.

Gigy Money ambaye Hivi sasa anaonekana akiwa amejiunga pamoja na Kundi zima la Wasafi linaloongozwa na Diamond Platnumz ili kushiriki katika tamasha lao la Wasafi Festival.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Gigy Money ameibuka na kudai kuwa ameona kuna ubora mkubwa wa kufanya kazi na Diamond kuliko kufanya kazi na hasimu Wake Ali Kiba.

Ali Kiba anakunja sana kuliko Diamond  na siku ambayo tulienda kufanya wote shoo Kahama Ali Kiba alinitenga kabisa Backstage”.

Wiki mbili zilizopita Diamond Platnumz na Ali Kiba walifanya shoo zao usiku mmoja ambapo Ali Kiba alipiga shoo mkoani Shinyanga/Kahama na Diamond alipiga shoo yake mkoani Mtwara.

Joseph Kusaga Ajibu Tuhuma Za Kumiliki Wasafi Tv na Radio

Mfanyabiashara maarufu na Mkurugenzi wa Vlouds Media Group Joseph Kusaga amejibu tetesi zinasombaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kumiliki vituo viwili vya runinga na radio, Wasafi TV na Wasafi FM.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Clouds 360 cha Clouds Tv, Joseph Kusaga amefunguka kuwa yeye anamiliki karibia vituo vyote vya radio za vijana hapa Tanzania.

Hapana mimi sitakwenda huko, mimi  namiliki radio zote za vijana, radio zote za vijana mimi namiliki, kwa njia moja au nyingine, ukimuita Seba atakwambia umenielewa. Lakini labda ni kwa sababu ya kuongeza wigo, labda wigo wetu sisi unaweza ukawa hautoshi, mimi nashiriki kwenye industry yote ya burudani”.

Lakini pia Kusaga alipoulizwa kuhusu umiliki wa Wasafi Tv na Radio hakutaka kuweka wazi kuwa anamiliki zote lakini badala yake alisema anamiliki redio nyingi za vijana hapa nchini ikiwemo Jembe Fm ya Mwanza na Safari Fm ya Mtwara.

Wiki iliyopita kwenye Gazeti moja Kuna taarifa ilichapishwa kwamba Mke wa Kusaga anamiliki nusu ya hisa za Wasafi Tv na Radio na hata Mitambo ya Wasafi inawashwa Clouds Media.

Diamond Atia Neno Baada Ya Naibu Waziri Kucheza ‘Mwanza’

Msanii wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ameibuka na kutia neno Baada ya video iliyomuonyesha Naibu Spika Dr. Tulia Akson akiwa anacheza na kuimba wimbo wa ‘Mwanza’ uliofungiwa.

Mwezi uliopita Baraza la Sanaa Tanzania liliufungi rasmi wimbo wa ‘Mwanza’ ulioimbwa na Diamond Platnumz kushirikiana na Rayvanny kwa madai ya kukiuka maadili ya Kitanzania.

Siku chache zilizopita video iliyowaonyesha viongozi mbali mbali wa Bunge ikiwemo Dr. Tulia wakicheza wimbo wa Mwanza wakiwa anasheherekea ushindi wake dhidi ya Uganda ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii na kuzua gumzo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond ametoa neno kuhusu video  hiyo huku akimshukuru sana kwa sapoti:

https://www.instagram.com/p/Bq7C-71lEan/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=3zs8izof9c0q

Diamond Platnumz Aanika Ndege Mpya Ya Wasafi Festival

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini na CEO wa WCB Diamond Platnumz ameitambulisha ndege ambayo itakuwa na jukumu la kubeba wasanii Watakaoperfom perfom kwenye stage ya Wasafi Festival Mombasa.

Ndege hiyo inadaiwa kuandaliwa na waandaaji wa shoo hiyo ambapo watatumia wasanii wa WCB kuwachukua jijini Dar na kuwapeleka Mombasa maalum kwa ajili ya shoo huku wengine wakidai amenunua Diamond japo mwenyewe bado hajaweka wazi kama ni ya kununua ama ya kukodi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond ameandika maneno haya:

Diamond Atangaza Kumuoa Mrembo Kutoka Kenya

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka WCB Diamond Platnumz ametangaza kufunga ndoa na mrembo ambaye ni mwanamitindo kutoka Kenya Anayejulikana Kama Tanasha Donna Barbier.

Diamond ametangaza ndoa na mrembo huyo Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa ambapo Alikiri kuwa kwenye mahusiano na mrembo huyo ambaye ni mtangazaji wa Radio NRG ya jijini Mombasa nchini Kenya.

Diamond alisema kuwa, mara baada ya kuachana na mzazi mwenzake ambaye alizaa naye watoto wawili, Princess Tiffah na Prince Nillan, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, wasichana wengi ‘aliowatokea’ na hata Zari mwenyewe hawakulichukulia jambo la ndoa kwa uzito kama alivyofanya Tanasha.

Tanasha ndiye mwanamke pekee aliyeonesha kujali na uzito juu ya jambo hilo hivyo rasmi natangaza kumuoa huyu.

Lakini nimejiridhisha kwamba mbali na umbo na mvuto wa kipekee pia ni mwanamke mwenye tabia nzuri.”

Alipoulizwa juu ya uwepo wa Tanasha kwenye ufunguzi wa Tamasha la Wasafi Festival mjini Mtwara, Diamond alifunguka kuwa ni kweli alikuwepo, lakini watu wengi hawakumjua kutokana na usiri uliokuwepo wa kumuonesha kabla ya yeye mwenyewe kumtambulisha alipokuwa stejini.

Nitakuwa na shoo kesho nchini Kenya katika Mji wa Thika ambapo Tanasha atanitambulisha rasmi kwa wakwe zangu“.

Diamond amesisitiza kuwa Tanasha ndiye mwanamke pekee ambaye amejikuta kweli ana vigezo vyote vya kuwa mke wake pamoja nakwamba siku za Nyumba alishawahi kutangaza ndoa na maex  zake kama Zari, Wema, Penny na Jokate.

Young Killer Adai Wasafi Festival ni Ukombozi Wa Kweli Kwenye Burudani

Msanii wa muziki wa hip hop nchini Young Killer ameibuka na kulimwagia sifa kibao Tour ya WCB ya Wasafi Festival Baada ya kushiriki katika tamasha Lao la kwanza mkoani Mtwara.

Young Killer Msodoki amefunguka kwa kulisifu tamasha la Wasafi Festival na kudai kuwa ni ukombozi halisi katika sekta ya Burudani Nchini Tanzania.

Katika mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Young killer amefunguka haya zaidi kuhusu shoo hiyo:

Ujio wa Wasafi Festival ni mkubwa na umekuja kiutofauti sana na kiukweli tasnia yetu inahitaji vitu kama hivi kwa sababu haya ni mapinduzi kwani muda mrefu tumekuwa tukimiss matamasha yamekuwa machache kwaiyo kuja kwa Wasafi Festival ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwani inaonyesha ni kwa jinsi gani Sanaa yetu hivyo Big Up sana kwa Wasafi”.

Young Killer pia atakuwa mmoja wa wasanii Watakaoperfom kwenye shoo nyingine ya Wasafi Festival itakayofanyika Mkoani Iringa siku ya Leo.

Diamond Ruksa Kumuoa Kim Nana-Lynn

Video vixen aliyejizolea umaarufu Kupitia kichupa cha wimbo wa ‘Kwetu’ wa Msanii Rayvanny, Irene Hillary maarufu kama Lynn amefunguka na kusema ni ruksa kabisa Kwa Diamond kumuoa Kim Nana.

Lynn alifunguka hayo siku chache Baada ya warembo hao wawili wanaosemekana kufaidi Penzi la staa huyo wa Bongo fleva kugongana katika shoo ya Wasafi Festival mkoani Mtwara.

Gazeti la Risasi linaripoti kuwa warembo hao ni Kama paka na panya kutokana na wote kumpenda staa huyo hivyo walivyokutana Mkoani Mtwara kila mmoja alipooza na kuonekana wakiangaliana kwa jicho la uhasama.

Kama utakuwa uliwafuatilia walipopanda jukwaani utakuwa uliwashuhudia walivyokuwa wakikatana jicho la ukali.

Lakini Kim anaonekana kuibuka kidedea maana tofauti na Lynn, yeye alionekana mwenye furaha huku akikata nyonga kuashiria hakuwa na stresi kama mwenzake.

Hata wakati wa kurudi Dar, Lynn alipanda gari la wanenguaji na njiani alionekana kabisa hana furaha, tofauti na Kim aliyepanda kwenye gari moja na wanamuziki wa Wasafi na kujitwalia mapozi kama yote hivyo kumaliza kabisa umalkia wa Lynn ndani ya Wasafi”.

Baada ya tetesi hizo za kuwepo wivu wa kimapenzi Lynn alipiga stori na Gazeti hilo na kufunguka kuhusu  mahusiano yake na  Diamond na Kim Nana.

Unajua kuna kitu watu hawakijui kuhusu mimi na Diamond. Mimi na Diamond hatua uhusiano wowote ule.

Diamond ni mshkaji wangu sana kwa hiyo hata akimuoa Kim haiwezi kuniuma kwa sababu atakuwa wifi yangu na nimebariki amuoe tu wala sina tatizo lolote,