Irene Uwoya Ajutia Ndoa Yake na Dogo Janja

Muigizaji wa Bongo movie mrembo Irene Uwoya ameibuka na kuwashauri wanawake wasije wakaolewa na wanaume ambao mioyo yao haijaridhia.

Kama utakumbuka mwaka juzi Irene Uwoya alishangaza kila mtu Baada ya kufunga ndoa na msanii wa Bongo fleva Dogo Janja Lakini ndoa hiyo ilidumu kwa miezi michache na hatimaye kuvunjika.

Lakini hivi sasa Uwoya ameibuka na mapya ya kuiponda ndoa hiyo na Dogo Janja Kwa kudokeza kuwa aliolewa na Dogo Lakini kiuhalisia ni kwamba hakumpenda hata kidogo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Uwoya alisema hiyo imewahi kumtokea akaolewa na mwanaume ambaye hakumpenda kitu ambacho kilimtesa hivyo wanawake wasiolewe ili tu waonekane nao wameolewa bali waingie kwenye ndoa na watu ambao wamewapenda kwa dhati.

Jamani wanawake wenzangu hakuna kitu kinachotesa kama kuolewa na mwanaume ambaye moyoni mwako hayupo, ni mateso makubwa hiyo ilishanitokea kwa hiyo nawasihi msijaribu kufanya hivyo kwani naamini ukitaka kuifurahia ndoa ni kuolewa na mwanaume unayempenda”.

 

Nipo Tayari Hata Kuhudhuria Harusi Ya Dogo Janja- Uwoya

Muigizaji wa Bongo movie na mrembo anayetrend Hivi sasa kwenye Mitandao ya kijamii Irene Uwoya ameibuka na kusema kuwa hana tatizo na aliyekuwa mume Wake Dogo Janja.

Irene Uwoya na Ex Wake staa wa Bongo fleva Dogo Janja waliweka wazi kuwa wameachana siku chache zilizopita baada ya kuwa kwenye ndoa kwa miezi kadhaa.

Baada ya kuingia kwenye mvutano mkali Wiki iliyopita na hata kurushiana madongo kwenye Mitandao ya kijamii hatimaye Uwoya amesema hana Bifu na Dogo Janja na Hivi sasa ana maisha yake na hata ikitokea amealikwa kwenye engagement party ya Dogo na Mpenzi Wake Mpya ataenda.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Uwoya ameweka wazi kuwa Ndoa Yake na Dogo Janja imevunjika Lakini sio kitu cha ajabu kwani ndoa nyingi zimeshawahi kuvunjika katika siku za nyuma.

Wolper Adaiwa Kumkuwadia Dogo Janja Kwa Demu Mpya

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper ameibuka na kukana kabisa taarifa zinazodai kuwa amemsaliti rafiki yake Irene Uwoya kwa kumkuwadia shoga yake kwa Dogo Janja.

Dogo Janja ana ‘kifaa’ kingine kipya ambaye ni mtoto mkali, mkazi wa jijini Arusha aliyetajwa kwa jina moja la Linna. Baada ya kusambaa kwa video na picha za Dogo Janja ambaye ni msanii wa Bongo Fleva na Linna wakiwa kwenye mahaba mazito ndipo baadhi ya watu wakaibuka na kila mmoja kuanza kusema lake.

Dogo Janja na Mpenzi Wake Linah

Gazeti la Ijumaa linaripoti kuwa kwa sasa uhusiano wa Uwoya na Wolper hauko sawa. Kufuatia bango hilo kuwa na madai mazito ya Uwoya kupaniki huku Wolper akitajwatajwa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wolper alifunguka na kusema haya:

Kikubwa ninafurahi kwa sababu baada ya kupelekewa hiyo ishu, Irene (Uwoya) hakutaka kuamini kwani ananijua jinsi ninavyompenda na kumchukulia. Anajua siwezi kuwa snichi kwake kwani ninamchukulia kama ndugu yangu. “So hata alivyoambiwa alikuwa ndiye mtu wa kwanza kukataa mimi kufanya hivyo.

Anajua mimi siwezi unafiki ndiyo maana hujawahi kuona nikimposti Dogo Janja (kwenye ukurasa wake wa Instagram) na huyo demu ambaye ni mdogo wangu (Linna) maana nitakuwa mchawi. Yaani mchawi kabisa.

Na mimi ninamlaumu Dogo Janja maana Dogo Janja hajui undugu wangu na Linna kwa hiyo ninahisi alitumia uanaume wake kuni-block (mtandaoni). “Mpaka hapa ninakuambia huyo mdogo wangu, Linna siyo mteja wangu tena na hana tena ukaribu na mimi tangu awe na Dogo Janja.

Sasa nikisema Dogo Janja mchawi nitakuwa mwongo? Mchawi ni mtu mharibifu. “Nilishangaa sana kusikia eti mimi ndiye nimemkuwadia wakati Dogo Janja nilikuwa ninamchukulia kama mwanangu na alikuwa shemeji yangu (kwa Uwoya). “Hiyo skendo ndiyo imenifanya niwakalie kimya Linna na Dogo Janja maana Dogo Janja alikuwa rafiki yangu kabla hata ya kuwa na Irene (Uwoya) na huyo aliyenaye ambaye ni mdogo wangu kabisa.

Kinachoniuma sana ni huo uvumi ulivyotokea maana nilimuuliza huyo mdogo wangu (Linna) na Dogo Janja wakakataa katakata na meseji zao ninazo alafu eti leo hii ninaonekana…. (tusi) wakati Irene (Uwoya) ni rafiki yangu na ni mfanyakazi mwenzangu“.

 

 

Shilole- Sijapendezwa na Kitendo Cha Uwoya na Dogo Janja Kuachana

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefungukia taarufa za Msanii wa Bongo fleva Dogo Janja na mke Wake staa wa Bongo movie Irene Uwoya kuachana.

Baada ya Uwoya na Dogo Janja kufunga ndoa iliyozungukwa na utata mwaka juzi na kuachana mwaka jana mwishoni hatimaye wawili hao walithibitisha kuachana siku chache zilizopita Baada ya kurushiana maneno ya kejeli kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa Dizzim Online, Shilole amefunguka na kuweka wazi masikitiko yake Baada ya kusikia wanandoa hao wameachana ambao pia walihudhuria harusi yake na Uchebe:

Mimi kusema ukweli sijisikii vizuri kabisa kusikia kuwa wameachana hasa kwa sababu haya dini hairuhusu kuachana labda pale inapobidi sanaa Lakini pia huwezi kuingilia maamuzi ya watu.

Unajua kwenye ndoa kuna mengi Mimi na wewe hatuji Lakini wao waliopo humo ndani ndio wanajua nini kinaendelea kwaiyo ni vyema mara nyingi kuwaacha wao wenyewe wanandoa waamue wanachoamua”.

 

 

Dogo Janja na Uwoya Warushiana Maneno Mtandaoni

Msanii wa Bongo fleva Abdul Chande maarufu kama Dogo Janja na aliyekuwa mke wake staa wa Bongo movie Irene Uwoya wamerushiana maneno Kupitia Mitandao ya kijamii.

Ndoa ya Dogo Janja na Irene Uwoya inaonekana kuzidi kuchafuka zaidi kutokana na wanandoa hao kuweka maneno ya vijembe kwenye kurasa zao za kijamii huku zikitafsiriwa kwamba wanatupiana.

Sakata hilo limetokea siku ya jana ambapo katika ukurasa wa Instagram wa Msanii Dogo Janja, aliandika bora uonekane kwamba huna hela kuliko kutumia hela nyingi ili kuwaonyesha kwamba uko vizuri.

Katika muendelezo wa ujumbe wake, ‘hit maker’ wa Banana amerusha jiwe gizani kwa kutoa ushauri kwa mtu huyo anayedhaniwa kuwa ni mkewe, kwamba aache kuishi maisha ya kuigiza.

Acha Kufake Fake Life. Its better to live your real life hujazaliwa kufrahisha kila mmoja, Komaaa”.

Mashambulio hayo ya gizani ya Dogo Janja yanatafsiriwa kwa haraka kuwa yanakwenda kwa muigizaji Uwoya kutokana na aina yake ya maisha anayoishi na kwamba inadaiwa ni msanii anayeishi maisha ghali sana tofauti na biashara ya sanaa ilivyo kwa sasa nchini.

Ujumbe Wa Birthday Wa Dogo Janja Kwa Uwoya Waibua Maswali

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Dogo Janja amemtumia ujumbe wenye utata mke wake Staa wa filamu za Bongo movie mrembo Irene Uwoya alipokuwa anasherekea siku yake ya kuzaliwa.

Siku ya jana Irene Uwoya alikuwa anasheherekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake ambapo aliweka wazi kuwa alikuwa anafikisha umri wa miaka thelathini.

Lakini Uwoya alijikuta ikitengeneza headlines na mume wake Dogo Janja Baada ya posti yake kuibua maswali mengi hasa kwa sababu kuna taarifa kwamba wawili hao wameachana Baada ya miezi kadhaa ya ndoa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Dogo Janja alimposti Irene Uwoya kwanza kwa picha ambayo iliwahi kutumiwa kuwakejeli waliofunga ndoa kutokana na tofauti ya umri wao.

Post hii imewapelekea wengi kuhisi huenda wawili hao wamerudiana licha ya Skendo ya Wema na Dogo Janja iliyotokea miezi michache iliyopita iliyisababisha wawili hawa kuachana.

Sijawahi Kuacha Kumpenda Dogo Janja- Irene Uwoya

Muigizaji wa Bongo movie Irene Uwoya ameibuka na kudai kuwa pamoja na yote yaliyotokea lakini bado anampenda aliyekuwa mume Wake Msanii wa Bongo fleva Abdul Chende ‘Dogo Janja’.

Baada ya kufunga ndoa mwishoni mwa mwaka jana Irene na Dogo Janja walifikia tamati ya mahusiano yao mapema mwaka huu Baada ya Penzi Lao kugubikwa na wingu la usaliti wa kimapenzi.

Baada ya ndoa hiyo kuvunjika kumekuwa na maswali mengi ya tamati ya ndoa hiyo kwani hivi karibuni Uwoya amesikika akisema yeye hakubadilisha dini ili kufunga ndoa na Dogo Janja.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Irene Uwoya alipohojiwa endapo ameshapewa talaka yake na Dogo Janja Msanii huyo alijibu

Sijapewa talaka na Dogo Janja na sijawahi kuacha kumpenda hata siku moja, lakini maisha mengine lazima yaendelee na ndiyo maana nikasema sasa hivi niko bize kufanikisha ndoto zangu nyingi nilizokuwa nimejiwekea kwa muda mrefu.

Mambo hayo ya kuolewa niwaachie wengine mimi sitaki tena ndoa”.

Lakini pia Uwoya ameongelea utajiri ambao amekuwa akiuonyesha kwenye mitandao ya kijamii katika siku za Hivi karibuni:

Jamani tatizo la watu wengi wanapenda sana kuwaangalia watu kwa wasiwasi na wengi wanapenda sana kujua mtu anafanya nini au amepata wapi fedha. Sidhani kama ni sawa kuweka wazi kila kitu ambacho mtu anakifanya, kuna wakati mtu unakuwa kimya wao wanaona mambo yako tu yakinyooka”.

 

 

Irene Uwoya Adai Kuwa Hataki Kuolewa Tena

Msanii wa Bongo movie na mjasiriamali Irene Uwoya ameibuka na kuweka wazi kuwa hakuna kitu hataki kusikia maishani Mwaka kwa Hivi sasa Kama kuolewa tena au ndoa.

Uwoya amefunguka na kusema kuwa amefikia kwenye uamuzi huo kwani aliyokutana nayo ndani ya ndoa yameshatosheleza moyo wake hivyo kwa sasa yupo kwa ajili ya kuangalia maisha yake na si vinginevyo.

Katika mahojiano yake aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Uwoya alisema kuna vitu vingi anavyo moyoni, lakini pia anaona siyo vyema kuwapa watu faida na ndiyo maana alikuwa anakaa kimya kwa muda mrefu tangu kusambaa kwa habari zake za kuachana na Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’.

Kiukweli kabisa nimeapa moyoni mwangu sitaki kabisa kusikia kama kuna kitu kinaitwa ndoa kwa sababu nahisi hivyo vitu kwenye maisha yangu vimeshapita, sihitaji kuvirudia, naangalia maisha mengine ya kujiendeleza mwenyewe.

Kama sasa hivi nina kazi kubwa ya kumalizia pub (baa) yangu ya Last Minute (ipo Sinza-Mori, Dar). Kwa hiyo akili yote imeahamia huko”.

Irene Uwoya ameshaolewa ndoa mbili ambapo ndoa ya kwanza ilikuwa na Marehemu Ndikumana ambaye alizaa naye Mtoto mmoja na ndoa ya pili ilikuwa na Staa wa Bongo fleva Dogo Janja ambaye wameachana mapema mwaka huu Baada ya tetesi za kutokuwa na uaminifu.

Sheikh Mkuu Amjia Juu Uwoya Baada Ya Kutangaza Msimamo Wake Wa Kidini

Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Alhad Mussa amemjia juu Msanii wa Bongo movie Irene Uwoya baada ya kutangaza kwamba hakuolewa kwa dini ya Kiislamu na aliyekuwa mume wake, Dogo Janja.

Sakata hilo lilianza wiki iliyopita Baada ya Uwoya kutoa kauli iliyodai kuwa yeye sio muislam na wala hajawahi kubadilisha dini alipofunga ndoa ya kiislamu na Dogo Janja kama  watu wengi walivyodhania.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Amani Shekhe huyo alisema, kauli ya Uwoya kudai kuwa yeye si Muislamu inaonesha kuwa wakati akibadili hakuifuata dini bali mwanaume.

Mwanadada huyo kuchukua uamuzi wa kutaka kuolewa na aliyekuwa mwenza wake hakuridhia kutoka moyoni, hivyo katika ndoa hiyo Uwoya alimfuata mwanaume na wala hakufuata dini“.

Irene Uwoya alifunga ndoa ya Kiislamu na Dogo Janja na kutangaza kuwa, amebadili dini na kuitwa Sheila, hata hivyo baada ya miezi kadhaa wawili hao waliachana kimyakimya bila kuweka wazi ndoa yao kuvunjika.

Sijawahi Kubadilisha Dini Yangu na Kuwa Muislamu-Irene Uwoya

Muigizaji wa Bongo movie mrembo Irene Uwoya ameibuka na kuwatolea Povu zito watu ambao wamekuwa wakimhoji kuhusu kubadilisha dini Baada ya kuachana na Dogo Janja.

Mwaka jana Dogo Janja na Irene Uwoya walishangaza dunia Baada ya kutangaza wamefunga ndoa na kusema Uwoya amebadili dini amekuwa Muislamu na hata jina lake ni Sheila lakini Baada ya kuachana na Dogo Janja amesema hajawahi kubadilisha dini yake ya Kikristo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Uwoya amesema kwa muda mrefu amekuwa akisema kuwa hawezi kubadili dini yake ya Kikristo hivyo watu wafahamu kuwa yeye ni Mkristo na waondoe dhana kwamba alikuwa dini nyingine tofauti.

Nawashangaa sana watu kila kukicha wananiuliza umerudi kwenye dini yako ya awali kama kuna siku hata moja nilishawahi kuwaambia kuwa nimebadilisha dini yangu ya Kikristo yaani siwezi na sijawahi kujaribu”.

Dogo Janja na Uwoya waliachana mwezi uliopita Baada ya tetesi kusambaa kwamba Dogo Janja alichepuka na Msanii Wema Sepetu wakati yupo kwenye ndoa na Uwoya.

Young Killer Akanusha Kumtukana Uwoya

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Young Killer ameibuka na kukana tetesi zilizosambaa kuwa alimdhihaki Msanii wa Bongo movie Irene Uwoya kwenye moja ya nyimbo zake.

Tetesi hizo zilisambaa Baada ya maneno aliyoimba  kwenye moja ya nyimbo yake kuzua utata ambapo alinukuliwa akiimba “Sishangai Hawa pimbi wakinitukana ni kawaida Kama bibi na vijana”.

Kufuatia maneno hayo kwenye verse ya nyimbo yake mashabiki wengi walidhani amemtupia dongo Dogo Janja ambaye kwa kipindi hiko alikuwa kwenye ndoa na Uwoya na walikuwa Kama na Bifu na Young Killer.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari, Young Killer amekanusha dongo hilo kumlenga Uwoya na kuweka wazi kuwa vijana waliooa Vibibi ni wengi sana kwenye mitandao ya kijamii.

Sikumaanisha hivyo na sidhani kama Uwoya ni bibi kwa kweli Mimi kwanza sidhani kama Irene Uwoya ni bibi wapo wengi waliooa watu ambao ni mabibi wapo wengi hata mitandaoni tunawaona usimchukulie tu Dogo Janja au namna gani vipi hebu mtoe kuna watu wengine kibao”.

Ndoa ya Irene Uwoya na Dogo Janja ilipigwa sana vita kutokana na tofauti ya kiumri iliyokuwepo baina yao ambapo Uwoya alidaiwa kuwa mkubwa kuliko Dogo Janja.

 

“Uwoya Chaguo Lake Lilikuwa Ndikumana Sio Dogo Janja”-H.Baba

Msanii wa muziki wa Dansi nchini Hamisa Ramadhan maarufu kama H. Baba ameibuka na kutoa Nemo kuhusu mahusiano ya msanii wa Bongo fleva Dogo Janja na Alice Kuwa mke wake msanii wa Bongo movie Wema Sepetu.

H. Baba ambaye aliwahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na Uwoya miaka ya nyuma amedai Dogo Janja hakuwa type ya Uwoya Baya kidogo kwani yeye huwa anapendelea wanaume aina ya Marehemu mumewe Ndikumana.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, H. Baba alifunguka kuwa Dogo Janja na Uwoya  wasingeweza kudumu kwenye ndoa kwa sababu mwanamama huyo chaguo lake lilikuwa ni Ndikumana pia anapenda wanaume warefu wenye nguvu na miili ya mazoezi.

Unajua Uwoya chaguo lake lilikuwa ni Ndikumana ila Mungu alimpenda zaidi, kwa Janjaro sidhani kama atamuweza maana Uwoya anapenda wanaume warefu wenye nguvu na miili ya mazoezi.

Lakini pia H. Baba amemshauri Dogo Janja akomae kumuomba msamaha mrembo huyo kwani no mke wake halali wa ndoa:

Uwoya angenitema kama Dogo Janja ningeumia sana yaani ningeandamana kutoka Dar mpaka Mwanza kwa miguu maana mke anauma sana lakini  Namshauri Dogo Janja akomae kama ataweza ukomavu kurudisha penzi ila Uwoya ana maamuzi yake binafsi akisema sikutaki ndiyo kamaliza”.

 

 

Uwoya Afungukia Skendo Ya Dogo Janja na Wema Sepetu

Msanii wa filamu za Bongo movie mrembo Irene Uwoya amefungukia skendo ambayo ilikuwa inamkabili aliyekuwa mume wake staa wa Bongo fleva Dogo Jnja na Bongo movie star Wema Sepetu.

Wiki chache zilizopita habari zilienea kuwa ndoa ya Uwoya na Dogo Janja imefika mwisho baada ya Dogo Janja  kubanjuka na Wema Sepetu wakati bado akiwa kwenye mahusiano na Irene Uwoya.

 

Katika mahojiano na gazeti la Risasi Jumamosi, Uwoya amesema kuwa, hakuwa na muda wa kuwauliza chochote kwa sababu wote ni watu wazima. Uwoya amesema hana mpango wowote wa kuongea chochote kuhusiana na madai hayo kwa sababu kama waliamua kufanya hivyo (kutoka kimapenzi) ina maana hawakuwa vichaa, bali waliamua na walikubaliana hivyo kwa upande wake hawezi kufanya chochote.

Unajua mimi nipo bize, ninafanya mambo yangu, halafu tena nitenge muda mwingine wa kuwahoji watu wazima wanaojitambua kuwa kwa nini waliamua kutembea na kufanya mapenzi? Kwangu mimi hapana kabisa… sina muda huo, wangekuwa hawana akili nzuri ningesema sawa, lakini ni watu wenye akili timamu kabisa”.

Lakini pia Uwoya ameweka wazi kuwa yeye aliishia kuwatazama tu ili aone mwisho wao utakavyokuwa hivyo anashukuru mambo yamekuwa hadharani kwani yeye ndiye alikuwa akionekana mkorofi siku zote.

Alisema katika hali kama hiyo yeye aliishia kuwatazama tu ili aone mwisho wao utakavyokuwa hivyo anashukuru mambo yamekuwa hadharani kwani yeye ndiye alikuwa akionekana mkorofi siku zote.

Niliamua kuwaangalia tu mpaka mwisho kwani nina vitu vingi vya kufanya ambavyo vinaniumiza sana kichwa changu”.

 

Ndoa Ya Dogo Janja na Irene Uwoya Haijavunjika- Kassim Mganga

Msanii wa muzik wa Bongo fleva kutokea Tip Top Connection Kassim Mganga ameibuka na kudai ndoa ya staa wa Bongo fleva Dogo Janja na Mkewe Uwoya haijavunjika.

Kassim Mganga ambaye alikuwa mmoja kati ya watu wachache waliohudhuria ndoa ya Dogo Janja na Uwoya Mwaka jana mwishoni amesema hana taarifa ya ndoa hiyo kuvunjika.

 

Kwenye moja ya Interview alizofanya hivi Karibuni katika kituo kimoja cha habari Kassim amefunguka na kudai kuwa hajui kama Ndoa hiyo imevunjika kwa kuwa hajapata taarifa Rasmi.

Sina taarifa ya kuvunjika kwa ndoa kati ya Dogo Janja na Irene Uwoya ninachojua bado wako pamoja mpaka hivi sasa”.

Lakini pia Kwenye Mahojiano hayo Kassim amewataka watu wasimuonee wivu Diamond kwa ajili ya mafanikio anayoyapata kwani kiukweli amebadilisha sana muziki wa Bongo fleva.

Picha Za Irene Uwoya na Ommy Dimpoz Zazua Mazito

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali Irene Uwoya amekuwa  anatrend sana Kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kuvunjika kwa ndoa yake na staa Bongo fleva Dogo Janja.

Siku ya jana Uwoya amerudi Kwenye headlines kwa ajili ya picha zake alizopiga na msanii mwingine wa Bongo fleva Ommy Dimpoz.

Ommy Dimpoz ambaye alikuwa mgonjwa kwa Miezi kadhaa baada ya kufunyiwa upasuaji wa koo nchini Afrika ya kusini.

Siku ya jana wawil hao wamezua gumzo Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana wakiwa pamoja baada ya kila mmoja kiposti picha hizo Kwenye kurasa zao za Instagram.

Mashabiki wengi wa Uwoya walimtaka aanzishe Mahusiano na Ommy na kudai ndio anaendana naye kuliko hata Dogo Janja.

Wawili hao hawajaweka wazi sababu ya kuonekna pamoja kama ni wako ktika harakati za kuleta project ya pamoja au ni Mahusiano.

Wema Adaiwa Kuvunja Ndoa Ya Irene Baada Ya Kuchepuka na Dogo Janja

Staa wa filamu za Bongo Movie Wema Sepetu amekumbwa na skendo ya mwaka baada ya kudaiwa Kuvunja ndoa ya Msanii mwenzake Irene Uwoya na mume wake Dogo Janja.

Wema Sepetu amejikuta katika wakati mgumu baada ya stori kutoka kwamba yeye na mume wa shoga yake Irene Uwoya ambaye amewahi kukaririwa akimuita shemeji kudaiwa kubanjuka.

Mange Kimambi ameripoti kuwa Wema na Dogo Janja walifanya mapenzi wakati Dogo Janja yupo na Uwoya.

Mange ameweka wazi kuwa alipata taarifa za Wema na Dogo Janja kufanya yao siku chache zilizopita lakini kwa kuwa anampenda Dogo Janja akaamua kumpotezea na hata kumtafuta na kumtaka kuhandle privately.

Lakini baada ya kutibuana na Wema jana Mange aliamua kumwaga ubuyu huo ambapo Mange amedai Wema ndiye alimuomba unyumba Dogo Janja.

 

Baada ya kuweka sakata hilo wazi Uwoya alionekana kumshukuru Mange kwa kumpa taarifa hiyo kwani tayari ndoa yake na Dogo Janja imekuwa  ikionekana kusuasua.