Esha Buheti alifungua mtoto wa kike

Esha Buheti ndio mama mpya bongo baada ya kujifungua mtoto wa kike leo. Muigizaji huyo wa filamu za bongo amebarikiwa na mtoto siku kadhaa baada ya Linah, Faiza Ally na Hamisa Mobetto kujifungua salama.

Kulingana na habari zinazoenea, Esha alijifungua Latina hospitali ya Sali International iliyopo ushuani Masaki.

Kama wenzake Esha alithibitisha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kupost picha ya mtoto wake chake na kuandika;

“Alhamdullilah ni mtoto wa kike, asante Mungu kwa zawadi hii, asanteni wote kwa dua zenu mimi na mtoto tupo salama.”