Alichoapa Ray C kufwatia kifo cha Dogo Mfaume kutokana na dawa za kulevya

Ray C ako na uhakika kuwa akirudi kutumia dawa za kulevya atakufa bila shaka. Mwimbaji huyo alisema hayo akiongelea vifo vya wasanii walioago kutokana na matumizi ya dawa za kulevya.

Mrembo huyo haswa aliongelea kifo cha Dogo Mfaume, alisema kama bado hajapata somo kutokana na kifo cha Mfaume basi akipita tena ile barabara kitakachofata ni kifo chake.

Dogo Mfaume

Ray C aliapa kutorejea kwenye matumizi ya dawa za kulevya, alisema maamuzi ya kubadili mwendeno wa maisha yake ni yeye wenyewe.

“Kuna Muda nakaa na kujiuliza barabara ilikuwa na mvua kubwa sana na ukungu sana kiasi cha kushindwa kabisa kuona mbele!!!!Mbele magari mengine nayo yalitaabika KuFocus!La mbele kabisa alikuwamo Langa bahati mbaya lilipotea,Nyuma yake kulikuwa na la Ngwea Nalo pia lilitokomea mojakwamoja angali naliona,Hata la Whitney pia alieweza kukodi hata ndege lakini nae alipita hiyohiyo barabara na hakufanikiwa kupita!Na hili nalo la Mfaume limeenda zake sababu ni ileile ya balaa la mvua kubwa inayotishia Maisha….

“Najiuliza kwanini Mimi niwe hai Leo na barabara tuliipita wote na ni ileile ya kutisha!!Kama sijalipata somo mpaka sasa basi nikiipita tena ile barabara kitakachofata ni Kifo…………

“Ya Mungu ni makubwa mno tena Sana,Na kila sababu ya kusema Asante Mungu wangu……Ingawa njia yetu ni moja lakini Maamuzi ya kubadili mwendeno Wa Maisha yetu ni sisi wenyewe……..

“Ewe Ndugu unaetaabika Amua sasa……Sema No To Drugs.” Aliandika Ray C.