Diana Azungumzia Mapenzi ya Jinsia Moja na Wema

Mwanadada Diana Kimari amefunguka na kuongelea swala la kuwa na mahausiano ya mwanadada mwenzake wema sepetu mpaka kufikia hatua ya kumchora tatoo ya jina lake mwilini.

Diana ambae aliwahi kusemwa sana kutokana na maamuzi hayo, anasema kuwa hajawahi kujihusisha na mahusiano ya jinsia moja kama watu wanavyosema lakini amekuwa akimpenda sana mwanadada huyo na wala haoni shida kuchora tatoo ya mwanadada huyo.

Diana anasema kuwa kitu icho aliwahi kukisiakia lakini hajwahi kukifanya nahata ntetesi za kuwa yeye anafanya pia anazisikia lakini amekuwa akinyamaza kimya kwa sababu hazina ukweli wowote.

Diana anasema kuwa katika maisha yake haoni kama kuna haja ya kumchukia au kumuongelea wema vibaya kwa sababu amekuwa moja ya watu wenye upendo wa kweli kwake kama mdogo wake na hajawahi kufanyiwa kitu kibaya na wema sepetu hivyo hakuwahi kufikiria kitu anaweza kumpa kumsgukuru zaidi ya kuweka alama kwake.

Hata hivyo Diana anasema kuwa kama kuchora tatoo hiyo ni kosa basi anamuomba Wema amsamehe kwa sababu hawezi kuifuta kutokana na shughuli yenyewe ya kuchora tattoo na kufuta ni ngumu lakini pia kwa sababu alichora kwa upendo.