Ebitoke Amefungukia Tuhuma za Kuiba Mume wa Mama Ashura

Mchekeshaji maarufu kutoka Timamu Tv Ebitoke amefungukia tuhuma ambazo zimekuwa zikimuandama kwa muda sasa kuwa yeye na mchekeshaji mwenzake Mama Ashura wana bifu baada ya kumuibia mume.

Ebitoke  alijipatia umaarufu siku za nyuma Kutokana na vituko vyake na make up yake ya sioni ameongelea habari ambazo zinaongelewa sana mtandaoni kuwa ameiba mume wa Mama Ashura ambaye amezaa naye.

Miezi michache iliyopita Mange Kimambi alivunja bonge la habari iliyowashangaza watu wengi kuwa Ebitoke anamchukua mume wa Mama Ashura ambaye pia ni Bosi wao anayewasimamia kazi zao pale Timamu Tv.

Pia ilisemekana kuwa tangu Ebitoke amchukue mume wa Mama Ashura wamekuwa kwenye bifu kali na pia ilisemekana kuwa Mama Ashura amekuwa akiteswa sana na mwanaume huyo.

Tangu taarifa hizi zienee Mama Ashura amekuwa haonekani Tena kwenye mitandao ya kijamii kama zamani na kuna hata taarifa kuwa hivi sasa mrefu kuzaa hapo Timamu Tv.

Ebitoke alifanya Interview na Millard Ayo Tv ambazo alipoulizwa kuhusu ishu yake ya Kumuona mume wa Mama Ashura alikataa kata kata kujibu tuhuma hizo:

Bwana hayo mambo mi sitaki kuyaongelea yaani ukiniuliza kuhusu huyo mtu sina cha kujibu lakini yupo tu mbona sema sitaki kumuongelea kabisa”.

Hata Ebitoke alivyobanwa na ndugu mtangazaji aeleze Mama Ashura alipo alikata kuendelea kufanya Interview na kuondoka.

Ebitoke Akumbwa Na Tuhuma za Kuiba Mume wa Mama Ashura

Msanii wa maigizo ya vichekesho nchini kutokea katika kundi la timamu Ebitoke  ametuhumiwa kuhusishwa na kuvunjika kwa ndoa ya msanii mwenzie Mama Ashura wa kundi hilohilo kwa kutembea na mume wake.Tuhuma hizo ziliibuka juzi kati mbaada ya mwana harakati Mange Kimambi kuamua kusema siri hiyo ambayo ilikuwa imejificha kwa  muda mrefu na kutoa hadi video zinazomuonyesha Mama Ashura akiwa barabarani na mtoto wake wa kiume wakiangaika baada ya kufukuzwa katika nyumba hiyo.

Ebitoke anaedaiwa kuwa alikuwa akikaa kwenye nyumba ya Mama Ashura na mume kwa muda kidogo ikiwa ni kama kumsaidia mahali pa kuishi aliamua kumgeuzia kibao shoga yake huyo na kutembea na mume wake ambae pia ndio meneja wa kazi zao za uchekeshaji.

Mpaka sasa inavyosemekana ni kwamba baada ya Mama Ashura kufukuzwa katika nyumba aliyokuwa akiishi na mumewe, Ebitoke ndio amekuwa mama mwenye nyumba hiyo na kumuacha rafiki yake akiangaika na mtoto barabarani.

Tetesi hizo zinadai kuwa hata baada ya Mama Ashura kufukuzwa , hakuruhuiswa kuondoka na kitu chochote na kwamba hata akaunti zao za mitandao ya kijamii meneja wao huyo ndie anaezimiliki hivyo hawajui hata neno la siri la kuingilia katika akaunti zao.

Ni kawaida kwa wasanii bongo kupinduana na kuchukuliana mabwana  hata kama wawili hao wanakuwa ni marafii sana, na hii inafanya kuharibu kazi zao na mahusiano yao mazuri katika kazi yanakuwa yanaishia hapo .

 

Ebitoke Aongelea Kuhusu Ukimya Wake

Alipoanza kujulikana katika tasnia ya sana alikuwa ni moja ya wasanii wasioisha kutajwa midomoni mwa watu lakini hivi karibuni ameonekana kupoa kidogo , badhi ya mashabiki wameanza kusema kuwa labda na yeye amefulia na zile kiki  alizokuwa anatafuta zimekwisha lakini msanii huyo wa maigizo ya vichekesho kwa jina la Anastazia Xavery akijulikana kwa jina  maarufu la Ebitoke amekana swala hilo na kusema kuwa yupo sana katika game na wala hategemei kuacha kazi yake kwa sabau ni kipaji alichozaliwa nacho.

Ebitoke amesema kuwa tangu amezaliwa, amezaliwa kwa ajili ya kazi ya kuchekesha kwaiyo ni kitu kilichopo katika damu yake na hawezi kuacha na kwa sasa ana madude mengi ya hatari bado hajayaonesha  ila anaomba watu wamvumilie kwa sababu amekuwa akitingwa na majukumu ya hapa na pale lakini ataibuka hivi karibuni.

ha! ha! haa!  mimi sio rahisi kupotea kihivyo kama watu  mnavyofikiria aisee, niko na madude mengi sana ya hatari  bado sijayaachia, sema kuna baaadhi ya majukumu ya kikazi kwa sasa ninayafanya.-Alifunguka Ebitoke

juzi juzi katika moja ya majukwaa ya matamasha ya fiesta ambalo hivi karibuni linafikia ukingoni Ebitoke alionekana katika jukwaa akiwa na msanii Ben Pol wakiombana na msamaha na kutangaza kusameheana na kurudiana hivyo zile tetesi za kuwa wameachana kufutika tena masikioni pa watu ambapo kwa muda kidogo wawili hao walionekana kuwa mbalimbali na kusemekana kuwa walikuwa wamegombana.

Ingawa Ben Pol mwenyewe amekuwa akikanusha habari za kuwa na mahusianao na mwanadada huyo lakini Ebitoke kila siku amekuwa akisema anampenda sana Ben Pol.

Napenda Mwanamke Anayejiamini- Ben Pol

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Bernad Paulo maarufu kama Ben Pol amefunguka kuhusu aina ya mwanamke anayempenda. Mwana muziki huyo amekuwa katika vichwa vya habari sana kutokana na kutajwa na mchekeshaji maarufu Anastazia Kisaveli ‘Ebitoke’.

Ebitoke amemtaja mara kwa mara kwamba anampenda kimapenzi Ben Pol lakini kijana huyo amepotezea. Katika mahojiano yake aliyoyafanya hivi karibuni Ben Pol aliweka wazi kuwa hana muda wa kumuongelea Ebitoke kwani kulitokea mvurugano baada ya Meneja wa Ebitoke kutoka Timamu tv kudai kuwa alimlipa Ben Pol kiasi cha shilingi milioni tatu ili tu aonekane na Ebitoke katika mitandao ya kijamii lakini Ben Pol amekataa tuhuma hizo.

Ben Pol ameweka wazi kuwa kitu pekee anachoangalia kwa mwanamke ili awe naye kimapenzi ni lazima awe najiamini pindi wanapokuwa kwenye maongezi.

“Endapo nikimpenda msichana kitu kikubwa ninachoangalia ni ‘confidence’ yake hasa pindi tukiwa tunachat, usmart, umakini na uharaka wa kujibu vitu unavyokuwa unaulizwa kwa wakati huo”.

Ben Pol ni moja kati ya wanamuzi wanaopendwa sana na wadada yaani mashabiki wake wengi ni wasichana kutokana na aina ya muziki anayoimba hata pia na muonekano wake . Hivi sasa Ben Pol anatamba na nyimbo yake mpya inayoitwa kidume aliyomshirikisha mwanamuziki kutoka Nigeria inayofanya vizuri sana katika stesheni nyingi za redio nchini.

Ebitoke: Mimi na Ben Pol sasa hivi tunafanya vitu vya ndani kwa ndani

Siku chache zilizopita, Ben Pol alisema kuwa hataki aulizwe kuhusu mahusiano yake na mchekeshaji Ebitoke. Msanii huyo alieleza kuwa anajiusisha na mambo ya muziki kwa sasa na hangependa kuongelea mambo yake binafsi.

Ebitoke amedhibitisha kuwa yeye na Ben Pol bado ni wapenzi ila hawataki tu kuweka mapenzi yao hadharani. Akiongea na Times FM, Ebitoke alisema mipango walionayo kwa sasa ndio inapelekea kutoonekana pamoja kwa sasa na kupostiana kwenye mitandao ya kijamii.

Ben Pol na Ebitoke

“Mimi na Ben Pol sasa hivi tunafanya vitu vya ndani kwa ndani, hatutaki tuviweke hadharani. Hamna siyo vya unyago na siwezi kumuongelea vibaya Bentoke labda watu wanaona haniposti mimi kila siku lakini si hivyo. Tunamipango mingi, kwanza kufanya kazi pamoja na kushirikiana katika jambo lolote na ameniaidi lazima ahakikishe natimiza malengo yangu na ameona mimi bado ni mdogo ananifundisha kila kitu jinsi gani nikue kwenye hii tasnia na the way hii mitandao ya kijamii ilivyo na maneno ya watu yalivyo,” alisema Ebitoke.

 

Mchekeshaji Ebitoke afunguka kuhusu Ben Pol kushindwa kumuondoa ubikira

Mchekeshaji wa kike Ebitoke alipata umaarufu sana miezi michache zilizopita alipolia kwenye mahojiano kwa TV huku akitaka msanii Ben Pol afunge naye ndoa.

Ebitoke alisema anampenda sana Ben Pol na hata alitaka mwimbaji huyo amuondolee ubikira wake. Alisema alikua tayari kufanya lolote ili Ben Pol ampende.

Soma pia: Ben Pol amjibu mchekeshaji aliyelia na kumwomba amuoe

Ben Pol na Ebitoke hatimaye walikutana na kwa sasa inasemekana kuwa wawili hao ni wapenzi. Akiongea kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) ya EATV, Ebitoke alisema kuwa Ben Pol hajafanikiwa ‘kufungua mlango wake’.

Ben Pol na Ebitoke

Mchekeshaji huyo alieleza kuwa bado hajawahi kulala na mwanaume yoyote yule katika maisha yake na alitaka Ben Pol ndo awe mwanaume wa kwanza kulala naye.

Hata hivyo kuna wale wanaodai kuwa Ben Pol na Ebitoke wanafanya tu utani ilhali wanazidi tu kujitangaza na kuzidi kupata kiki katika kazi zao.

 

Ebitoke: Sijampenda Ben Pol kisa nimpe ubikira yangu

Mchekeshaji wa kike Ebitoke aligonga vichwa vya habari kwa kusema kuwa anampenda sana Ben Pol na anataka mwimbaji huyo amoe.

Ebitoke alifungua roho katika mahojiano na Sasa TV na kueleza jinsi anavyompenda Ben Pol, machozi yalimchuruzika usoni mchekeshaji huyo akieleza jinsi anavyompenda Ben Pol.

Soma Pia: Ben Pol amjibu mchekeshaji aliyelia na kumwomba amuoe

Ebitoke

Katika mahojiano na Juma3tata, Ebitoke alifunguka kuhusu kumpea Ben Pol ubikira wake. Alisema kuwa lazima mwimbaji huyo amoe kwanza ndo ampe ubikira wake.

“Napenda watu waelewe kitu kimoja, mimi sijampenda Ben Pol kisa nimpe bikira yangu, kwa mfano akikataa kunioa basi nitamwacha aendelee na familia yake, kwa sababu watu wanaongea kinoma, lakini kuhusu hilo nitaendelea kujituza mpaka mwanaume wa kweli atokee kwenye maisha yangu ndiyo nitampa bikira yangu,” Ebitoke alisema.

Ben Pol amjibu mchekeshaji aliyelia na kumwomba amuoe

Mchekeshaji wa kike Ebitoke anampenda Pel Pol kwa dhati, alilia akifanya mahojiano huku akimwomba Ben Pol amuoe.

Ebitoke alifungua roho katika mahojiano na Sasa TV na kueleza jinsi anavyompenda Ben Pol, alisema ishu ya Ben Pol kuwa na mtoto ilimuuma sana kwasababu alikua anadhani ako na bibi.

https://www.youtube.com/watch?v=h_cKUc2TVgQ

Ben Pol amemjibu Ebitoke, anataka kukutane naye uso kwa uso ili kudhibitisha kama mchekeshaji huyo anamaanisha anachosema ama ni utani tu.

“Kwanza niseme tuu naheshimu hisia za kila mtu yeye ni binadamu na ameonesha hisia zake soo naziheshimu sana. Kweli nimeziona habari mitandaoni tuu tangia jana watu wakiposti lakini sikuamini siunajua habari za mitandao bro! ila leo pia nimeona video yake akisisitiza ombi lake lakini bado siamini na nitaamini na nitafurahi kama tukionana uso kwa uso,” alisema Ben Pol.